Mtunza mahesabu vs Muhasibu

Mtunza mahesabu vs Muhasibu

LOVINTAH GYM

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
459
Reaction score
655
BOOK-KEEPING VS ACCOUNTING

Kiufupi Book keeper ni mtunza mahesabu na Accountant ni Muhasibu.



Book keeping na Accounting hufananishwa sana kutokana na vitu vifuatavyo:

1. Zote zinahusika na mambo ya kifedha

2. Lengo ni moja, kukuza upatikanaji wa fedha

3. Zote zinahitaji elimu ya misingi ya uhasibu



Pamoja na yote hayo, bado book keeping ni tofauti na accounting kutokana na vitu vifuatavyo:



1. SCOPE (Upeo)

Accountant yoyote anaweza kuwa book keeper, ila book keeper hawezi kuwa accountant.

Book keeping ni kutunza record zote za kifedha, ila Accounting inaanza pale booking inapoishia.

Accounting itachukua record na kuzitumia kutengeneza report, ambayo itasaidia kujua mwenendo wa biashara.



2. BUSINESS STAGE (Hatua gani ya biashara)

Book keeping ni nzuri hata kwa mtu binafsi kujipima ukuaji wako wa kifedha.

Kama biashara yako ni changa kabisa ni kheri uka download app ambazo zitakusaidia kufanya book keeping.

Kama umekua kiasi unaweza kuajiri mtu ni vyema akamuajiri book keeper na akihitaji msaada zaidi ndio atafute Accountant.

Kama biashara yako inauwezo wa kuajiri watu zaidi ya 30 basi ni vyema ukawa na Book keeper akisaidiana na Accountant.



3. REPORT

Kwenye book keeping ni lazima mtunza mahesabu arekodi kila shughuli za kifedha zinazofanyika kila siku.

Kwa Accountant, yeye huandaa repoti ambazo zitaonyesha shughuli za kifedha zilizofanyika mwaka mzima.



4. GUIDANCE (Muongozo)

Book keeping itasaidia kutoa mapendekezo madogo madogo kujua biashara inavyoenda.

Accounting itakusaidia kutoa mapendekezo makubwa jinsi biashara inavyoenda, na kipi kifanyike ili biashara ikuwe nk.



5. EDUCATION (Elimu)

Book keeper sio lazima awe na elimu ya juu sana, maana ni ku rekodi tu kwa usahihi, mwenendo wa biashara na shughuli zake za kila siku.

Accountant ni lazima asomee maana kuna kuandaa financial report ambazo atahitaji kuzitafsiri zina maanaisha nini na kutoa mapendekezo.



Kwa ukuaji wa Science na Technology, zinasababisha kuwe kuna urahisi wa ufanyaji kazi za kihasibu, ila urahisi wake unasababisha uhitaji wa wahasibu kuwa mchache na book keepers.

Kwahiyo kama unampango wa kuwa Muhasibu ni vyema ukawa unaji update kwa kusoma short course ambazo zinatumika katika uhasibu.

- Tallying ERP

- Xero

- SAP nk



Karibuni kutoa maoni.

#accountant #business #accounting #bookkeeping #technology #uhasibu
 
Mhasibu utamjibuje mtu mwenye mawazo haya? Kuna mfanya biashara mmoja std seven anadharau sana masomo ya biashara, kwake yeye masomo ni sayansi, urubani n.k.
Anaamini ukishajua wapi ukaagize mzigo na uupeleke wapi urudishe fedha na faida inatosha.

"Nimeenda Japan, nimeleta mzigo B2 ukiisha ntapata B 2 na M500 huo uhasibu wa nini? Yaani Mizania ndo iniambie biashara yangu inavyoendelea wakati mm ndo nimeweka pesa hapo na najua kuhesabu pesa? Serikali tu inalazimisha mambo ya ajabu ajabu kupoteza muda shule. Mwanangu amemaliza form four anakata mzigo huko China analipa mhasibu laki sita apeleke hesabu TRA. " huyu unamjibuje tena akiwa keshalewa?
 
Mhasibu utamjibuje mtu mwenye mawazo haya? Kuna mfanya biashara mmoja std seven anadharau sana masomo ya biashara, kwake yeye masomo ni sayansi, urubani n.k.
Anaamini ukishajua wapi ukaagize mzigo na uupeleke wapi urudishe fedha na faida inatosha.

"Nimeenda Japan, nimeleta mzigo B2 ukiisha ntapata B 2 na M500 huo uhasibu wa nini? Yaani Mizania ndo iniambie biashara yangu inavyoendelea wakati mm ndo nimeweka pesa hapo na najua kuhesabu pesa? Serikali tu inalazimisha mambo ya ajabu ajabu kupoteza muda shule. Mwanangu amemaliza form four anakata mzigo huko China analipa mhasibu laki sita apeleke hesabu TRA. " huyu unamjibuje tena akiwa keshalewa?
Kwasasa huwezi mjibu chochote, inafaa tu unamsikiliza basi maana ukianza kumueleza hata iwe vipi hatokuelewa, Binadamu wengi wakishaamua jambo lao ni ngumu sana kufungua akili yake kukubali mitazamo au mawazo mapya mpaka aamue yeye.
Mwanzoni bookkeeping yake inaweza ikamtosha, ila akitaka ku expand biashara atajikuta yeye mwenyewe anaona umuhimu wa muhasibu, anaona umuhimu wa kuwa na manager, HR nk
Na hapo ndipo atakapojutia kwanini haku mshawishi mtoto wake hata mmoja asome mambo ya biashara ili utajiri uendelee, atajikuta akizeeka basi ule utajiri ndio unazeeka na yeye.
Wahindi kuanzia wakiwa wadogo kama baba ana biashara flani basi ataanza kushinda na mtoto wake kwenye hio biashara ili mtoto apate basic, confidence on how to run the business.
Ataenda kumuendeleza zaidi ili awe better manager na on going concept iendelee ku take place.
Angalia kama Mo Dewji, Bakhresa etc.. hawana dharau, wanajua umuhimu wa ku invest kwenye elimu ya mtoto, hata kama atasoma Mechanical, au kitu chochote lazima atajitahidi asome CPA au ACCA, au MBA
 
Back
Top Bottom