S.Liondo
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,408
- 1,713
Pamoja na kwamba mimi na CCM ni kama Moshi na Pua, lakini kuna mbunge mmoja wa CCM ambaye taratibu ninajikuta nikianza kumkubali. Huyu si mwingine ila ni Mbunge wa Ludewa Mh. Deo Filikunjombe. Mheshimiwa huyu amekuwa mjasiri kusimamia kile anachoamini kuwa ni sahihi hata kama ni tofauti na msimamo wa chama chake. Kwakweli anajiamini na wala haogopi vitisho na mashinikizo ya chama chake. Nakumbuka kwamba yeye ni mmoja wa wabunge waliotia sahihi wakati Mh. Zitto alipokuwa anatafuta sahihi za wabunge ili kumwajibisha Waziri mkuu. Leo hii pia amepiga kura ya wazi kupinga azimio la "kura za siri na za wazi". Ametamka neno "Hapana" kuonyesha hakubaliani na msimamo huo japo ndio wa chama chake kwa sasa. Mimi ninaamini kama wana-CCM wote wangekuwa kama huyu bwana basi tungekuwa na serikali murua. Hongera Mheshimiwa Deo Filikunjombe.