Muendelezo Vita Dawa ya Kulevya: Masogange apelekwa kwa Mkemia Mkuu

Unavyoelezea 'random sampling' na maana ya ''random sampling' haviendani mkuu.
Iweke sawa kamanda mimi siyo mtu wa Statistics.Uko sahihi ilitakiwa niliwekee hizo ".. "Sikumaanisha pure random sampling lakini ujumbe unefika ...
 
Sisi hatuhitaji hao wake wa Makonda. Bali wale wasambazaji huu ni uwajibikaji au kuharibu tu sifa ya watanzania. Ni sawa na wanakamata makokoro badala ya kiwanda. Halafu mnajisifia mmefanya kazi.
 
Hivi hii vita ilenga watumiaji wa dawa za kulevya? Au wauzaji wa dawa za kulevya ?? Mbona kama serikali imebadilisha gear angani
 
Hii ni episode ya nne kwenye hii series au hii ni season 4 nielewesheni jamani. Halafu series hii na Ile ya hashishi ni the same au ndiyo ile ile maana series ni nyingi mpaka zinanichanganya.
 
Kama ni vipimo vya mkemia mkuu kubaini wasafirishaji,watumiaji na wauzaji ,basi lifanyike zoezi la upimaji wananchi wote ili kukomesha ishu hii.
 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Simon Sirro amesema mtuhumiwa Agness Gerald, maarufu Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuchukua vipimo vya damu ili kubaini kama anatumia dawa za kulevya.



Masogange ambaye ni mrembo maarufu anayetamba katika video za wasanii mbalimbali wa bongo fleva alikamatwa na polisi juzi.

Kamishna Sirro amewaambia wanahabari leo kuwa Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali na kwamba majibu yakipatikana kesho atafikishwa mahakamani

"Tunamchunguza Masogange katika mambo matatu ili kujua kama anauza , anatumia au anasafirisha dawa za kulevya, " amesema Kamishna Sirro.

Katika hatua nyingine, Kamishna Sirro amesema watuhumiwa 349 wamekamatwa kwenye operesheni ya kupambana na dawa za kulevya iliyoanza Februari Mosi mwaka huu.


Chanzo: Muungwana

Nachokiona hapa Wale ambao ilibidi tuwashitaki kama wauzaji sasa tunaishia kuwapima ili tuone kama wanatumia. Lile kosa kubwa la kuuza limeshindikana baada ya Serikali kuamua kuifanya waziwazi. Sasa tunaishia kuchunguza kama wanatumia. Tushapoteza target yetu, tunachofanya ni kufanya kama angalau angalau.

Yaani ni sawa na Unamdai au unategemea kulipwa 1,000/= sasa sababu imeshindikana sasa unaangalia usikose japo 100/=. Huyu Agness na wengine pengine wangechunguzwa kimya kimya wangeweza kukutwa na mzigo wa kutosha tu
 
Huu nii utani my dear!

Sisi hatuhitaji kuwajua watumiaji mbona ukipita vituo vya daladala wamejaa wengi tu tena wanabembea bila shida. Ila tunahitaji wakamatwe wauzaji na wasambazaji ili hii biashara ikome kabisa au ipungue maana wanaoumia ni vijana wenzetu na watoto wetu. So wakishampima Masogange akikutwa anatumia watakuwa wamezuia kiasi kuingia kwa madawa hapa nchini?

Huu ni utani uliotukuka!!!
Sasa bila hata hiyo jitihada ya "angalao" kudaka mmojam1, watapunguaje sasa?
Unapochangia, ainisha mbinu unazoona wewe zinafaa kama wangelizitumia. Lakini kubwabwaja bila kuonesha njia unaweza kuonekana kama ni mnufaika flani'iv!
 
