Mtei akoleza moto wa Mnyika

Mtei akoleza moto wa Mnyika

Mzee Mtei taingia atoe ile kauli yake ya usawa wa dini alionyesha udhaifu mkubwa sana..
 
Mnyika kwa sasa ni famous kuliko hata JK.
ccm hawakujifunza kutokana na Lemma.
 
Kweli kabisa Mnyika ameonyesha uthubutu wake mapema ila wengine wote wakiwemo media watasema sana JK akimaliza muda wake hapo ndipo utasikia hata yasiyosemwa!!

Kabisa huyu jamaa ni dhaifu, na niniwasi na uadilifu wake.
 
Mzee anazeeka vibaya,mara kwa mara amekuwa akitoa matamko yanakidhalilisha na kukipunguzia umaarufu chama chetu cha makamanda.kauli yake nyingine ni ile kuhusu tume ya katiba mpya kuwa imejaa waislam.


Nilitegemea kabisa wazee wa chama wangekuja na msimamo unaowarudisha vijana wetu katika mstari maana wao ndio walezi wetu,matokeo yake mzee amejisaidia mezani.
 
siku zote wazee huwa ni moderators,lakini imekuwa tofauti kwa mzee wetu mtei,uzee unamuijia vibaya mzee wetu,ashauriwe asiwe anawahi/anakurupuka kutoa matamko
 
Kama budget ya upinzani ni nzuri au mbaya, hiyo si hoja na wala siyo sababu itakayomfanya JK aonekane ni kiongozi jasiri.

Udhaifu wa JK ukianza kuorodheshwa itakuwa ni makala ndefu sana. Udhaifu wake zaidi upo katika vision, strategies, planning and supervision. Katika hivyo vyote ameonesha udhaifu mkubwa. JK ametufanya wote tushindwe kujua tunataka na tunajenga Taifa la namna gani. JK ni kiongozi ambaye anaongoza nchi kwa unafiki bila msimamo na ndiyo maana hata viongozi wa chini yake hawaelewi wafanye nini maana hawajui anataka nini, anatafuta kupendwa na wevi na wanaoibiwa, wachapa kazi na wavivu, wanaouchukia udini na wanaoupenda, wanaouchukia mwungano na wanaoupenda, wanaovunja sheria na wanaotaka utawala wa sheria, n.k. Kiongozi hustahili kuwa hivyo, ni lazima ueleweke unataka nini na unasimamia nini, na hiyo ndiyo huacha landmark yako katika Taifa.

Viongozi wote makini Duniani hueleweka misimamo yao, haijalishi itakuwa mizuri au mibaya. Lakini huwezi kuwa kinyonga, mtu usiyeeleweka unataka nini na unasimamia nini. Unatamka kuwa unataka utawala wa sheria, lakini Magufuli akisema atabomoa nyumba za wale wote waliokiuka sheria ya barabara, unasema tena, ooh hapana usifanye hivyo. Wewe kweli ni kiongozi unayesimamia sheria? Tunasema wahujumu uchumi na mafisadi wapelekwe kwenye vyombo vya sheria, wewe tena unasema, tukipeleka wahujumu uchumi wote mahakamani uchumi utayumba. Huku unawaambia wananchi kuwa tumewapa meno TAKUKURU lakini nyuma ya pazia unawaambia wasiwapeleke watu fulani fulani (rejea taarifa za Weakleaks).

Rais wetu hata kama tukitaka kumtetea namna gani, ukweli ni kuwa ni dhaifu sana, na anayependa kujipendekeza kwa kila mtu. Kiongozi hustahili kuwa hivyo, unatakiwa uwe na msimamo, na hapo ndipo utawatafuta wasaidizi wanaoendana na msimamo wako, nao watakuwa na ujasiri wa kusimamia ambayo wana uhakika ndiyo unachosimamia.

