Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 10,884
- 18,824
By SHANWA, 1967.
TEGU, mwana wa Goja, alisimama kwenye ardhi iliyoinuka ambayo iliyatenga mabonde ya Ugweno na Usangi, mahali alipozaliwa. Ingawa alikuwa mvulana mwenye umri wa miaka kumi na sita tu, lakini alionekana kuwa alikuwa mrefu kama mtu mzima. Ngozi ya mbuzi aliyoivaa begani mwake haikuweza kuifunika kabisa miguu yake na mikono yake.
Uso wake ulionekana umejaa ghadhabu na fadhaa. Alikuwa amemwendea rafiki yake Mundula, na huko waliutumia wakati wao mwingi katika mchezo wa kutupa mishale kwa kutumia pinde zao. Mundula alikuwa na shabaha nzuri, kwani katika mishale kumi aliyoitupa, tisa ilipiga kwenye alama. Maskini Tegu alikuwa akiikosa alama kila alipoitupa mishale yake. Kwa muda fulani Mundula hakusema neno lo lote. Lakini Tegu aliutupa mshale wake mmoja vibaya sana hata ilimfanya Mundula acheke sana kwa sauti kubwa. Tegu angaliweza kumsamehe rafiki yake, lakini wavulana fulani waliokuwa wakipita pale walimcheka pia na walimtania kwa kumwita kwa jina la msichana. Wengine walimletea mtungi ili wabadilishe na uta wake. Damu ya Tegu ilichemka kwa hasira na aibu. Joto la damu yake liliweza kusikika katika mashavu yake. Kwa hasira aliyokuwa nayo karibu auvunje upinde wake kwa kutumia goti lake.
Bonde la Usangi
Njia iliyokuwa mbele yake ilikuwa na mawe na changarawe nyingi, njia yenyewe ilikuwa inateremka kwenye bonde ambalo ardhi yake imelimwa, sehemu ambayo majani ya migomba yalipepea katika upepo na yalimetameta chini ya nuru ya jua. Nyumba ziliweza kuonekana hapa na kule zikijitokeza kwenye majani mabichi, nyumba hizo zilikuwa ni za misonge. Watoto walionekana wakicheza kwenye sehemu zilizokuwa wazi na moshi ulionekana ukipanda kutoka kwenye nyumba fulani fulani. Wanawake walikuwa mashambani wakiinama sana katika mashamba yao ya viazi vitamu, huku wakilima wakitumia majembe madogo yenye mipini mifupi au wakitumia miti iliyochongwa sana na yenye ncha kali.
Tegu aliweza kuona nyumba ya chifu kwa upande wa kushoto kwenye mtelemko wa mlima. Kulikuwa na ua mkubwa kuizunguka nyumba hiyo na aliweza kumwona mlinzi amesimama mlangoni akiangalia kwenye kijia kinachotoka bondeni. Kutoka vilimani kulikuwa na vifereji vingi vya maji vilivyoungana na kufanya mto uliojipindapinda kama nyoka ukipita kwenye bonde.
Maji yenye rangi ya udongo yalikuwa yakitiririka kwenye sehemu fulani. Mayungiyungi yalionekana yakijificha kidogo mtoni, na magugu na matete yalikuwa yameota kando ya mto. Mbuzi walionekana wakitembea huko na huko karibu na vibanda, ng'ombe nao walikuwa wamesimama wakila nyasi katika sehemu za juu. Hakika ilikuwa ni hali ya amani na utulivu.
Kifo cha chifu
Ghafula wanawake walitoka nyumbani mwa chifu. Tegu aliwasikia wanalia na kuomboleza, huku wakiinama kuuchukua udongo na vumbi na kuutia katika vichwa vyao. Kutokana na kitendo hicho, alielewa kwamba chifu amefariki. Huko makondeni aliwaona wanawake wakiinuka ili kusikiliza. Wanaume walitoka kwenye nyumba zao wakikimbia kuelekea kwenye msiba. Alipozisikia ngoma zikilia, aliondoka mbio kuelekea bondeni.
