Los santos
JF-Expert Member
- Jan 14, 2021
- 961
- 2,038
Mtoto Shamsudini Jamadu Msemo (13), aliyemwagiwa mafuta ya taa na kisha kuchomwa moto na mama yake mzazi, amefariki dunia leo Jumanne Oktoba 3, 2023 katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) alikokuwa akipatiwa matibabu.
Agosti 31, mwaka huu mtoto huyo ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Reli Juu, wilayani Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro, alidaiwa kufanyiwa ukatili huo baada ya kuchukua fedha za mama yake na kwenda kununua viazi vya chips na kisha kupika na kula wakati alipohisi njaa.
Inadaiwa kuwa, baada ya mama yake kubaini mwanaye huyo amechukua fedha zake, alimfunga mikono na miguu kwenye mti ambao upo nyumbani kwao na kisha kumuagiza mtoto wa jirani kwenda kununua mafuta ya taa na ndipo alipotenda tukio hilo la kikatili.
Ikiwa zimapita siku 34 tangu mtoto huyo afanyiwe ukatili huo na mama yake mzazi, mpaka sasa hajulikani alipo huku Jeshi la Polisi likiendelea kumsaka bila mafanikio.
Hata hivyo, baada ya mtoto huyo kufikishwa katika Hospitali ya KCMC kwa ajili ya matibabu, wataalam wa majanga ya moto hospitalini hapo walibaini kuwa mwili wa mtoto huyo uliungua kwa asimilia 65 kutokana na majeraha ya moto aliyopata.
Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi
#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa
Agosti 31, mwaka huu mtoto huyo ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Reli Juu, wilayani Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro, alidaiwa kufanyiwa ukatili huo baada ya kuchukua fedha za mama yake na kwenda kununua viazi vya chips na kisha kupika na kula wakati alipohisi njaa.
Inadaiwa kuwa, baada ya mama yake kubaini mwanaye huyo amechukua fedha zake, alimfunga mikono na miguu kwenye mti ambao upo nyumbani kwao na kisha kumuagiza mtoto wa jirani kwenda kununua mafuta ya taa na ndipo alipotenda tukio hilo la kikatili.
Ikiwa zimapita siku 34 tangu mtoto huyo afanyiwe ukatili huo na mama yake mzazi, mpaka sasa hajulikani alipo huku Jeshi la Polisi likiendelea kumsaka bila mafanikio.
Hata hivyo, baada ya mtoto huyo kufikishwa katika Hospitali ya KCMC kwa ajili ya matibabu, wataalam wa majanga ya moto hospitalini hapo walibaini kuwa mwili wa mtoto huyo uliungua kwa asimilia 65 kutokana na majeraha ya moto aliyopata.
Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi
#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa