Muhimbili wajivunia ubora Kurugenzi ya upasuaji

esther mashiker

JF-Expert Member
May 29, 2018
616
552
1579410758435.png

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH), inajivunia ubora unaotolewa katika Kurugenzi ya Upasuaji kwa kuongeza huduma nyingi pamoja na ubora wa mashine za kisasa ambapo wameokoa fedha nyingi kama Watanzania wangefuata huduma hiyo nje ya Nchi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa huduma za upasuaji, Dk Sufian Baruani alisema kwa kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya tano wameweza kufanya mambo mbalimbali ikiwemo upanuzi wa vyumba, ununuzi wa vifaa vipya zikiwemo mashine za kisasa pamoja na kuongeza wataalam wa kibingwa. “Hospitali ya Taifa Muhimbili tumefanya upanuzi wa vyumba vya upasuaji kutoka 11 hadi 20 na tumepunguza wagonjwa kukaa muda mrefu kusubiria huduma hii.

Awali muda ulikuwa hadi wiki sita hadi nane, kwa mfano idara ya watoto hivi sasa muda umepungua hadi wiki mbili,” alisema Dk Baruani.

Kuhusu kuongeza huduma, alisema waliweza kuanzisha huduma ya kupandikiza vifaa vya usikivu na kuweza kuwafanyia wagonjwa 34 na kugharimu Sh bilioni 1.2. Alisema ili kuhakikisha huduma zinakuwa bora zaidi nchini, vifaa mbalimbali vimeagizwa na kuwa vitakuwa msaada kwa Taifa katika uboreshaji wa huduma. “Tumeagiza vifaa vyenye thamani ya Sh milioni 800 kwa ajili ya upasuaji wa matundu madogo. Pia tumeagiza vifaa vya Sh milioni 700 ili kuboresha huduma za macho.

Vifaa hivi ni kwa ajili ya kupima matatizo mbalimbali ya macho pamoja na vifaa vya kutengeneza miwani,” alisema Dk Baruani. Aliongeza kuwa katika huduma ya tezi dume, wameshanunua mashine ya kisasa yenye thamani ya Sh milioni 70 ambayo itasaidia kuchukulia vipimo vya tatizo hilo na kununua vifaa vya maabara vya kutengeneza meno ya bandia.

Alisema huduma hizo za matibabu za uvimbe wa taya (Haemangioma) kwa kutumia mionzi yaani interventional radiology na tangu mwaka 2017 hadi sasa wagonjwa 302 wamehudumiwa kwa gharama nafuu ya milioni nane kwa kila mgonjwa na endapo wangeenda nje ya nchi ingegharimu Sh milioni 100 kwa mgonjwa mmoja.
 
Gharama ya milioni nane kwa mgonjwa si ndogo.

By the way kama vifaa hivi vinanunuliwa na serikali na majengo ni mali ya serikali vyote vikiwa ni kodi ya wananchi na hali kadhalika mishahara. Mtupe na breakdown ya hizi gharama za milioni nane ni kuhusiana na nini.

In Magu's words: 'watanzania wa leo si wajinga kihivyo' kuambiwa ambiwa tu. Tupeni breakdown vinginevyo maelezo yote hayo ni kama taarab tu.
 
Milioni nane si hela ndogo kwa mgnojwa mmoja. Bado gharama za matibabu ni kubwa sana nchini kwetu. Kwa hela hiyo, ni Watanzania wanagpai watumuda gharama hizo. Na unawezaambia Bima ya Afya haihusiki katika kugharamia matibabu kama hayo!
 
Huku ni kujibaraguza kufunika ile kashfa ya Mloganzila na hapo Muhimbili
Mkuu wewe Una Akili sana sana sana Mkuu,Sijui Kila MTU analiona hili ulilolisema?
Natamani Mkuu Uandike tena,mi Wiki iliopita Nimepoteza ndugu yangu pale,Aligongwa na Gari lakini alikuwa Anafahamu na Kula kwa Muda wa Siku 3,
Yaani Kuanzisha faili tuu SAA nzima,Mwisho wakaamua Kumpeleka Muhimbilli,Sasa Kutafuta Ambulance Massa 2,kutafuta Sijui Dawa,yaani Acha tuu,Alifanikiwa Kwenda Moii na Alifia Moii! baada ya Siku 3.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli bila Wanasiasa na Siasa maisha yetu hayawezi kwenda. Taasisi kubwa kama hii haiwezi kupanga (haiko huru) na kufanya maendeleo kwenye taasisi bila ridhaa ya wanasiasa. Usikute hata huyu Mkurugenzi anachaguliwa na Rais?
 
Ukisikiliza vyombo vya habari ndo utajua kuwa wananchi wengi wanakosa matibabu kwa sababu ya gharama. Leo asubuhi kuna mama alikuwa Radio Free Africa- Mwanza anaomba msaada wa kutibiwa mtoto wake ambaye ana matatizo ya moyo. Kwa kweli ukisikia anavyoeleza lazima utatokwa na machozi. Bugando wamemweleza kutibu maradhi hayo n milioni 8. Lakini mama anasema wanaishi maisha magumu hawezipata hela hiyo labda achangiwe na wasaramia wema. Huyo ni yule aliyemudu kufika RFA , je, huko Vijijini hali ikoje!
 
Back
Top Bottom