Mtoto aliyezaliwa na kupewa jina la Fiston Mayele

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,700
9,779
Naona nchini Tanzania uhuru umeanza kuzidi, na watu wanaibua vitu vya kijinga kila kukicha!

Assume wazazi wanafanikiwa kupata mtoto, wanakaa, wanajadili jina la mtoto wao, wanaamua kumuita jina ambalo hata kwenye mfumo wetu wa majina wa Tanzania, Africa na dunia kiujumla haupo!

Mzazi anaitwa Mkulungwa Masasa (Baba), Sajlath Madaa (Mama), mnapata mtoto mnamuita Fiston Mayele
N.B: Majina ya wazazi tajwa hapo juu siyo halisi
Halafu kwenye cheti cha kuzaliwa cha mtoto
Baba: Mkulungwa Masasa
Mtoto:Fiston Mayele
Hii yote ni kwa sababu ya ushabiki wa kijinga! Wazazi wanafikiria wakati huu, na hawamfikirii mtoto kabisa!

Hivi ikitokea katika maisha yake cheti chake kikahitajika, hivi atazungumza nini ili aeleweke? Shuleni atumie Fiston Mayele, kwenye application ya loans chuo kikuu jina la baba lisomeke Mkulungwa Masasa, hata kama mimi ndo loan officer namnyima mkopo!

Sijui wazazi wengine wamekula maharage ya wapi! Fiston Mayele Mkulungwa Masasa, haiingii akilini! Sijui kwenye kitambulisho cha taifa, NIDA, huyu mtoto atawaeleza vipi ili wamwelewe!

Wazazi mbadilike,

Ziada: Muache kuwapachika local names watoto wenu, wakikua wanayakataa, wanaleta shida! Eti, Mabolo Mkuyenge, haki ya nani hata kama mimi ndo mtoto ntalikataa!

Screenshot_20220530-074422.jpg

Nawasilisha:
 
Mkuu,
kwenye cheti cha kuzaliwa
Baba: Mkulungwa Masasa
Mtoto: Fiston Mayele Mkulungwa Masasa

Angekuwa na akili angemwita angalau Mayele! au Fiston! Moja tu linatosha!
Surname: mayele
First name: fiston
Last name: mkulungwa.
NB: majina mawili ni ya mtoto na moja LA mzazi. Huo ndio utaratibu wa kupeana majina sasa majina mawili ya mzazi ya kazi gani?
 
Surname: mayele
First name: fiston
Last name: mkulungwa.
NB: majina mawili ni ya mtoto na moja LA mzazi. Huo ndio utaratibu wa kupeana majina sasa majina mawili ya mzazi ya kazi gani?

Babu wa mtoto hana nafasi!

Hii nchi tunakoelekea sasa!
Kama mimi ndo babu wa mtoto, au basi!
 

Babu wa mtoto hana nafasi!

Hii nchi tunakoelekea sasa!
Kama mimi ndo babu wa mtoto, au basi!
Hana kabisa. Kwani mtoto ni wake? Labda mtoto aitwe kwa jina lake
MF: masasa fiston mkulungwa.
Kumaanisha masasa ni surname ya mtoto ambalo pia ni jina LA babu yake.
 
Nadhani kuna namna inapaswa kujiuliza ni wapi tulipokosea na ikiwezekana kurekebisha kabla haijawa mbaya zaidi.

Kama taifa la leo liko hivi vipi la kesho??
 
Hiyo cha mtoto nilienda Musoma kikazi kuna zoezi tulienda kufanya ikiwemo kutembelea baadhi ya wakazi vijijini ....Kuna mtu watoto wake wawili wa kiume first names ni International football players ila ubin wa baba
 
John Pombe Joseph Magufuli

Mizengo Kayanza Peter Pinda

Fiston Mayele Mkulungwa Masasa

Haya makolo semeni hao wa kwanza na wa pili walipata shida gani hadi muone huyo wa tatu ni shida?
 
Mkuu,
kwenye cheti cha kuzaliwa
Baba: Mkulungwa Masasa
Mtoto: Fiston Mayele Mkulungwa Masasa

Angekuwa na akili angemwita angalau Mayele! au Fiston! Moja tu linatosha!
Mkuu mtoto sio lazima atumie jina la baba kama Sirname, kwenye cheti cha kuzaliwa huwa kuna line inaandikwa jina la mtoto, la baba na mama. Kama jina la mtoto ni moja kama ulivyosema wewe mfano aitwe Fiston, basi jina kamili litasomeka kama Fiston Mkulungwa Masasa ila kama kimeandikwa Fiston Mayele atakuwa huru kutumia Fiston Mayele Mkulungwa Masasa au Fiston Mayele Mkulungwa au Fiston Mayele Masasa.

Hata wewe ukitaka unaweza kumpa mtoto majina unayotaka, mfano vyeti vya zamani vilikuwa vina nafasi mbili juu ni jina la mtoto na chini kabisa kuna nafasi ya jina lingine. Ilikuwa kawaida kwa wengi unakuta ana jina la nyumbani na jina analotumia shule hivyo kuna wengine waliyaandika yote kwenye cheti cha kuzaliwa , moja lina appear kwenye kipengele cha jina la mtoto na la pili lina appear kama jina lingine. Akiandika lile jina lingine analiweka katikati na la ukoo. (akipenda analipotezea lile lingine haliandiki kwenye matumizi ya kawaida ila kwenye cheti linakuwepo ila siku hizi naona wameweka line moja hivyo ukiandika lazima uyatumie yote)

Ila kwa vyeti vya sasa unayaandika yote kwenye line ya jina la mtoto hata ukitaka majina matatu yote
 
Back
Top Bottom