Kifo cha chifu kilimfanya Tegu azisahau taabu zake mwenyewe. Chifu alikuwa ameugua kwa muda wa miaka mingi. Alikuwa akiugua ugonjwa usio wa kawaida ambao uliwaua jamaa zake mmoja baada ya mmoja na hata mwishowe hakuna hata mmoja aliyesalia hai. Baada ya Mzee Kichechi kufariki hapakuwa na mtu aliyekuwa na haki ya kukikalia kiti cha Ufalme. Watu wote waliingiwa na woga kwa ajili ya kifo cha chifu wao. Wakati alipokuwa hai chifu huyu aliweza kumzuia Mfupa, mchawi aliyeogopwa, kuzitumia dawa zake za uchawi ili kuwadhuru watu. Sasa ilionekana kuwa hapatakuwa na mtu ambaye ataweza kumzuia Mfupa katika kujitwalia mamlaka ya Uchifu.
Tegu alikimbia mbio akipita kwenye kijia kilichokuwapo kando ya mto, akapita safu za miti, akafika kwenye shamba la migomba. Kutoka hapo ilipokuwa migomba hakukuwa mbali na nyumba ya baba yake. Tegu alipoikaribia nyumba ya baba yake alisikia sauti ya mti ukichongwa.
Mchongaji na jamaa yake
Sauti hiyo haikumpendeza Tegu hata kidogo. Tegu alikuwa amechoka kumwona baba yake akishughulika na uchongaji tu daima. Baba yake alikuwa mpole, mpole sana kwake na kwa mama yake.
Tegu alipofika kiwanjani, sauti ilinyamaza. Tegu akapaaza sauti, akamwambia baba yake, 'Kichechi amefariki dunia'. Baba yake akaitikia kwa kuinamisha kichwa chake akasema, ‘Kifo hiki kimekuwa kikitazamiwa kwa muda mrefu.' Baada ya kusema hayo, alivipanga vyombo vyake vya kazi upande mmoja, akakaa na kuikunja miguu yake mbele ikipitana, akawa anafikiri sana. Mikono na miguu yake ilikuwa myembamba, na ingawa hakuwa mzee sana, uso wake ulikuwa kama kipande cha ngozi ya zamani, iliyojaa mistari.
Tegu aliutupa chini upinde wake na podo la mishale wakati Nata alipokuwa anaingia kutoka mtoni huku akiuchukua mtungi wa maji kichwani. Nata alikuwa amekasirika kwa kuwa njiani aliteleza, na maji yakammwagikia usoni. Wanawake wenzake walimcheka na wakamdhihaki kwa kuwa hakuwa na nguvu na kwamba alikuwa dhaifu. Mama yake akauliza, 'Sijui mtoto wetu ametuletea ndege au mnyama gani ili kunisaidia kuwalisha wanaume wawili?' Tegu akamjibu, 'Nimekuwa nikifanya mazoezi tu, mama.'
Mama yake akaendelea, 'Hakika unahitaji mazoezi mengi. Baba yako hakufanya lo lote kukufundisha mwanangu. Akina baba wengine wamekuwa wakiwachukua watoto wao porini kuwinda. Baba yako hakufanya kitu cho chote ila kukaa tu na kuchonga sanamu.
Goja akasema kwa ukali, 'Acheni kuongea maongezi ya namna hiyo. Ninyi mnafikiri kila kitu hakiendi sawa hapa petu.' Nata akamjibu, 'Mambo mengi hayaendi vyema hapa. Watu wengine wanakula nyama, lakini sisi hatuna nyama ya kula ingawa tunao ng'ombe wengi kama wale wa Mfupa.'
Tegu alimtazama baba yake kwa uso wa huzuni. Alijua kwamba kulikuwa na ukweli fulani katika maneno ya mama yake. Uso wa Goja ulikuwa ni wenye hasira sana kwa vile alivyolitaja jina la mganga.
Goja akajibu, 'Mfupa amewapata ng'ombe wake kwa njia mbaya isiyo ya halali. Ng'ombe wangu nimewapata kwa njia ya haki, kwa ajili ya kufanya kazi kwa bidii.'
Tegu akamwuliza baba yake, 'Mbona hukunichukua porini kuwinda na kunifundisha kuwa mpiganaji hodari? Baba yake Mundula ni mpiganaji hodari na mwindaji shujaa. Amemfundisha Mundula mambo mengi, na wavulana wengine wamefundishwa namna ya kupiga mishale vizuri.'
