Vifo vya namna hiyo vimekuwa vya kawaida kwa waathirika wa Covid 19. Wanasema ukifikia stage ya ARDS, bila Respiratory Ventilator, una only 20 minutes before death.
Huko Ecuador, maiti nyingi za waliofariki kwa Covid 19 zimekuwa zikiokotwa kwenye mabasi, vituo vya mabasi na majumbani kiasi cha kushindwa kupata hata takwimu halisi za waliokofa na kuugua.
Huko Kahama, nako kuna kisa kinachunguzwa. Kuna mchina na mkewe walichukua chumba hotelini. Wahudumu waligundua mchina mwanamke alikuwa ni mgonjwa hasa japo hakusema. Walipoujulisha uongozi wa hotel, walichukuliwa kwenda hospitali. Uchunguzi unaendelea lakini hwakuruhusiwa kurudi hotelini japo walikuwa wamekwishalipia kwajili ya kukaa siku kadhaa. Kuna hisia walitaka kuifanya hoteli ndiyo isolation place yao.
Ushauri: Kipindi hiki, kama siyo lazima sana, ni aheri kujizuia kusafiri. Na ukisafiri, kama una usafiri binafsi, ukichoka, pumzika ndani ya gari kuliko kulala hotelini.