JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,300
- 5,434
Familia moja Jijini Mwanza imeonesha jinsi ilivyo na mahaba na mshambuliaji Fiston Mayele wa Klabu ya Yanga, baada ya kumpa jina mtoto wao linaloendana na mchezaji huyo raia wa DR Congo.
Kwa ufupi ni kuwa mtoto huyo naye anaitwa Fiston Mayele, siyo kwamba ni jina la utani, HAPANA, ni jina hali halisi.
Mashabiki hao wakiwa na cheti halisi cha jina la mtoto huyo kinachosomeka Fiston Mayele walionesha hadharani na pia wakapata nafasi ya kukutana na Mayele mwenyewe original kisha kupiga naye picha na kumbeba mtoto huyo.
Mayele alikuwa Mwanza pamoja na timu yake ambapo walicheza mechi dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mei 28, 2022.
Mama mzazi anaitwa Sundi John Kalumbi wakati jina la baba mtu ni Victor Maguta Ndulu, wakazi wa Nyamagana. Mtoto huyo alizaliwa Januari 17, 2022.