mtihani mzito

Habari zenu wanaJF. Wife leo kapigiwa simu, unajua mambo ya wivu nikauliza aliyepiga simu ni nani ? Akasema kwa kuwa nataka kujua aliyepiga simu tubadilishane simu (pamoja line zake) yeye achukue ya kwangu na mimi nichukue ya kwake kwa muda wa wiki moja. Ameng'ang'ania hilo swala na mimi nina vimeo kwenye simu yangu yaani sijui la kufanya kujiepusha na hili. Msaada wa mawazo unahitaji kuninasua katika hili.

Kuna wanawake wanapenda sana ligi. Kwani angejibu kwamba huyo aliyempgia ni nani si yangekwisha? Au kashagundua kwamba una vimeo ndio maana amekuwa mkali.

Sasa mkishaanza kushindana kwa staili hiyo sasa hivi mtaruvuga ndoa yenu. Halafu wewe kwenye simu yako usituambie kwamba una vimeo vingi kiasi cha kushindwa kutumia muda wa leo kuwa block wote. Kisha kesho mbadilishane tu simu, uone kama na kwake hutakuta yasiyotarajiwa! Kwanza una moyo wa kuvumilia utakayoyaona kwenye simu yake?!?
 
Badilisheni tu wala haina tabu mwenye idadi kubwa ya wapenzi atajulikana. na baada ya hapo mfikie makubaliano kuanzia sasa tuache kila mmoja adelete kwenye simu yake na kuanza maisha mapya.
 
yeye achukue ya kwangu na mimi nichukue ya kwake kwa muda wa wiki moja. Ameng'ang'ania hilo swala na mimi nina vimeo kwenye simu yangu yaani sijui la kufanya kujiepusha na hili. Msaada wa mawazo unahitaji kuninasua katika hili.

Nadhani ni wazo zuri na njia bora ya kutibu kama unaumwa ugonjwa wa kutokuwa mwaminifu...Haina haja ya kumficha ..mpe simu yako.. na hizo Klorokwini lazima uzimeze....ili upone.. otherwise, utaendelea kuumwa hadi unakufa...

Bora umpe simu Mama ili ujue hatima yako mbele ya Pilato..Mimi binafsi nitapiga kelele usulubiwe..lakini kuna baadhi wataomba usamehewe..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom