Nakubaliana na Mawazo yako. Pendekezo la katiba kutoka kwenye hili bunge la Jiwe linaweza kuzaa katiba mbovu kuliko hii iliyopo sasa kwasababu moja kubwa; wabunge wote pamoja na spika wao ni vikaragosi wa Jiwe!!Hiyo hoja ya katiba inaenda kujadiliwa kwenye bunge gani? Kumbuka kiongozi wa bunge ni mwenyekiti wa bunge, huyu ndio mwenye maamuzi hoja ipi iingie ndani ya bunge, na ukumbuke katibu wa bunge ni mteule wa rais asiyetaka katiba mpya. Unazungumza nadharia na sio uhalisia. Mwenye maamuzi na hilo bunge ni rais Magufuli, na anachotaka ndio kinajadiliwa bungeni, na asichokitaka hakijadiliwi.
Spika pamoja na wabunge karibuni wote ni
wateule wa Jiwe hivyo wapo pale kutekeleza matakwa yake, hivi sasa mpango wale ni kutaka kubadilisha katiba ili waondoe kipengele kinachohusu ukomo wa Urais!! Hii ndio sababu yake moja wapo ya kuwaondoa wakongwe wakina Chenge etc bungeni ili kusiwe na wabunge ambao wangediriki kupinga mpango huu.
Katiba ya wananchi itapatikana pale tu Tume huru ya uchaguzi itakapopatikana na kwanza kabisa kuanza kazi yake kwakusimamia uchaguzi ulio huru na haki; wabunge watakaotokana na uchaguzi huo ndio wafanye kazi ya kutayarisha katiba itakayokubalika na wananchi, vinginevyo miaka yote tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu!!