Mtwara - Mwaka 2020...??

Mu-Israeli

JF-Expert Member
Mar 21, 2012
2,454
975
Hii ndio Mtwara ya mwaka 2020..??
 

Attachments

  • south03.jpg
    south03.jpg
    154.3 KB · Views: 518
  • south02.jpg
    south02.jpg
    117.9 KB · Views: 398
Mwaka 2020 ni miaka 7 kuanzia sasa na pengine sababu iliyokushawishi kudhani hivyo ni ugunduzi wa mafuta ghafi na gesi huko Mtwara.
Nadhani ndoto kama hizo pia walikuwa nazo wananchi wa Mwadui na Shinyanga kwa ujumla wakati tu Almasi ilipogunduliwa huko.
Sio hao tu bali pia wananchi wa Mererani(wakati huo Arusha), Geita na kwingineko kwenye rasilimali madini.
Hivyo kwangu mimi mada hii naiona kama ni ndoto, ukizingatia ya kwamba sio ndoto zote humuitaji muotaji awe amelala.
 
Dar es salaam imeshindikana kuwa hivyo itawezekanaje Mtwara?

Itawezekana kwani Mtwara haijajengwa sana, hivyo itapangwa na kujengwa vizuri kwa pesa za gesi na mafuta..
BTW, mnajua kuwa, pamoja na gesi, Mtwara kuna mafuta kibao ...??
 
Mwaka 2020 ni miaka 7 kuanzia sasa na pengine sababu iliyokushawishi kudhani hivyo ni ugunduzi wa mafuta ghafi na gesi huko Mtwara.
Nadhani ndoto kama hizo pia walikuwa nazo wananchi wa Mwadui na Shinyanga kwa ujumla wakati tu Almasi ilipogunduliwa huko.
Sio hao tu bali pia wananchi wa Mererani(wakati huo Arusha), Geita na kwingineko kwenye rasilimali madini.
Hivyo kwangu mimi mada hii naiona kama ni ndoto, ukizingatia ya kwamba sio ndoto zote humuitaji muotaji awe amelala.

Kweli, lakini wana-Mtwara wameonyesha uzalendo, sio kama jamaa wa Geita walioacha dhahabu yao inaporwa na wao wanakodoa macho tu..
Mtwara 'usipime' mazee...!!

Mtwara mwaka 2020... itakuwa hivi...!!! Umeziona njia za treni ya umeme pale chini ya barabara ..??

tumblr_m30vk8v58q1rqi3zvo1_1280.jpg
 
Pia tutaandama mtatupotezea na kuharibu mazalio ya Samaki nchanga

Kweli kabisa hapo kwenye blue, ila tutakuwa busy zaidi na fainali za kombe la dunia la mwaka 2026....
Check stadium hiyo ambapo fainali hiyo itapigwa....
Mtwara Olympic stadium...Mashabiki watawasili kwa treni za umeme (umeziona hapo (upande wa kulia) karibu ya uwanja....??)....

Tunaweza Watanzania, tunaweza.....

4_stadium.jpg
 
Itawezekana kwani Mtwara haijajengwa sana, hivyo itapangwa na kujengwa vizuri kwa pesa za gesi na mafuta..
BTW, mnajua kuwa, pamoja na gesi, Mtwara kuna mafuta kibao ...??
Mawazo yako ni mazuri sana ila mipango mingi ya Serikali haifanikiwi kwa kuwa hakuna watu wa kufikiria mbali na kupanga nini kifanyike baada ya miaka kadhaa,wengi hufikiria mipango ya muda mfupi,jiji la Dar es salaam ukiona ramani yake enzi ya mkoloni utaona kuwa walipanga mipango ya muda mrefu tofauti na lilivyo sasa.
Omba Mungu hicho unachodhani kitafanyika ila chukulia mfano wa Nigeria na natumai majibu ya kile unachodhani kitatokea kwa Mtwara,hujavipata hivyo vitu ugomvi umeanza je vikipatikana itakuaje?
 
Mu-Israel naangalia hii hadithi yako halafu narejea kwa wana Mtwara walio katika harakati za kutaka uwazi wa mikataba ya gesi, nahisi wanasukumwa na kiu ya haraka ya maendeleo kwa kua na Taswira hizo!

Miaka 7 ni muda mchache sana kwa miradi mikubwa kama hiyo kutekelezwa. Na itoshe kusema, hiyo michoro sio ya mji wa Mtwara....lakini naheshimu mawazo yako bro!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom