Mtoto wa Wassira ajiunga Chadema

Mtoto wa Wassira ajiunga Chadema




Kadi ikitiliwa saini, Houston, Texas, Marekani (picha: Blogu ya CHADEMA USA)


Viongozi wa Tawi la CHADEMA-Houston wamkabidhi Kadi ya CHADEMA, Makongoro Wassira (picha: blogu ya CHADEMA USA)





 
Katika watu wanaikashifu Chadema na kuwa na maneno ya maudhi ni Waziri Wassira. Sasa kwa kuonyesha kuwa M4C haina msamaha hata kwa familia yake mtoto wake aishie USA aitwae Makongoro Wassira amejiunga na M4C.

Akizungumza wakati anakabidhiwa kadi alisema yeye ni wa kwanza tu kujiunga M4C lakini ndugu zake wote wapo mbioni kujiunga na anadhani baba yake pekee ndie atabaki CCM.

Peopleeeeeeeeeeeeeeee power.

IMG_1641.JPG

Viongozi wa Tawi la Chadema Houston wamkabidhi Kadi ya Chadema Makongoro Wassira
Angalia picha hapa CHADEMA USA

Atapokelewa kama mwanachama mwingine yeyote, hataingia moja kwa moja kwenye chumba cha kulala kwasababu ni mtoto wa Wassira ila atakaa sebuleni kama wageni wengine wote na akionekana anapepesa macho sana itabidi apelekwe upenuni akapunge upepo.
 
Makamanda hawaokotezi ila kila mtu mjanja hufuata penye uhai na neema.Utafuataje panapokufa?
 
Mtoto wa Wassira rudi Tanzania kamrithi mzee Bunda.
 
kuna tofaoti gani ya chadema na ccm wote wapo kwa maslahi ya kanisa
 
Historia inatuambia kuwa Wassira aliwahi kujinga na chama cha upinzani (NCCR MAGEUZI).Pengine siku za mwisho za CCM zikikaribia anaweza kuwa mwanachama wa CHADEMA.


Umesahau kwenye mazishi ya kamanda Bob Nyanga Makani? baada ya Mukama kuchemka, Kamanda Mbowe alimtaja Wasira kuwa ni miongoni mwa waasisi wa cdm, kabla ya kutimkia NCCR na kuukwaa Ubunge?
 
Duh!Afadhali nadhani sasa yale matusi ya kufananishwa na mnyama yatapungua kutoka CDM kwa kumstahi huyu mtoto wake!
 
Sidhani. Ni kama Mhe. Rachel Mashishanga (CDM) na baba yake Stephen Mashishanga.
 
kama kuna kitu chadema wanapaswa kuangalia si nani anaingia kwenye chama la hasha! ......wanachotakiwa kufanya ni kuhusu nani ahusike wapi na kwa kazi ipi?! nafikiri si kila mtu anayetoka ccm anaiongezea chadema umaarufu tayari chadema ni maarufu sana wakati huu sasa tunataka waelekeze kazi yao kwenye mkakati zaidi maana tunaona katika watu kumi maarufu ambao chadema iliwapata toka CCM watu saba kati ya hao
wamekuja ama wanafanya kazi sahihi ya kujituma kuhakikisha yafutayo
1kuwa chadema kinakuwa chama kisichoaminika
2taswira ya chama kwa raia ionekane kama chama kisichokuwa serious ila maigizo
3wanapenda chama kionekane kama hakina mfumo rasmi ila kila mtu ni msemaji
4ama wanataka nafasi za karibu na viongozi wa juu hasa za majungu dhidi ya wanachama wengine hata kuingia kimapenzi ili mradi wapate nyeti
5wako tayari kuona chama kinakufa kama wanalotaka halitekelezwi
mfano SINGIDA kuna mgombea alihama kutoka CCMakapitishwa moment aliuza jimbo mara 1
SHIBUDA ni tatizo kuliko kitu chochote ndani ya chama kwa sasa
mh RACHEL masishanga huwa ni miongoni mwa watu wanaotazama ubunge wao tu na si chama ni mdau wetu mzuri kwenye fb na mitandao mingine kushawishi vijana wadogo kutukana chama ANAUNGANA NA WATU WANAOTUKANA CHADEMA KUWA NI CHAMA CHA WACHAGA TENA waziwazi
JOSEPH SELAISIN NAYE ANACHOFIKIRIA HATUKIJUI BARABARA
 
Tabia ya unafiki sio nzuri, siasa sio kabila kwamba baba yako akiwa mchaga na wewe ni mchaga. Mtoto wa wasira anahaki kwenda chama chochote. Tena ninyi mbona wazazi wenu wako vyama vingine lakini hamsemi. Umasikini wa mawazo huleta umaskini wa vipato. Jadilini ya maana siwatu
 
huyu sio mtoto wa waziri steven wasira..... Ni mtoto wa kaka yake.

Amewaingiza chadema choo cha kike...
 
Back
Top Bottom