Mtoto wa mjini Ndiye Mshamba wa mwisho mjini

Mtoto wa mjini Ndiye Mshamba wa mwisho mjini

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,793
Reaction score
7,170
Kukiwa kuna ubishi mwingi wa watu waliozaliwa mjini ni wajanja sana kuliko waliozaliwa kijijini, ubishi huu umekuwepo tangu enzi za mababu lakini siku hizi ndio imethibitika kuwa, wengi wanojiona ni watoto wa mjini ndio washamba zaidi kuliko waliozaliwa kijijini.
Kwanza watoto wengi waliozaliwa kijijini wamepata virutubisho vyote vinavyotokana na matunda, majani, dawa za kienyeji, ndizi mbichi na mbivu, karanga kupata vitamini zaid kupitia jua , mayai ya kienyeji ya kanga, kuku na samaki wa haina zote, hivyo uwafanya wakue vizuri na kuweka akiba ya akili nyingi , ambavyo huwapeleka kuwa vinara kwenye uongozi wa juu pindi wapatapo madaraka baada ya kumaliza shule. Tena watu hawa huwa ni wafnyabiashara wazuri sana mjini, kwani hukutana na hali ngumu ya maisha ambavyo ujenga akili ya kujinyanyua , ndio maana wengi wamefanikiwa kimaisha. Wakati watoto wa mjini, hawapati virutubisho vya kutosha kutokana na umaskini uliotukukuka, mlo mara moja, mapambano ya kati ya konda wa daladala. hivyo uonekana ni watu wa vurugu kama vile kuvuta bangi sigara, utoro shuleni, vibinti kuanza mapenzi kabla ya umri wake. Watoto hawa hutegemea sana urithi wa nyumba au vibanda vilivyojengwa na baba zao, hupenda kujenga vijiwe vya umbeya kama vile kucheza bao, kuzingira maclabu mbalimbali kama vile vijiwe vya mpira na nk. watu hawa huwa hawajishughulishi na uzalishaji kwani wengi wana dharau kazi, uendekeza ushirikina hivyo kuwafanya waache kimaendeleo na watu wa kuja kutoka mikoa mbali mbali kama vile moshi, arusha kagera, mtwara, kigoma mbeya na songea. Watoto wamjini wengi hawajui jiographia ya nchi kwa vile hawajawahi kutembea nje ya mji wao hivyo kuwafanya wawe washamba wa vyombo kama vile meli treni, magari makubwa, ndege na mabasi.
Nahitishisha kwa kusema kuwa watoto wa mjini ndio washamba wa mjini kwa kuwa wao ndio wanuza mali za mababu zao na kusogezwa zaidi kuwafanya wanaoitwa washamba kuwanunua kwa kasi zaidi. Kama kuna ubishi rejea watawala hasa mawazir, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa wote wamezaliwa vijijini.
 
Pole sana ndugu wa kijijini. Ukizaliwa mjini tayari form 6. Kumbuka jogoo wa shamba hawiki mjini. Angalia JK huyo hapo kakulia magomeni na vijiwe vyake kariakoo. Ndio anamaliza awamu yake ya pili ya uongozi. Watu wa shamba wanapiga kelele tu.angalia na UHURU kenya ndio ameingia kenya. Mtoto wa mjini mwenye DIPLOMA ni sawa na profesa aliyetokea mikoani.

Mfano mdogo tu angalia watu wa mikoani wanavyouana sababu ya wanawake {tena wabaya}. Mfano huko arusha kina Ambrisye, mwanza IGP etc..... Usichezee mjini kabisa
 
Kukiwa kuna ubishi mwingi wa watu waliozaliwa mjini ni wajanja sana kuliko waliozaliwa kijijini, ubishi huu umekuwepo tangu enzi za mababu lakini siku hizi ndio imethibitika kuwa, wengi wanojiona ni watoto wa mjini ndio washamba zaidi kuliko waliozaliwa kijijini.
Kwanza watoto wengi waliozaliwa kijijini wamepata virutubisho vyote vinavyotokana na matunda, majani, dawa za kienyeji, ndizi mbichi na mbivu, karanga kupata vitamini zaid kupitia jua , mayai ya kienyeji ya kanga, kuku na samaki wa haina zote, hivyo uwafanya wakue vizuri na kuweka akiba ya akili nyingi , ambavyo huwapeleka kuwa vinara kwenye uongozi wa juu pindi wapatapo madaraka baada ya kumaliza shule. Tena watu hawa huwa ni wafnyabiashara wazuri sana mjini, kwani hukutana na hali ngumu ya maisha ambavyo ujenga akili ya kujinyanyua , ndio maana wengi wamefanikiwa kimaisha. Wakati watoto wa mjini, hawapati virutubisho vya kutosha kutokana na umaskini uliotukukuka, mlo mara moja, mapambano ya kati ya konda wa daladala. hivyo uonekana ni watu wa vurugu kama vile kuvuta bangi sigara, utoro shuleni, vibinti kuanza mapenzi kabla ya umri wake. Watoto hawa hutegemea sana urithi wa nyumba au vibanda vilivyojengwa na baba zao, hupenda kujenga vijiwe vya umbeya kama vile kucheza bao, kuzingira maclabu mbalimbali kama vile vijiwe vya mpira na nk. watu hawa huwa hawajishughulishi na uzalishaji kwani wengi wana dharau kazi, uendekeza ushirikina hivyo kuwafanya waache kimaendeleo na watu wa kuja kutoka mikoa mbali mbali kama vile moshi, arusha kagera, mtwara, kigoma mbeya na songea. Watoto wamjini wengi hawajui jiographia ya nchi kwa vile hawajawahi kutembea nje ya mji wao hivyo kuwafanya wawe washamba wa vyombo kama vile meli treni, magari makubwa, ndege na mabasi.
Nahitishisha kwa kusema kuwa watoto wa mjini ndio washamba wa mjini kwa kuwa wao ndio wanuza mali za mababu zao na kusogezwa zaidi kuwafanya wanaoitwa washamba kuwanunua kwa kasi zaidi. Kama kuna ubishi rejea watawala hasa mawazir, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa wote wamezaliwa vijijini.
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya Mtoto ambaye Kitovu chake kimetupwa migombani kikaliwa na FISI na yule ambaye kitovu chake kimetupwa baharini kikaliwa na SAMAKI......hehehehe #Team Downtowners