Goja alimtazama mwanawe, uso wake wenye mistari mistari na macho yake ya kikahawia haikuonyesha dalili yo yote ya kuwa na hasira. Baba akamwambia mwanawe, “Tazama idadi ya ng'ombe tulio nao. Utakuwa tajiri sana nitakapokufa. Huna budi kuridhika; jaribu kuelewa kwamba watu wanaopigana, wao ni kama ng'ombe, wasio na fahamu, wanaofaa kwa kuuawa tu. Mtu mmoja anayeweza kutengeneza vitu kwa mikono yake na kuvibadili na watu wengine ili kupata mahitaji yake, ni bora kuliko wapiganaji mia moja.'
Nata akaruka juu na kisha akamwangalia mumewe akamwambia, ‘Lakini kama wanaume wote wangalikuwa kama wewe, basi Wakamba na Wamasai wangevishambulia vijiji vyetu na wangechukua kila kitu tulicho nacho. Sote tungekuwa watumwa, kama nilivyo mimi.'
Hapo tena, Tegu alifikiri kwamba mama yake alikuwa amesema maneno yenye busara. Alimtazama baba yake kwa dharau kwani alijua kwamba mwanamke hapaswi kuyasema maneno kama hayo kwa mwanamume.
Mama yake akaendelea, 'Je, haiwezekani kwa mtu kutengeneza vitu kwa mikono yake na papo hapo kuwa mpiganaji hodari? Ni kweli kwamba mtu anayepigana na hali hana ngo'mbe ni sawa na mbwa asiye na mkia, lakini pia, mtu mwenye ng'ombe na ambaye hawezi kupigana ni kama mbwa asiye na meno.'
Goja aliinuka na kusimama. Alikuwa mtu mfupi na alionekana mdogo mbele ya mkewe. Goja akasema, 'Inatosha! Siku zote nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe na nina hekima pia. Kwa ajili hiyo watu wengi hunijia ili kuomba mashauri. Inawezekana namna gani, mimi ambaye sijawa mwindaji mkubwa, au sijawahi kupigana, kutazamiwa kuwafundisha watu mambo hayo? Nendeni! Kuna watu wanakuja kuniamkia sasa. Hao ni wazee wa kabila letu.'
Wazee wanaomba mashauri
Nata aliondoka kwa haraka. Goja aliendelea kukaa pale pale huku ameikunja miguu yake. Alingoja mpaka wageni wake walipokaa chini mbele yake. Wazee wakamwamkia, Salaam za heri kwako Goja.' Mmoja wa wageni akaendelea kusema, "Tumekuja kwako kwa ajili ya kifo cha Kichechi.'
Goja alikaa kimya akijua kwamba hapakuwa na neno jingine zaidi. Baada ya muda, yule msemaji aliendelea kusema, 'Kwa kuwa Kichechi amefariki, hatuna mtu tunayeweza kumchagua awe chifu. Je, unaweza kutupa shauri?' Wote walikuwa kimya kwa muda, halafu Goja akasema, 'Je, mnaweza kutengeneza halmashauri itakayotawala kwa muda mpaka mtakapomchagua yule atakayekuwa chifu?'
Mzee mwingine akamjibu, 'Mfupa atakuwa na mamlaka makubwa juu yetu.' 'Ikiwa ni hivyo, basi uite mkutano, na watu wakate shauri juu ya jinsi watakavyotawaliwa.'
Watu kadha walianza kusema kwa mara moja, lakini mmoja alipaaza sauti yake na kufanya asikiwe zaidi akasema, Mfupa hataruhusu mkutano huo kufanyika, na watu wote wanamwogopa sana.'
Goja akawaambia, ‘Uiteni kwanza mkutano na tuone utakavyotokea. Sina shauri jingine la kuwapa.' Wazee walisimama shingo upande wakasemezana, 'Afadhali tutimize jambo hili mara moja kabla Mfupa hajapata nafasi ya kufanya mipango itakayokuwa ni kwa manufaa yake.'
Goja naye aliondoka kwenda nyuma kana kwamba alikuwa anakwenda kuuchagua mti mwingine auchonge. Alipoiangalia miti yake alisema, ‘Hakuna mti utakaonifaa kwa kazi yangu nyingine. Sina budi kwenda kwenye ghala yangu nyingine.'
