Kim nana sio siri nakupenda kijana mwenzio/
niende wapi na wewe ni langu chaguo/
napenda nikuoe unifurie nguo/
wakati wajoto uwe wangu kimbilio/
ukijihisi mpweke mi ni wako ufunguo/
please
Kim nana sikia changu kilio/
nielewe
Kim nana nionee huruma kijana mwenzio/
Usiku
snipa sipati usingizi/
Na kesha kukuwaza changu kipenzi/
Nazidi kumwomba mwenyezi/
unielewe
Kim nana kipenzi/
kijana mwenzio sio siri sijiwezi/
niki ku call unadai umebanwa na kazi/
ooh piga badae badae unaniumiza kipenzi/
any way yote namwachia mwenyezi/
Kim nana hivi unakumbuka?/
ahadi zako zile ulizonipa/
ulisema ikifika leo jibu langu utanipa/
au unafurahi kuniumiza snipa?/
Mbele ya hadhira leo ukweli nakupa/
haya sasa muda umeishafika/
na matatizo yangu bila wewe hayawezi tatulika/
jinsi nnavyokupenda mpaka mistari nimeiandika/
elewa nnavyokupenda wangu malaika/
snipa