Sent from my BlackBerry Z10 using JamiiForums
 
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya Mtoto ambaye Kitovu chake kimetupwa migombani kikaliwa na FISI na yule ambaye kitovu chake kimetupwa baharini kikaliwa na SAMAKI......hehehehe #Team Downtowners


Sent from my BlackBerry Z10 using JamiiForums

kwa yuleni kitovu kilicholiwa na samaki ni mvivu sana na anapenda sana kurithi bila kufanya kazi
 
kwa yuleni kitovu kilicholiwa na samaki ni mvivu sana na anapenda sana kurithi bila kufanya kazi
mgt software kwani hapa tunazungumzia class ipi ya maisha? Maskini au Matajiri?
Kumbuka hata vijijini kuna wazee wenye pesa na watoto wao hurithi mali inapotokea mzee hayupo,Hivyo hivyo hata Mijini.
Anyways Najiongelea mimi kama mimi Mtoto wa Kabwela niliyezaliwa mjini ukipiga hesabu ya Ada yangu ya shule kuanzia std 1 mpaka Form 6 sidhani kama inafika Laki tano au imepitiliza kidogo.Inshort sikuwa na cha kurithi zaidi ya elimu(elimu ya mtaani(mjini) +ya darasani=PHD.
Yani hapa nilipo nautafuta uprofessa
NOTE:BORA MVIVU AMBAYE KITOVU CHAKE KIMELIWA NA SAMAKI KULIKO MVIVU AMBAYE KITOVU CHAKE KIMELIWA NA FISI...Mjini ni mjini tu ndugu yangu trust me.
 
Pole sana ndugu wa kijijini. Ukizaliwa mjini tayari form 6. Kumbuka jogoo wa shamba hawiki mjini. Angalia JK huyo hapo kakulia magomeni na vijiwe vyake kariakoo. Ndio anamaliza awamu yake ya pili ya uongozi. Watu wa shamba wanapiga kelele tu.angalia na UHURU kenya ndio ameingia kenya. Mtoto wa mjini mwenye DIPLOMA ni sawa na profesa aliyetokea mikoani.

Mfano mdogo tu angalia watu wa mikoani wanavyouana sababu ya wanawake {tena wabaya}. Mfano huko arusha kina Ambrisye, mwanza IGP etc..... Usichezee mjini kabisa

Pole sana,
Duh sikuwahi kufikiri kama bado kuna watu wenye upofu wa fikira kama wewe,
Sikia dsm si kila kitu kwa kila mtu, kama ni wa kuelewa utakuwa umeelewa sana!!
 
Jamaa sijui anawaza nini? Ukizaliwa mjini form six? Labda div zero! Mi nimezaliwa mjini ila wajanja wametoka vijijini wamevijenga viwanja vyote tulivyo kuwa tinacheza mch
ezo wa kujificha. Nyie kuleni unga usiofaa kwa ugali ndo form six yenu.
 
sijaelewa kama mleta mada anawazungumzia Wazaramo ambao wananyang'anywa ardhi na watu wa mikoani nasasa ata KONGOE inataka kuwa ya watu wa mikoani na hao wanaojiita wamjini wanaelekea muhoro, mkuranga
 
duh... afadhali mimi sijazaliwa mjini wala kijijini, nimezaliwa hospital ya ocean road, wengine baado kabisa ....
 
kama umezaliwa mjini hasaa kariakoo au ilala jua kuwa kanyumba kako kananyemelewa na mie kukanunua we taja tu bei uone mtoto washamba aliyekuja na treni kutoka mpanda nitakavyo kanunua
 
Pole sana ndugu wa kijijini. Ukizaliwa mjini tayari form 6. Kumbuka jogoo wa shamba hawiki mjini. Angalia JK huyo hapo kakulia magomeni na vijiwe vyake kariakoo. Ndio anamaliza awamu yake ya pili ya uongozi. Watu wa shamba wanapiga kelele tu.angalia na UHURU kenya ndio ameingia kenya. Mtoto wa mjini mwenye DIPLOMA ni sawa na profesa aliyetokea mikoani.

