Wanaokumbuka hadithi za utotoni...wanakumbuka hadithi ya kuwa paka ana roho saba
na kwa kuwa ana roho saba basi ukijaribu kumuua unashangaa anaibuka tena akiwa hai..
Unaweza mlinganisha Waziri Muhongo na hadithi za paka wenye roho saba...
Kila ikitokea scandal ya kutosha kumtimua Waziri Muhongo..'upepo' unabadilika
'anabaki ana dunda tu'
Kwanza kuna scandal maarufu ya Escrow...licha ya kuwa imerudi tena
na tunatakiwa kulipa tena mabilioni..Waziri Muhongo utasema sio yeye
alieishupalia huko nyuma kuwa yale mabilioni ni halali kuyalipa
Scandal ya Flow meter bandarini....baada ya waziri mkuu kuvamia bandarini
akatajiwa ni waziri gani alihusika na suala zima la scandal hiyo ya flow meter..
'upepo' ukapita....Waziri Muhongo ana dunda...
Likaja la Dangote ...na uzushi kuwa anataka gesi bure....na kauli za kushangaza
na kitendo cha Waziri Muhongo kuwa bega kwa bega na washindani wa Dangote
na kutokea sintofahamu za kila aina..hadi Dangote alipoenda Ikulu
ndo 'yakaisha'...still Muhongo ..;ana dunda tu'
Ndo likaja hili la 'kupandisha bei ya umeme'...ambalo ushahidi uko wazi wizara
ilikuwa inajua 'mchakato wote toka february 2016...hadi juzi...
na hata sababu za Tanesco kupandisha bei....ikiwemo ya Tanesco
kuingiliwa maamuzi na kulazimishwa kupunguza bei na kuondoa 'service charge'
maamuzi ya kisiasa ambayo source ni waziri Muhongo....
Sasa badala ya Magufuli kumtimua waziri Muhongo kwa kusababisha hiyo mess
Magufuli anakuja kumtimua Mramba ambae maamuzi mengi kama sio yote
yalianzia kwa 'orders' za waziri Muhongo.......
Muhongo huyu huyu ambae kila mara anaongea kwa uwazi kabisa kuwa
Tanesco iache kuzalisha....iwe inanuanua umeme kwa asilimia 100
wakati anajua kuwa Tanesco inanunua kwa bei ya juu kuliko inavyouza
kwa umeme huo ambao inanunua ambao bado ni aslimia chini ya 50
sasa je iwapo itanunua kwa asilimia 100...watapataje faida?
kama asilimia chini ya 50 tu wanategemea ruzuku serikalini?
Huyo ndo Muhongo.....ije mvua lije jua....Magufuli anamuamini na kumsikiliza
na hata kumpongeza kwa maamuzi yake yanayoleta 'utata' kila sehemu
kuanzia kwenye gesi,umeme,vitalu vya gesi,madini na kila anachokigusa..
Kweli hadithi za utotoni za paka kuwa na roho saba...hazikuwa burudani tu ya kufurahisha
genge......
Wa kanda huyo mwenzetu hawezi kuondolewa........jibu liko wazi hakuna kuuliza