Mtoto frank wa Dodoma anahitaji msaada,

Mtoto frank wa Dodoma anahitaji msaada,

Lukwangule

Senior Member
Joined
May 25, 2009
Posts
157
Reaction score
2
Nyie mmeangalia taarifa ya habari ya TBC1 leo jioni saa mbili kuhusu mtoto mlemavu ambaye kichwa chake kinaning'inia na anajitahidi kuishi kama kawaida lakini hawezi kukaa analazimika kusimama akisoma? Nyie nyie kijana anaitwa Frank Mungu wangu madaktari wapo wapi? Huyu mtoto anateseka sana. familia maskini na serikali nayo sijui maskini? Lakini watu ni matajiri wa roho je hawawezi kurekebisha tatizo hili ambalo huyu mtoto hakuzaliwa nalo? Mimi najisikia vibaya sana
 
umeme ulikatika tunaomba kama una picha utuwekee
 
Jamani hii habari imenitoa machozi kweli hujafa hujaumbika ..nafikiria jinsi gani ya kumsaidia mtoto huyu vile mola atakavyonijaalia ..
Preta huyu mtoto alianguka kutoka juu ya mti lakini jinsi anavyoendelea kukua ndo anazidi kupinda yaani hawezi kukaa ni kusimama tu ...
mwenye picha atuwekee tafadhari
 
Nilijikuta nasali kumwombea huyu mtoto, sijui wana JF tufanyaje jamani tumsaidie huyu mtoto, nadhani mchango wetu unahitajika sana jamani. Kwa kweli kumwona binadamu na hasa mtoto anateseka namna ile nikiwa kama mzazi inauma sana.
 
HUWA NI VIGUMU SANA KWA WANAUME KUTOA MACHOZI.....!Nilinynyuka taratibu nikaenda chumbani....nilipotoka hakuna pale sebuleni aliyetambua nilichokuwa nakifanya chumbani........!Nilikimbuka UJAMAA/SOCIALISM..........kuwa ndiyo jibu la mtu wa chini na wa kati.........!Isingekuwa CAPITALISM POLICY ya COST-SHARING kijana FRANK...(WAPO NA WENGINE WENGI TU) asingekuwa katika hali ile....! KISIASA.......lets rethink to revive UJAMAA KIROHO.......TZ tumrudie MUNGU KIUCHUMI.....watendaji waliingusha sera ya ujamaaTUWASAIDIE WENYE SHIDA WENGINE PIA...!
 
Jamani hii habari imenitoa machozi kweli hujafa hujaumbuka ..nafikiria jinsi gani ya kumsaidia mtoto huyu vile mola atakavyonijaalia ..
Preta huyu mtoto alianguka kutoka juu ya mtu lakini jinsi anavyoendelea kukua ndo anazidi kupita yaani hawezi kukaa ni kusimama tu ...
mwenye picha atuwekee tafadhari

A u serious?????😕😕
 
Kwa kweli mtoto analiza. ni kusimama muda wote akiwa darasani na hawezi kucheza michezo kama ya wengine.
 
Back
Top Bottom