Muhongo atoroka!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,153
Reaction score
162,570
  • Hii habari ni kweli au ni kutaka tu kuuza gazeti?
  • Sitashangaa gazeti hili likijikuta linatakiwa kumuomba radhi Muhongo
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, hajaonekana bungeni jijini Dodoma bila ruhusa ya Spika tangu uteuzi wake katika baraza la mawaziri utenguliwe wiki tano zilizopita.

Mei 24, mwaka huu, Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Prof. Muhongo katika baraza la mawaziri, ikiwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya kwanza ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu (Makinikia).

Hata hivyo, uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa mtaalamu huyo wa Jiolojia wa kimataifa hakuwapo bungeni wakati uteuzi wake wa uwaziri ukitenguliwa, huku taarifa zikidai alirudi nyumbani kwao, Musoma mkoani Mara, kuhudhuria mazishi ya dada yake.

Simu ya Prof. Muhongo iliita bila kupokewa alipotafutwa na Nipashe kwa siku tofauti, ikiwamo jana, kuzungumza sababu za utoro bungeni.

Kutokana na kutoonekana bungeni kwa Prof. Muhongo, Nipashe jana ilizungumza na Katibu wa Bunge kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Dk. Thomas Kashililah, ambaye alisema ofisi yake haina taarifa za Mbunge huyo wa Musoma Vijijini (CCM) jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu.

Kiongozi huyo wa Bunge pia alisema ofisi yake haijui aliko tangu alipoachishwa nafasi ya uwaziri mwishoni mwa mwezi uliopita.

Dk. Kashililah aliongeza kuwa kwa kawaida mbunge anapokuwa na udhuru, humwandikia Spika kumwelezea hatakuwa bungeni kwa muda fulani na ofisi ya Katibu wa Bunge hupewa nakala.

"Sijapata nakala yoyote ya udhuru wa Profesa Muhongo na wala sijui alipo tangu siku ile", alisema Dk. Kashililah.


Katibu wa Bunge huyo alisema hii ni mara ya pili kwa Muhongo kuondoka bungeni kwa muda mrefu bila ya ruhusa kwani hata alipomwandikia barua ya kujiuzulu Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete, hakuhudhuria Bunge kwa muda mrefu.

Prof. Muhongo alijiuzulu nafasi ya Waziri wa Nishati na Madini Januari 24, 2015 kwa shinikizo la Bunge, kutokana na taarifa ya Kamati moja ya chombo hicho juu ya kashfa ya uchotwaji fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.


Chanzo: Nipashe
 
Tufanyeje ili uzalendo wa zamani uturudie tuache kushabikia yasiyojenga nchi? Tumewapa nguvu sana Mawaziri tukasahau bunge! Haiwezekani tulie na Waziri tuu,wakati mambo yote anayotenda yanajadiliwa na kupata baraka za bunge. Kwa nini waliompa baraka wasikimbie akimbie yeye? Ninajua kuna sheria inamruhusu kuamu jambo,lakini hiyo sheria pia hiyo sheria imetungwa na kupitishwa na wabunge. Nanashauri bunge liongeze ufanisi.
 
Muhongo anajuta kurudi nchini angejua.......lakini ninge ange.....ni majuto mjukuuu!!!
 
Muhongo anajuta kurudi nchini angejua.......lakini ninge ange.....ni majuto mjukuuu!!!
Nje hapakuwa na hela ya kuzoa kama hapa! ya bure, heshima, utukufu, kuwalingia wakoma uliowaacha nyuma etc! Lise wise Tibaijuka!
 
Nipashe ni la Mengi.. Linatumika kumchafua Muhongo
 
Gazeti lenyewe nipashe sishangai kilichoandikwa humo na sio mara ya kwanza kumwandika vibaya profesa wa ukweli ila suala la uwemezaji kwa wawekezaji WA kibongo bado sana
 
Muhongo angejifunza kwa Masilingi enzi za kubinafishwa kwa Kilimanjaro Hotel
Vurugu na Mume wa K-Lyn havijawahi kumuacha mtu salama.

Ile Mengi kuambiwa ana mtaji wa kuwekeza kwenye juice na maji ya kufunga ilimuuma sana.Muhongo atajuta,hawa Maprofesa sijui huwa wanafuata nini kwenye siasa
 
Tatizo la Mhongo ni kukariri yale ya darasani halafu anashindwa kuhusianisha na yale ya uhalisia wa maisha ya kila siku ya watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…