maroon7
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 11,341
- 15,842
Wakuu nimekutana na habari hii kutoka gazeti la The citizen kuhusu maabara ya kisasa iliyogharimu zaidi ya Tsh 2 Billion kwa ufadhili kutoka Uturuki lakini cha kusikitisha inamiaka karibu miwili eti bila matumizi na badala yake sampuli zinapelekwa India licha ya maabara hiyo kutoa majibu sawasawa na yale ya India.
Tena bila aibu viongozi wa Muhimbili wanasema kabisa sample kupelekwa kwenye hiyo maabara na nyingine inapelekwa India na majibu kurudi yaleyale. Mtaalam kutoka Uturuki Prof Fatmahan Atalar ambae anasimamia mradi huo kuhakikisha wataalamu wetu wanajua kutumia maabara hiyo amelalamika hali ya kushangaza ya wataalamu wetu kukwepa kabisa kujifunza na kutumia maabara hiyo achilia mbali kupeleka tu sampuli hapo licha za juhudi zake binafsi kuzunguka idara zote kuwahamasisha lakini wote wanakacha.
Cha kushangaza zaidi hata reagents tu kuhudumia hiyo maabara hawataki kununua hali iliyopelekea mtaalam huyo kutoka Uturuki kutumia pesa yake binafsi kiasi cha shilingi milioni 140 ambazo aliahidiwa kurudishiwa lakini kapigwa changa la macho.
Maabara hiyo ya aina yake inaweza kuokoa maisha ya watu wengi afrika mashariki na kati kwa mujibu wa Prof huyo.
My Take; Waziri wa afya anapaswa kutoa tamko juu ya nini hasa kimepelekea hii hali na kwanini baada ya The citizen kuanika hii ndio waseme sasa wataanza kuitumia?
Pili uwezo wao wa akili na shule zao upimwe kwanini wakimbie mitini hata kujifunza tu kama shule zao sio za magumashi?
Mwisho ikiwezekana wakapimwe mkojo igundulike kama kuna vitu wanatumia vinavyodhoofisha uwezo wao wa kufikiri.
Sh2 billion lab stands idle for nearly 2 years