Kwanza kabosa naomba mods mbadilishe title ya hii post ili iendane na jina halisi la my Kiswahili hero.
Namfagilia saaaaan Joram Kiango, penye harufu ya hatari yeye ndo anacheka. Kijana aliyekulia nchini Marekani na kupata mafunzo huko, kisha kuanzisha kampuni binafsi ya upelelezi.
Tafadhali nirusuni niwawekee picha, maana mi ni mshabiki mkubwa wa hizi series. Na nilisikitika sana niliposikia jaam Ben R. Mtobwa amefariki, anyway. Things come and go, seasons change and people as well.
View attachment 75270 Hiki ni political, na ni kizuri kinoma, enzi hizo za uchaguzi wa vyama vingi unapoingia, this guy amejitahidi kuelezea hivyo vyama na waassi wake, then blending it with fiction. Kuwa Kina Inspekta Kombora na jeshi lake wameshindwa kazi, mpaka alipoingia kijana mtanashanti, Joram
View attachment 75271 Arusha ndo imezungumzwa humu, Nharenaro, maasi yanapovuka kiwango na mwasichana flani kuuawa kinyama, muda uleule, sehemu ileile, na polisi aliyeenda kufanya upelelezi anauwawa kwa style ilele. Joram atafanikiwa?
View attachment 75272 Hapa Afrika ndo inaangazwa, hujuma zote wanazofanyiwa, dhuluma na kila kitu, ukombozi ndo njia pekee ya kutoka humo. lakini mashujaa kutoka nchi mbalimbali walipopelekwa, hakuna anayerudi hai, Joramanatazamwa na Ulimwengu mzima, ataweza?
View attachment 75273 Taarifa za kutoka kwenye kikao nyeti cha watu wazito sana na wenye hadhi mtaani na nyadhifa nzito maofisini, wanakubaliana kutofanya chochote mpaka wamuue kwanza Joram, kisa na mkasa?
View attachment 75274 Hapa tuko mwisho wa Reli, Kigomam, Joram alidhani amekwenda mapumzikoni kufaidi samaki wa Ziwa Tanganyika, haikuwa hivyo, abadala yake akajikuta uso kwa uso na mumbe wa mauti.
Nakala zingine kuna watu wamezimisplace, ila hizi copy nikazimisha popote pale ninapohamia. I love them books. Kama kuna mtu ana ambazo sijaweka hapa, tafadhali.
Kwa mara nyingine nasisitiza mods wabadili title ya post, inaniumiza roho kusema ukweli. weka jina sahihi, Joram Kiango, ama ukishindwa sema kabisa Harakati za Joram Kiango.