Mtumeeeeeeeee!!!

sixlove

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
549
371
Jamaa mmoja aliwatembelea wakwe zake, mkoa fulani ambao unasifika kuwa na simba wengi. Ilipofika wakati wa kwenda kulala wakwe zake walimtahadharisha kuwa asitoke usiku kuna simba, wakaagana na jamaa akaelekea kulala chumbani, ambako alilala shemeji yake( mtoto wapata miaka 4)

ilipofika usiku wa manane jamaa alibanwa haja ndogo na huko nje simba wanaunguruma, alishikwa na woga na huku mkojo ukiendelea kumbana. basi jamaa akaamua kumtoa yule mtoto kitandani alipokuwa amelala nakumuamishia kitandani kwake, kisha akakojoa kwenye kitanda alichokuwa amelala dogo.

baada ya kumaliza kukojoa, jamaa alienda kumchukua mtoto ili amrudishe mahali pake, akakuta mtoto amesha kunya kitandani kwake.

UNAFIKIRI KILICHOFATIA NI NINI?
 
Du nouma umenichekesha sana cjui jamaa apo atachukua uamuzi gani wa haraka maana kuumbuka nje nje
 
ahhahahahahah, ntabadilisha magodoro lile la mavi nalipeleka kwa mtoto na lile la mkojo , lol bora nililalie mwenyewe. ila so funny
 
dah,umeua mkuu mana nimecheka mpk bc na hacra nilzoamka nazo nahc zimeanza kupungua kwa kusoma hi kali ya mwaka.hureee "LIKE"teh teh teh!
 
Waliozoea kunya kitandani utawajua tu. Ngoja nimsubiri WA KUSOMA aje awape somo hapa.

Ile id yako ya WakuRead ilikuwa haipendezi, ila hii ya complicator inakufaa zaidi, sasa jambo dogo sana wewe una-complicate na kulifanya kuwa kubwa, ila pole sana kwa kubadili id huku ukijua hatutakugundua
 
ila adabu kwa mtoto itakuwa ndo imeisha hapo, maana mtoto atajua tu kuwa alokojoa ni huyo shemejie
 
Back
Top Bottom