Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Wakuu nilikuwa napitia pitia katika blogu mbalimbali nikabahatika kuangukia kwa inayoitwa blogu ya jamii ya Muhidini Issa Michuzi. Nimeshangazwa na habari picha nilizoziona zikionyesha mikutano ya kampeni ya chama cha upinzani chadema huku baadhi ya picha zikiwa na ujumbe wa bango la chama tawala. Nionavyo hapa blogu ya jamii imekiuka maadili ya uandishi kwa makusudi.
Maana kwa kufanya hivyo ni sawa na habari ile kuwa inapotosha mtazamaji/msomaji wake. Ujumbe wake hauendani na taswira inayoonekana au mwandishi alivyokusudia.
Picha inaonyesha kampeni za chadema sehumu kubwa ya picha hiyo imetolewa bango la CCM, huu si upotoshwaji wa makusudi na kukiuka maadili ya kihabari yanayotaka habari isipotoshe umma kwa muonekano wake ama kwa ujumbe wake?
Mimi si mwandishi/mpiga picha ila najuwa kuwa hakukuwa na ulazima kwa blogu ya jamii kupiga picha zile kwa namna ile huku wakijuwa kuwa haitaleta tafsiri sawa, vinginenvyo niamini kuwa imefanywa makusudi kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wapinzani na kampeni zao, kwa kuipendelea CCM!
Picha, kwa wataalamu wanajuwa, kuwa inaweza kupigwa ama horizontal, aerial or oblique...na angle zote hizo unaweza kuepuka object ambayo hutaki itokee katika picha, tuseme Michuzi hafahamu hili au anafanya makusudi uhuni huu?
Kama blogu ya jamii inaona kero kuweka picha za vyama vya upinzani si wasiweke tu, kwani nani anawalazimisha waweke kihuni huni kama vile?
Hivi Michuzi akiambiwa anaipendelea CCM ndiyo anafanya inadi na inda kwa kufanya uhuni wake kama vile!
Michuzi haoni haya kuwa anajishusha kikazi kwa kuweka picha zenye ujumbe wa kupotosha kama zile?
Wapenda mageuzi na maadili ya uandishi wanapaswa kulani uhuni huu wa golobu ya jamii ya kupotosha kwa makusudi maadili ya picha za kihabari na uandishi kwa ujumla.http://www.issamichuzi.blogspot.com/
Maana kwa kufanya hivyo ni sawa na habari ile kuwa inapotosha mtazamaji/msomaji wake. Ujumbe wake hauendani na taswira inayoonekana au mwandishi alivyokusudia.
Picha inaonyesha kampeni za chadema sehumu kubwa ya picha hiyo imetolewa bango la CCM, huu si upotoshwaji wa makusudi na kukiuka maadili ya kihabari yanayotaka habari isipotoshe umma kwa muonekano wake ama kwa ujumbe wake?
Mimi si mwandishi/mpiga picha ila najuwa kuwa hakukuwa na ulazima kwa blogu ya jamii kupiga picha zile kwa namna ile huku wakijuwa kuwa haitaleta tafsiri sawa, vinginenvyo niamini kuwa imefanywa makusudi kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wapinzani na kampeni zao, kwa kuipendelea CCM!
Picha, kwa wataalamu wanajuwa, kuwa inaweza kupigwa ama horizontal, aerial or oblique...na angle zote hizo unaweza kuepuka object ambayo hutaki itokee katika picha, tuseme Michuzi hafahamu hili au anafanya makusudi uhuni huu?
Kama blogu ya jamii inaona kero kuweka picha za vyama vya upinzani si wasiweke tu, kwani nani anawalazimisha waweke kihuni huni kama vile?
Hivi Michuzi akiambiwa anaipendelea CCM ndiyo anafanya inadi na inda kwa kufanya uhuni wake kama vile!
Michuzi haoni haya kuwa anajishusha kikazi kwa kuweka picha zenye ujumbe wa kupotosha kama zile?
Wapenda mageuzi na maadili ya uandishi wanapaswa kulani uhuni huu wa golobu ya jamii ya kupotosha kwa makusudi maadili ya picha za kihabari na uandishi kwa ujumla.http://www.issamichuzi.blogspot.com/