Mfano mdogo tu angalia watu wa mikoani wanavyouana sababu ya wanawake {tena wabaya}. Mfano huko arusha kina Ambrisye, mwanza IGP etc..... Usichezee mjini kabisa

Ni Kweli wanaojidai wamezaliwa Mjini ni washamba Dana
 
Nenda masaki mikocheni mbezi nk wamiliki wa nyumba Kwa asilimia 98 hawajazaliwa mjini wahadhili vyuo vikuu,madaktari bingwa,Mawaziri, wakuu Wa majeshi,asilimia 99 ya viongozi si wazaliwa Wa mjini
 
mbona mnazungumzia dar pekee? Ipo miji mingine mikubwa tu (ingawa si kama dar) sisikii maoni yake. Au haistahili kua miji?
 
Ha ha ha nahisi hii thread itakesha ngoja waje wabeba mabox maana watoto wa mjini wakishafeli shule tu wanakimbilia kukwea pipa kwenda kubeba box..

Mimi mtoto wa Town primary downtown Forodhani lakini nakubali watoto wa shamba wanatisha kwenye kuchakalika, asilimia kubwa ya watoto wa town wanabebwa na wazazi wao tu na network zao.. Lakini ukisema kila mtu asimame kivyake watoto wa shamba hawafai.. Wana hasira na maisha vibaya mno
 
Ha ha ha nahisi hii thread itakesha ngoja waje wabeba mabox maana watoto wa mjini wakishafeli shule tu wanakimbilia kukwea pipa kwenda kubeba box..

Mimi mtoto wa Town primary downtown Forodhani lakini nakubali watoto wa shamba wanatisha kwenye kuchakalika, asilimia kubwa ya watoto wa town wanabebwa na wazazi wao tu na network zao.. Lakini ukisema kila mtu asimame kivyake watoto wa shamba hawafai.. Wana hasira na maisha vibaya mno

Kusoma kwako forodhani hakukufanyi ukawa na hadhi ya kuwa mtoto wa mjini inawezekana kabisa wewe ni mtoto wa shamba na ukaingia forodhani kimakosa au msaada wa mjomba/shangazi. Na ndio maana unashindwa kuelewa na kuchambua vitu . Na kuwa mtoto wa mjini au ku fail shule hakutoshi kukufanya upande ndege kwenda kubeba box nje .unasema wamebebwa na wazazi wao . Hiyo ni chuki na wivu wa kike .hivi mzazi akiwa na uwezo na akajua uthamani wa elimu na maisha ya nje na akaamua kumpeleka mwanae nje je hapo amembeba.inaelekea wewe una chuki sana na kubaki kwako bongo. Nyie ndio mkishamaliza kidploma chako ukapata kazi ya kuchomekea shati na kamshahara ka laki tatu na nusu kwa muhindi ,ukakopeshwa ka used VITZ. na ukapanga kachumba kako self container sinza basi unaona maisha umeyapatia kifuatacho hapo ni vikao vya harusi hongera bar eti maisha mazuri unaoa. Kuwa mtoto wa mjini ni zaidi ya kwenda ulaya . Kuna watoto wa mjini wako ulaya na wanaishi ki mjini mjini. Na kuna wamjini wengine walibaki bongo wanaishi kimjini mjini. Kama umetoka shamba hata uwe na degree 100 huwezi kuwagusa . Kwani wao ndio mji na ndio kila kitu. Uliza upewe mifano . Kwahiyo watoto wa mjini wa wakuja haitakuja kutokea wakafanana upeo
 
kama umezaliwa mjini hasaa kariakoo au ilala jua kuwa kanyumba kako kananyemelewa na mie kukanunua we taja tu bei uone mtoto washamba aliyekuja na treni kutoka mpanda nitakavyo kanunua

Hata ungeinunua london yote kama wa shamba ni wa shamba tu. Ushamba hauwezi kumtoka mtu sababu ya pesa au elimu. Ushamba ni asili na u mjini ni asili pia
 
Mtoa uzi hapo kwenye lishe na virutubisho utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watoto wanaozaliwa vijijini wanaathirika na utapiamlo (lishe duni).
 
Nenda masaki mikocheni mbezi nk wamiliki wa nyumba Kwa asilimia 98 hawajazaliwa mjini wahadhili vyuo vikuu,madaktari bingwa,Mawaziri, wakuu Wa majeshi,asilimia 99 ya viongozi si wazaliwa Wa mjini
Ndio maana huduma zinazorota, wanaleta ushamba ktk utendaji
 
watu wa mjini wamekulia katika mazingira tata sasa wakija town wakapata chance huwa wanajitahidi sana kulipizia ili wasahau shida zao na si kweli kwamba wanauchungu na maisha ndo maana hata utendaji serikalini unakuwa wa shida mtu alikuwa analala na mbuzi leo kawekewa mabililioni kwanini asiibe
 
Back
Top Bottom