Tegu, aliyekuwa akiangalia namna baba yake alivyofanya wakati wale wazee walipofika, alishangazwa mno hata akalia akasema, 'Hapo ni nusu ya njia tu kwenda Ngulu. Je, huendi kwenye mkutano?'
Baba yake akamjibu, 'Sina nia ya kumwona Mfupa akikalia Kiti cha Ufalme.' Tegu alikitikisa kichwa chake. Ataweza namna gani kumwelewa baba yake? Naye pia aliinuka akasimama, na bila ya kusema neno jingine zaidi, alikimbia kwenda kwenye nyumba ya mkutano. Alikusudia kupata kiti kizuri atakachokikalia wakati wa mkutano.
Kwa kweli alifanya jambo zuri kwa kufanya haraka, kwani mara tu ngoma zilipoanza kulia, watu walianza kujazana kwenye nyumba ya mkutano ambayo iliezekwa kwa nyasi. Ndani, kwa upande mmoja, sakafu ilikuwa imeinuliwa kidogo. Watumishi wa marehemu chifu walishughulika kuvipanga viti vitakavyokaliwa na Wazee. Mbali na viti vingine, kiliwekwa Kiti cha Ufalme ambacho chifu tu ndiye aliyeruhusiwa kukikalia.
Mganga anatokea
Nyumba ya mkutano ilijaa baada ya muda mfupi tu, na hapo ndipo ngoma ziliponyamaza. Kisha, wazee walipokwisha kuketi katika viti vyao, na kabla ya mtu yoyote hajaanza kusema, kitu fulani kilitokea, kitu ambacho kilimtisha kila mtu. Mchawi, Bwana Mfupa, aliingia ndani ya nyumba ya mkutano.
Wale ambao walikuwa hawajakaa vitini mwao, ghafula walinyamaza walipomwona Mfupa anakwenda kuelekea kule kilikowekwa Kiti cha Ufalme. Pumzi za watu zilisikika kama upepo mkubwa wakati ukivuma kwenye majani makavu, walipomwona Mfupa akiuinamisha mwili wake wenye kibiongo na kuukalisha kwenye kiti cha heshima kuu. Msemaji wa Wazee aliinuka polepole, uso wake ukiwa umejaa fadhaa na mashaka, mwili wake wa kizee ukitetemeka alipokuwa akijaribu kuyashinda mawazo na hofu zake.
Msemaji huyo alimwuliza Mfupa, ‘Kwa mamlaka na uwezo gani unakaa kwenye Kiti cha Ufalme?' Bila kujibu neno, Mfupa aliwatazama watu na huku ameyafumba macho yake nusu. Itakuwa ni vigumu kueleza jinsi Tegu alivyoyachukia macho hayo, pia alivyoichukia ngozi yake iliyopayuka ikiwa na alama kadhaa za kikahawia kama za ngozi ya mbwa. Jinsi gani mtu anaweza kuwa karibu mweupe, mwenye nywele nyeupe na ngozi isiyo na afya! Mfupa alipotaka kujibu alitabasamu akasema, 'Hakuna mahali pengine pa kukaa. Pia hakuna mwingine mwenye haki zaidi yangu ya kukikalia Kiti cha Enzi.'
Mgeni anaingia
Kelele zilizofanywa kutoka nyuma zilimfanya Tegu ageuke na kutazama mlangoni. Watu wote mkutanoni nao wakatazama mlangoni. Watu walistaajabu kuona kwamba kulikuwa kimya na hata sauti ya upumzi haikusikika. Kule mlangoni alikuwapo mgeni mmoja mwenye kimo kirefu. Kichwani alivaa aina ya kilemba cha manyoya marefu na nyasi zilizotiwa rangi. Usoni alikuwa amevaa kinyago cha mti. Kinyago hicho kilikuwa na matundu mawili ambayo macho mawili ya kutisha ya yule mgeni yaliweza kuonekana yaking'aa. Alikuwa tumbo wazi lakini kiunoni alivaa vazi fupi lililotengenezwa kwa nyasi; mikononi mwake pia mlizungushwa kanda za nyasi. Hakuna mtu aliyesema neno kwa muda fulani. Kisha mgeni akasema kwa sauti ndogo, 'Mfupa, ondoka kwenye Kiti cha Ufalme.'
