Mtu mmoja afariki, wawili wajeruhiwa katika ajali ya barabarani mkoani Arusha

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236
Mtu mmoja wamefariki dunia na wawili kujeruliwa katika ajali iliyotokea katika eneo Kikatiti jijini Arusha iliyohusisha lori lililobeba matofari kuyagonga magari sita yaliyokuwa mbele yake.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema chanzo cha ajali hiyo iliyotokea jana saa 2:30 usiku ni lori iliyokuwa imebeba matofali ilifeli breki ikiwa katika mteremko maeneo ya Kikaticha ambapo liligonga magari mengine yaliyokuwa mbele yake.

Amesema gari hilo liligonga gari aina ya Kruger ambayo ilikuwa ikiendeshwa na mzee aliyejulikana kwa jina la Carol Melkizedeck (70) ambaye alifariki muda mfupi na kusababisha foleni katika eneo hilo baada ya magari yaliyokuwa yamegongwa kufunga barabara.

Aidha, Kamanda Mkumbo ameeleza kuwa baada ya gari iliyokuwa imebeba matofali kuyagonga magari hayo ilipinduka na kuingia mtaroni, ambapo dereva na msaadizi wake walijeruliwa na kukimbizwa hospitalini.
 
Mtu mmoja wamefariki dunia na wawili kujeruliwa katika ajali iliyotokea katika eneo Kikaticha jijini Arusha iliyohusisha lori lililobeba matofari kuyagonga magari sita yaliyokuwa mbele yake.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema chanzo cha ajali hiyo iliyotokea jana saa 2:30 usiku ni lori iliyokuwa imebeba matofali ilifeli breki ikiwa katika mteremko maeneo ya Kikaticha ambapo liligonga magari mengine yaliyokuwa mbele yake.

Dereva mwenye utu na ubinadamu anapoendesha lori na likafeli breki, atalipeleka nje ya barabara ili ikibidi lipunduke badala ya kutumia magari mengine yaliyo mbele yake kama breki.
 
KAMANDA MPINGA UWE UNAZUNGUKIA OFISI YAKO YA ZAMANI.
Madereva walikuwa na bado wanakuelewa sana.
 
Dereva mwenye utu na ubinadamu anapoendesha lori na likafeli breki, atalipeleka nje ya barabara ili ikibidi lipunduke badala ya kutumia magari mengine yaliyo mbele yake kama breki.
Ajali ikikukabili akili unazotumia kujinusuru si hizi ulizonazo sasa.
 
Ajali ikikukabili akili unazotumia kujinusuru si hizi ulizonazo sasa.
Mkuu, sidahani kama kuachia lori likagonge magari mebele yako ni njia ya kujinusuru. Hiyo ni brain freez.

Watu husahau hata kupangua gia kwenda gia kubwa ili injini isaidie kupunguza mwendo
 
R.I.P Mwenyenzi Mungu awape Nguvu na faraja wafiwa wote..ajali zimezidi madereva wawe makini
 
Mkuu, sidahani kama kuachia lori likagonge magari mebele yako ni njia ya kujinusuru. Hiyo ni brain freez.

Watu husahau hata kupangua gia kwenda gia kubwa ili injini isaidie kupunguza mwendo
Mkuu hali ya taharuki inayokukuta unaweza kufunga break kwa mdomo, yaani kupiga makelele!
Ajali isikie kwa kusimuliwa.
 
Back
Top Bottom