Mkuu usisahau aliwahi kutamka hadharani kuwa "wauza unga" wote anawajua, ila akawataka waache vinginevyo atawashughulikia! Miaka inazidi kusonga mbele na wenyewe wanatamba mitaani!! Tuna bahati mbaya sana wa-Tz!
 
tulipofikia Tanzania bila watu wenye kudhubutu kama Mnyika na wengine basi swala la ukombozi wa kweli litakuwa gumu sana.MUNGU TUNAOMBA VIONGOZI WENYE HEKIMA NA WENYE KUJALI WENGINE.AMEN
 
wazee na waasisi wa mageuzi wanaunga mkono matusi bungeni,ni jambo la aibu sana
 
Kwani rais kazi yake ni kuwatia ndani wezi?
Na hiyo bajeti ya upinzani ina tofauti gani na bajeti ya serikali?

Kaa hapo karagabaho Rais akisema mtu akamatwe atakamatwa na akisema asikamatwe hakamatwi rais alishasema warudishe hawatashitakiwa sasa hapo napo unataka mwalimu wa kukufundisha jambo dogo kama hilo.Halafu ujue kambi ya upinzani haiongozi nchi so hata bajeti yao ikiwa mbaya au nzuri aina madhala kwa maendeleo ya taifa.
 
attachment.php

attachment.php
 
Ni kwa asiyemjua huyu mzee tu ndio atakayesumbuka, anajulikana kwa tabia yake ya kujadili watu kwa majina yao.

Hana tija kwa taifa letu apuuzwe.
 
Jk & chama chake cha majambazi ni dhaifu kwa Taifa letu!

Ila hakika nawaambia mwisho wao waja.

Zaliwa 1977
Zika 2015
 
Tukiachana na mambo ya bajeti, mimi nataka wana JF wanifafanulie EPA ilihanzishwa kwa madhumuni gani?

EPA = External Payment Arrears. Ni account maalum ilifunguliwa BOT wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kulipia madeni ya nje. Madeni haya yalitokana na nchi kutokuwa na fedha ya kutosha ya kigeni kununulia bidhaa nje. Wafanyabiashara wa ndani walipotaka kununua bidhaa kutoka nje (kumbuka unaponunua bidhaa nje unahitaji fedha ya kigeni makaratasi yetu hayachukuliwi) walilipa kwa pesa yetu equivalent ya ile ya nje wanayotaka kununua bidhaa then serikali inakuwa inadaiwa na suppliers wa nje.

Bahati mbaya madeni yaliyo mengi hayakulipwa wakati ule kutokana na serikali kutokuwa na fedha za kigeni kulipa kwa wakati ule. Mengi ya makampuni yaliyokuwa yanadai fedha kutoka kwenye account hiyo yalifisika, mezwa na makampuni mengine makubwa nk. kabla hayajalipwa. Sasa wajanja (wezi) wetu waka chukua advantage hiyo na kuanza kufanya transaction hewa kupata hizo fedha.

Hiyo ndio EPA.
 
Yeye alipokuwa waziri wa fedha alifanya kubwa lipi kwa Tanzania, ni mlafi alieutaka uongozi kwa nguvu, na kwa kudhihirisha hivo ukuu wa chama akampa MKWE WAKE bwana mbowe! chama cha kifamilia! na kubwa pale aliposemea uwingi wa waislamu katika mchakato wa katiba ilhali anajua fika kuwa idadi ile imeongezeka kwa kuwa kuna wanaotoka zanzibar je mtu huyu SI DHAIFU! watu kama hawa wakipewa nchi wataufanyia nini umma wa watanzania! toa boriti katika jicho lako kwanza ndio utoe la jirani yako! hana sera huyu mzeee
 
Kwa picha hii tuna uhakika hakuna baya lolote litamtokea kijana wetu , tunaushahidi wa huyu jamaa

Hapa ina maana Mh. Lukuvi anamuomba jamaa kifaa cha CDM ili asiipinge tena bajeti. Kama kawaida yao magamba wanampa vitisho ili aogope.


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
pambav zake,wewe utakuwa umezaliwa miaka ya 90,humjui nyerere unamsikia tu.Tuulize sisi tuliokuwepo enzi za utawala wake wa udikteta.Acha kuropoka dogo unamezeshwa maneno unatapika.Unataka kuchokoza machungu yetu dhidi ya huyo mzee mchonga meno
Mh!Tupate wapi tena mtu kama Nyerere,mwenye uchungu sio kama JK yaani maisha magumu anasababisha yeye.Au amechoka kazi?
 
Back
Top Bottom