SURA YA KWANZA
MGENI ANATOKEA
MGENI ANATOKEA
TEGU, mwana wa Goja, alisimama kwenye ardhi iliyoinuka ambayo iliyatenga mabonde ya Ugweno na Usangi, mahali alipozaliwa. Ingawa alikuwa mvulana mwenye umri wa miaka kumi na sita tu, lakini alionekana kuwa alikuwa mrefu kama mtu mzima. Ngozi ya mbuzi aliyoivaa begani mwake haikuweza kuifunika kabisa miguu yake na mikono yake.
Uso wake ulionekana umejaa ghadhabu na fadhaa. Alikuwa amemwendea rafiki yake Mundula, na huko waliutumia wakati wao mwingi katika mchezo wa kutupa mishale kwa kutumia pinde zao. Mundula alikuwa na shabaha nzuri, kwani katika mishale kumi aliyoitupa, tisa ilipiga kwenye alama. Maskini Tegu alikuwa akiikosa alama kila alipoitupa mishale yake. Kwa muda fulani Mundula hakusema neno lo lote. Lakini Tegu aliutupa mshale wake mmoja vibaya sana hata ilimfanya Mundula acheke sana kwa sauti kubwa. Tegu angaliweza kumsamehe rafiki yake, lakini wavulana fulani waliokuwa wakipita pale walimcheka pia na walimtania kwa kumwita kwa jina la msichana. Wengine walimletea mtungi ili wabadilishe na uta wake. Damu ya Tegu ilichemka kwa hasira na aibu. Joto la damu yake liliweza kusikika katika mashavu yake. Kwa hasira aliyokuwa nayo karibu auvunje upinde wake kwa kutumia goti lake.
Bonde la Usangi
Njia iliyokuwa mbele yake ilikuwa na mawe na changarawe nyingi, njia yenyewe ilikuwa inateremka kwenye bonde ambalo ardhi yake imelimwa, sehemu ambayo majani ya migomba yalipepea katika upepo na yalimetameta chini ya nuru ya jua. Nyumba ziliweza kuonekana hapa na kule zikijitokeza kwenye majani mabichi, nyumba hizo zilikuwa ni za misonge. Watoto walionekana wakicheza kwenye sehemu zilizokuwa wazi na moshi ulionekana ukipanda kutoka kwenye nyumba fulani fulani. Wanawake walikuwa mashambani wakiinama sana katika mashamba yao ya viazi vitamu, huku wakilima wakitumia majembe madogo yenye mipini mifupi au wakitumia miti iliyochongwa sana na yenye ncha kali.
Tegu aliweza kuona nyumba ya chifu kwa upande wa kushoto kwenye mtelemko wa mlima. Kulikuwa na ua mkubwa kuizunguka nyumba hiyo na aliweza kumwona mlinzi amesimama mlangoni akiangalia kwenye kijia kinachotoka bondeni. Kutoka vilimani kulikuwa na vifereji vingi vya maji vilivyoungana na kufanya mto uliojipindapinda kama nyoka ukipita kwenye bonde.
Maji yenye rangi ya udongo yalikuwa yakitiririka kwenye sehemu fulani. Mayungiyungi yalionekana yakijificha kidogo mtoni, na magugu na matete yalikuwa yameota kando ya mto. Mbuzi walionekana wakitembea huko na huko karibu na vibanda, ng'ombe nao walikuwa wamesimama wakila nyasi katika sehemu za juu. Hakika ilikuwa ni hali ya amani na utulivu.
Kifo cha chifu
Ghafula wanawake walitoka nyumbani mwa chifu. Tegu aliwasikia wanalia na kuomboleza, huku wakiinama kuuchukua udongo na vumbi na kuutia katika vichwa vyao. Kutokana na kitendo hicho, alielewa kwamba chifu amefariki. Huko makondeni aliwaona wanawake wakiinuka ili kusikiliza. Wanaume walitoka kwenye nyumba zao wakikimbia kuelekea kwenye msiba. Alipozisikia ngoma zikilia, aliondoka mbio kuelekea bondeni.