Wamuachie haraka, kuendelea kumshikilia huyo ni kutumia vibaya kipozoe cha mioyo ya watu
Huyo hatoki mapema. Kuna watu wanapendezwa nae sana pale sentro. Yaani ni kiburudisho tosha kwa Wazee wa Sentr na kila wakati anatumwa ili watu watizame kikalio
 
For sure dis is very good fight against drugs but other thing nlikuwa naomba serikali igeukie na ushoga kwa spidi hii coz n laana
 
Sasa wanamchunguza Masogange kama anasafirisha dawa za kulevya wakati alishakamatwa akisafirisha????? Halafu miaka yote walikua wapi wakati agnes anakamtwa south Africa???

Kweli hii ndio nchi ya "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA"..

Ndiyo maana Rais Magufuli na Makonda wamejua kuwa viongozi serikalini including polisi, wafanyakazi katika sehemu nyeti za serikali kama Airport uhamiaji mahakimu wanahusika! yaani nchi imeoza kwa rushwa. Nani anajua yule mtoto wa kiongozi angalia website hii www.v2catholic.com ya kule China ya Hong Kong waliodakwa kule China ya Bara na kijana mmoja msanii marufu waliachwaje kuchukuliwa hatua baada ya balozi kuingilia kati na ndiyo maana Rais kapiga 'stop' mabalozi kuingilia kati waache wanyongwe! Kudos President Dr Magufuli, kudos Makonda! aluta continua! Vijana wetu at last wataepuka na janga la madawa ya kulevya.
 
Kuna mahali tunakaribia kupoteana. Tunataka wasambazaji na wauzaji, mbona watumiaji tunao kila kona na wanajulikana waziwazi?


Ndio maana nikauliza ni jinsi gani mkemia mkuu wa serikali hupima na kumgundua msambazaji na mtumiaji. Na hivyo vipimo kama vipo iangaliwe jinsi ya kuwapatia matrafiki. Ukipigwa mkono barabarani pamoja na notification unapiwa kuhusiana na usambazaji au uuzaji wa mihadarati.

Na washawasha!
 
Kwa mkemia mkuu kufanya nini sasa? Yaani sasa tunaishia kutafuta "watumiaji". Kumbe mbwembwe na mikogo yooote bado hatuwajui wauzaji na wasambazi wakuu mpaka leo.
Wauzaji na wasambazaji wanaowajua ni watumiaji. Hivyo logically ukitaka kuwajua na kuwakamata wauzaji na wasambazaji hawa njia nyepesi ni kuanza na watumiaji ambao wako kila mahala na ni rahisi kuwabaini.

Au nalo hili ni ngumu kulielewa? Mkakati ni kuwa wabane barabara hao watumiaji (kwa mateso ikibidi) hadi wataje waliowauzia hayo madawa. Baada ya hapo kawabane sawa sawa hao wauzaji hadi wakutajie hao wasambazaji walikozipata hizo dawa. Baada ya hapo wakamate na kuwabana barabara hao wasambazaji wataje walikozipata hizo dawa. Na endelea hivyo hadi mwisho wa mnyororo (chain) ambao ni viwanda na mashamba yanayozalisha hayo madawa.Viwanda na mashamba haya yako nchi za nje. Kwa hiyo ushirikishaji wa interpol utahitajika kuanzia stage fulani. Kwa hiyo tumeanza na stage 1 ya akina Masogange na akina Manji. We are in the right track my friend, be relaxed. Hawa watumiaji wakishathibitisha walikozipata hizo dawa, wanakuwa upande wa serikali kama mashaidi: hawafungwi jela bali wanaanza kutibiwa na kuwa rehabilitate kuwa raia wema. Wale watumiaji (baada ya kuthibitishwa chemically) ambao watakaidi kuwataja waliowauzia lazima wataipate fresh na wanaweza hata kufungwa jela hadi watakapotoa ushirikiano.
 
nh.jpg
Bg ass

Ova
 
Wanampeleka kuziba kauli za mwana daresalm kumkingia kifua tu hapo jibu ni moja alitumia ila kaacha kes kwisha
 
Back
Top Bottom