Leo nimesikia maelezo ya Mawakili watano waliomuwekea pingamizi Rais anayemaliza muda wake Ndugu Karia. Binafsi maelezo yao yana mashiko. Hivi kweli Rais anayeheshimika kwa nini asifuate taratibu na kanuni.
Kama ilivyo sheria na taratibu za TFF mgombea wa Urais wa TFF sharti ni kuwa adhaminiwe na wajumbe wasiozidi watano na wajumbe wote wanaotakiwa kutoa udhamini wako 47. Sheria na taratibu za TFF zinaendelea kueleza kuwa mjumbe yeyote akishatoa dhamana yake kwa mgombea HAWEZI tena kumdhamini mgombea mwingine.
Kama nilivyosema jumla ya wajumbe wanaotoa dhamana wako 47 na Rais anayemaliza muda wake amewazungukia wajumbe 46 waliomdhamini na kubakia na mjumbe mmoja tu. Sasa kwa mtu mwenye busara, hekima, upendo na mshikamano huo utaratibu aliouchukua Rais anayemaliza muda wake kweli ni sahihi?.
Kwa nini Rais anayemaliza muda wake hataki ushindani?. Binafsi naona HAFAI kuendelea kuwa Rais wa TFF kama kweli alifanya njama ili wenzake wasishindane naye.
Kama ilivyo sheria na taratibu za TFF mgombea wa Urais wa TFF sharti ni kuwa adhaminiwe na wajumbe wasiozidi watano na wajumbe wote wanaotakiwa kutoa udhamini wako 47. Sheria na taratibu za TFF zinaendelea kueleza kuwa mjumbe yeyote akishatoa dhamana yake kwa mgombea HAWEZI tena kumdhamini mgombea mwingine.
Kama nilivyosema jumla ya wajumbe wanaotoa dhamana wako 47 na Rais anayemaliza muda wake amewazungukia wajumbe 46 waliomdhamini na kubakia na mjumbe mmoja tu. Sasa kwa mtu mwenye busara, hekima, upendo na mshikamano huo utaratibu aliouchukua Rais anayemaliza muda wake kweli ni sahihi?.
Kwa nini Rais anayemaliza muda wake hataki ushindani?. Binafsi naona HAFAI kuendelea kuwa Rais wa TFF kama kweli alifanya njama ili wenzake wasishindane naye.