Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,243
- 90,303
Wayahudi waliomshitaki Yesu kwa Herode na Pontio Pilato, wanafunzi wake walioukuwa wafuasi wake wanaotembea naye kila siku na Warumi waliokuwa wakoloni watawala wa Judea ambao ndio walimuhukumu Yesu wote wanashuhudia kwamba Yesu Kristo alitundikwa na kuuwawa msalabani, wanachotofautiana tu ni kama alifufuka kweli baada ya siku tatu kama alivyohaidi.
Inakujae mtu wa uarabuni ambaye hakuwepo wakati wa tukio lenyewe na hana rejea yoyote ya tukio hilo aje miaka 600 baadaye mbeleni na kusema Yesu Kristo hakuuwawa msalabani bali yalikuwa ni mazingaombwe tu yaliyopelekea mfuasi wake mmoja kuchukua sura yake na kusulubishwa badala yake huku Yesu Kristo mwenyewe akitoroka!
Inakujae mtu wa uarabuni ambaye hakuwepo wakati wa tukio lenyewe na hana rejea yoyote ya tukio hilo aje miaka 600 baadaye mbeleni na kusema Yesu Kristo hakuuwawa msalabani bali yalikuwa ni mazingaombwe tu yaliyopelekea mfuasi wake mmoja kuchukua sura yake na kusulubishwa badala yake huku Yesu Kristo mwenyewe akitoroka!