Kifo cha chifu kilimfanya Tegu azisahau taabu zake mwenyewe. Chifu alikuwa ameugua kwa muda wa miaka mingi. Alikuwa akiugua ugonjwa usio wa kawaida ambao uliwaua jamaa zake mmoja baada ya mmoja na hata mwishowe hakuna hata mmoja aliyesalia hai. Baada ya Mzee Kichechi kufariki hapakuwa na mtu aliyekuwa na haki ya kukikalia kiti cha Ufalme. Watu wote waliingiwa na woga kwa ajili ya kifo cha chifu wao. Wakati alipokuwa hai chifu huyu aliweza kumzuia Mfupa, mchawi aliyeogopwa, kuzitumia dawa zake za uchawi ili kuwadhuru watu. Sasa ilionekana kuwa hapatakuwa na mtu ambaye ataweza kumzuia Mfupa katika kujitwalia mamlaka ya Uchifu.
Tegu alikimbia mbio akipita kwenye kijia kilichokuwapo kando ya mto, akapita safu za miti, akafika kwenye shamba la migomba. Kutoka hapo ilipokuwa migomba hakukuwa mbali na nyumba ya baba yake. Tegu alipoikaribia nyumba ya baba yake alisikia sauti ya mti ukichongwa.
Mchongaji na jamaa yake
Sauti hiyo haikumpendeza Tegu hata kidogo. Tegu alikuwa amechoka kumwona baba yake akishughulika na uchongaji tu daima. Baba yake alikuwa mpole, mpole sana kwake na kwa mama yake.
Tegu alipofika kiwanjani, sauti ilinyamaza. Tegu akapaaza sauti, akamwambia baba yake, 'Kichechi amefariki dunia'. Baba yake akaitikia kwa kuinamisha kichwa chake akasema, ‘Kifo hiki kimekuwa kikitazamiwa kwa muda mrefu.' Baada ya kusema hayo, alivipanga vyombo vyake vya kazi upande mmoja, akakaa na kuikunja miguu yake mbele ikipitana, akawa anafikiri sana. Mikono na miguu yake ilikuwa myembamba, na ingawa hakuwa mzee sana, uso wake ulikuwa kama kipande cha ngozi ya zamani, iliyojaa mistari.
Tegu aliutupa chini upinde wake na podo la mishale wakati Nata alipokuwa anaingia kutoka mtoni huku akiuchukua mtungi wa maji kichwani. Nata alikuwa amekasirika kwa kuwa njiani aliteleza, na maji yakammwagikia usoni. Wanawake wenzake walimcheka na wakamdhihaki kwa kuwa hakuwa na nguvu na kwamba alikuwa dhaifu. Mama yake akauliza, 'Sijui mtoto wetu ametuletea ndege au mnyama gani ili kunisaidia kuwalisha wanaume wawili?' Tegu akamjibu, 'Nimekuwa nikifanya mazoezi tu, mama.'
Mama yake akaendelea, 'Hakika unahitaji mazoezi mengi. Baba yako hakufanya lo lote kukufundisha mwanangu. Akina baba wengine wamekuwa wakiwachukua watoto wao porini kuwinda. Baba yako hakufanya kitu cho chote ila kukaa tu na kuchonga sanamu.
Goja akasema kwa ukali, 'Acheni kuongea maongezi ya namna hiyo. Ninyi mnafikiri kila kitu hakiendi sawa hapa petu.' Nata akamjibu, 'Mambo mengi hayaendi vyema hapa. Watu wengine wanakula nyama, lakini sisi hatuna nyama ya kula ingawa tunao ng'ombe wengi kama wale wa Mfupa.'
Tegu alimtazama baba yake kwa uso wa huzuni. Alijua kwamba kulikuwa na ukweli fulani katika maneno ya mama yake. Uso wa Goja ulikuwa ni wenye hasira sana kwa vile alivyolitaja jina la mganga.
Goja akajibu, 'Mfupa amewapata ng'ombe wake kwa njia mbaya isiyo ya halali. Ng'ombe wangu nimewapata kwa njia ya haki, kwa ajili ya kufanya kazi kwa bidii.'
Tegu akamwuliza baba yake, 'Mbona hukunichukua porini kuwinda na kunifundisha kuwa mpiganaji hodari? Baba yake Mundula ni mpiganaji hodari na mwindaji shujaa. Amemfundisha Mundula mambo mengi, na wavulana wengine wamefundishwa namna ya kupiga mishale vizuri.'
Goja alimtazama mwanawe, uso wake wenye mistari mistari na macho yake ya kikahawia haikuonyesha dalili yo yote ya kuwa na hasira. Baba akamwambia mwanawe, “Tazama idadi ya ng'ombe tulio nao. Utakuwa tajiri sana nitakapokufa. Huna budi kuridhika; jaribu kuelewa kwamba watu wanaopigana, wao ni kama ng'ombe, wasio na fahamu, wanaofaa kwa kuuawa tu. Mtu mmoja anayeweza kutengeneza vitu kwa mikono yake na kuvibadili na watu wengine ili kupata mahitaji yake, ni bora kuliko wapiganaji mia moja.'
Nata akaruka juu na kisha akamwangalia mumewe akamwambia, ‘Lakini kama wanaume wote wangalikuwa kama wewe, basi Wakamba na Wamasai wangevishambulia vijiji vyetu na wangechukua kila kitu tulicho nacho. Sote tungekuwa watumwa, kama nilivyo mimi.'
Hapo tena, Tegu alifikiri kwamba mama yake alikuwa amesema maneno yenye busara. Alimtazama baba yake kwa dharau kwani alijua kwamba mwanamke hapaswi kuyasema maneno kama hayo kwa mwanamume.
Mama yake akaendelea, 'Je, haiwezekani kwa mtu kutengeneza vitu kwa mikono yake na papo hapo kuwa mpiganaji hodari? Ni kweli kwamba mtu anayepigana na hali hana ngo'mbe ni sawa na mbwa asiye na mkia, lakini pia, mtu mwenye ng'ombe na ambaye hawezi kupigana ni kama mbwa asiye na meno.'
Goja aliinuka na kusimama. Alikuwa mtu mfupi na alionekana mdogo mbele ya mkewe. Goja akasema, 'Inatosha! Siku zote nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe na nina hekima pia. Kwa ajili hiyo watu wengi hunijia ili kuomba mashauri. Inawezekana namna gani, mimi ambaye sijawa mwindaji mkubwa, au sijawahi kupigana, kutazamiwa kuwafundisha watu mambo hayo? Nendeni! Kuna watu wanakuja kuniamkia sasa. Hao ni wazee wa kabila letu.'
Wazee wanaomba mashauri
Nata aliondoka kwa haraka. Goja aliendelea kukaa pale pale huku ameikunja miguu yake. Alingoja mpaka wageni wake walipokaa chini mbele yake. Wazee wakamwamkia, Salaam za heri kwako Goja.' Mmoja wa wageni akaendelea kusema, "Tumekuja kwako kwa ajili ya kifo cha Kichechi.'
Goja alikaa kimya akijua kwamba hapakuwa na neno jingine zaidi. Baada ya muda, yule msemaji aliendelea kusema, 'Kwa kuwa Kichechi amefariki, hatuna mtu tunayeweza kumchagua awe chifu. Je, unaweza kutupa shauri?' Wote walikuwa kimya kwa muda, halafu Goja akasema, 'Je, mnaweza kutengeneza halmashauri itakayotawala kwa muda mpaka mtakapomchagua yule atakayekuwa chifu?'
Mzee mwingine akamjibu, 'Mfupa atakuwa na mamlaka makubwa juu yetu.' 'Ikiwa ni hivyo, basi uite mkutano, na watu wakate shauri juu ya jinsi watakavyotawaliwa.'
Watu kadha walianza kusema kwa mara moja, lakini mmoja alipaaza sauti yake na kufanya asikiwe zaidi akasema, Mfupa hataruhusu mkutano huo kufanyika, na watu wote wanamwogopa sana.'
Goja akawaambia, ‘Uiteni kwanza mkutano na tuone utakavyotokea. Sina shauri jingine la kuwapa.' Wazee walisimama shingo upande wakasemezana, 'Afadhali tutimize jambo hili mara moja kabla Mfupa hajapata nafasi ya kufanya mipango itakayokuwa ni kwa manufaa yake.'
Goja naye aliondoka kwenda nyuma kana kwamba alikuwa anakwenda kuuchagua mti mwingine auchonge. Alipoiangalia miti yake alisema, ‘Hakuna mti utakaonifaa kwa kazi yangu nyingine. Sina budi kwenda kwenye ghala yangu nyingine.'
Tegu, aliyekuwa akiangalia namna baba yake alivyofanya wakati wale wazee walipofika, alishangazwa mno hata akalia akasema, 'Hapo ni nusu ya njia tu kwenda Ngulu. Je, huendi kwenye mkutano?'
Baba yake akamjibu, 'Sina nia ya kumwona Mfupa akikalia Kiti cha Ufalme.' Tegu alikitikisa kichwa chake. Ataweza namna gani kumwelewa baba yake? Naye pia aliinuka akasimama, na bila ya kusema neno jingine zaidi, alikimbia kwenda kwenye nyumba ya mkutano. Alikusudia kupata kiti kizuri atakachokikalia wakati wa mkutano.
Kwa kweli alifanya jambo zuri kwa kufanya haraka, kwani mara tu ngoma zilipoanza kulia, watu walianza kujazana kwenye nyumba ya mkutano ambayo iliezekwa kwa nyasi. Ndani, kwa upande mmoja, sakafu ilikuwa imeinuliwa kidogo. Watumishi wa marehemu chifu walishughulika kuvipanga viti vitakavyokaliwa na Wazee. Mbali na viti vingine, kiliwekwa Kiti cha Ufalme ambacho chifu tu ndiye aliyeruhusiwa kukikalia.
Mganga anatokea
Nyumba ya mkutano ilijaa baada ya muda mfupi tu, na hapo ndipo ngoma ziliponyamaza. Kisha, wazee walipokwisha kuketi katika viti vyao, na kabla ya mtu yoyote hajaanza kusema, kitu fulani kilitokea, kitu ambacho kilimtisha kila mtu. Mchawi, Bwana Mfupa, aliingia ndani ya nyumba ya mkutano.
Wale ambao walikuwa hawajakaa vitini mwao, ghafula walinyamaza walipomwona Mfupa anakwenda kuelekea kule kilikowekwa Kiti cha Ufalme. Pumzi za watu zilisikika kama upepo mkubwa wakati ukivuma kwenye majani makavu, walipomwona Mfupa akiuinamisha mwili wake wenye kibiongo na kuukalisha kwenye kiti cha heshima kuu. Msemaji wa Wazee aliinuka polepole, uso wake ukiwa umejaa fadhaa na mashaka, mwili wake wa kizee ukitetemeka alipokuwa akijaribu kuyashinda mawazo na hofu zake.
Msemaji huyo alimwuliza Mfupa, ‘Kwa mamlaka na uwezo gani unakaa kwenye Kiti cha Ufalme?' Bila kujibu neno, Mfupa aliwatazama watu na huku ameyafumba macho yake nusu. Itakuwa ni vigumu kueleza jinsi Tegu alivyoyachukia macho hayo, pia alivyoichukia ngozi yake iliyopayuka ikiwa na alama kadhaa za kikahawia kama za ngozi ya mbwa. Jinsi gani mtu anaweza kuwa karibu mweupe, mwenye nywele nyeupe na ngozi isiyo na afya! Mfupa alipotaka kujibu alitabasamu akasema, 'Hakuna mahali pengine pa kukaa. Pia hakuna mwingine mwenye haki zaidi yangu ya kukikalia Kiti cha Enzi.'
Mgeni anaingia
Kelele zilizofanywa kutoka nyuma zilimfanya Tegu ageuke na kutazama mlangoni. Watu wote mkutanoni nao wakatazama mlangoni. Watu walistaajabu kuona kwamba kulikuwa kimya na hata sauti ya upumzi haikusikika. Kule mlangoni alikuwapo mgeni mmoja mwenye kimo kirefu. Kichwani alivaa aina ya kilemba cha manyoya marefu na nyasi zilizotiwa rangi. Usoni alikuwa amevaa kinyago cha mti. Kinyago hicho kilikuwa na matundu mawili ambayo macho mawili ya kutisha ya yule mgeni yaliweza kuonekana yaking'aa. Alikuwa tumbo wazi lakini kiunoni alivaa vazi fupi lililotengenezwa kwa nyasi; mikononi mwake pia mlizungushwa kanda za nyasi. Hakuna mtu aliyesema neno kwa muda fulani. Kisha mgeni akasema kwa sauti ndogo, 'Mfupa, ondoka kwenye Kiti cha Ufalme.'