Mtanzania: Hali si shwari Zanzibar; Pemba yataka uhuru kamili

Hili halikwepeki ni lazima litatokea pemba kujitenga na mi sioni kama linaathali kubwa saaana, tuanze kufikiria hili lililobaya zaidi la Chuki za kidini linalokua kwa kasi ya kutisha.
 
kizazi kilichopita walikuja na sera za "mapinduzi daima",kizazi kipwa wamekuja na "zanzibar kwanza" cha kujiuliza kwanini kizazi kipya kimeugeukia msimamo wa wazazi wao,je kizazi kipya hakija nufaika na mapinduzi,je kizazi kipya hakija faidika na muungano..........?
 
Nadhani bado hujapata kifungua kinywa mama! Hapo ni kuonyesha watu wanajadiliana kutengana wakiwa bado wako chini ya mwamvuli wa muungano, je muungano ukivunjika si itakuwa balaa!?

Hizo ni fitna za huo mungano baada kuona umoja wa znz unatishia ukoloni wa Tanganyika kwa wa zanzibar.
 
wwe ni muongo, mnafik, mzandik, hakuna sehmu yyote wapemba wanadai Pemba yao cku zote wapemba wamekuwa mstari wa mbele kuidai Zanzibar, wwe unachuki na wapemba kwa sababu waliodai hayo mamlaka ni waunguja badilisha kichwa cha habari kisomeke unguja wanataka mamlaka yao, kwa cc wazanzibar tunasema hao ni wahuni wa ccm na mamluki wa Tanganyika wala hawatupi shida kuelekea mamlaka kamili ya Zanzibar, wanataka kututoa nje ya mada but wamechelewa hzo ndo siasa za ccm zimepitwa na wakati waendelee kutoa povu lkini 2015 tunataka Tanganyika na Zanzibar zenye mamlaka kamili bila chama cha majambazi aka ccm inawezekana.
JK kaleta mambo! Kila mtu sasa ni mzandiki! Yote kwa yote siyo mimi bali ni kauli za wapemba wenyewe! Waunguja nao wanalia nchi yao kuvamiwa na Wapemba!

​Kazi kweli kweli!
 
Tusiendekeze upuuzi kama huu. Ni lazima tuelewe kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Tukiendekeza hili la leo, kesho na keshokutwa tutasikia Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma nao wanataka kujitenga na kudai uhuru kamili.
​Kwani hukuwahi msikia marehemu Nandonde akidai Mtwara kujitenga na kuungana na Msumbiji!
 
Wewe wacha uongo, ni wapi FaizaFoxy alipomtukana Nyerere? Mimi sikubaliani na mambo mengi sana ya Nyerere lakini siwezi kumtukana yeye wala wewe.

Akipingwa Nyerere nyinyi mnaona ni matusi? wacheni ulimbukeni.

Nyerere alikuwa binadamu kama wewe na mimi na yeye mwenyewe kakiri kuwa alikuwa na makosa na hakuwa malaika. Sasa wewe kama nani wa kuniona mimi nisiyekubaliana na siasa na utawala wake kuwa nnamtukana?

Hata hili mnaloliongelea la Pemba kakosea sana, soma vizuri wanavyoongea utajuwa kuwa hili linaongelewa ndani ya Muungano na kabla ya Muungano.

Ni kipi cha ajabu mnachokiona hapo? wakati hayo aliyosema Nyerere hakuyaota wala si ya ajabu yalikuwepo, Upemba na Uzanzibari haukuanza leo wala jana, ni asili. Kama mlikuwa hamjui muelewe hayo.

Wala hakuna cha maana isipokuwa inadhihirisha kuwa Nyerere hakuwa na muono, anasema nje ya muungano wakati hayo yanaongelewa ndani ya muungano, huo muono uko wapi hapo?

Naona Udini wako umekupofua hata huwezi tumia facts za msingi kutoa hoja. MUUNGANO upi unaongelea? Hivi sasa hakuna Muungano hata kidogo ni Ujirani mwema tu ama urafiki wa mashaka. Katiba ya Zanzibar inajieleza vizuri wameishajitoa ktk Muungano bali hawataki kuachia marupurupu ya Muungano km vile kuwa na maeneo makubwa waliyoodhi huku bara, viongozi wao kusafiri kwa gharama za Tanganyika, kama Maalimu seif alivyokwenda Manyara na Rukwa na kupokelewa na viongozi wa Tanganyika kutumia raslimali za Tanganyika. Lakini Nchimbi alivyokwenda Zanzibar kufuatilia ugaidi nafikiri ulimwona alivyong'aka kuwa Zanzibar ina wenyewe. Vile vile nyie wazenj mpo wengi huku bara mkifanya kazi ktk serikali ya Tanganyika lakini wakati huo huo mnalalamika kuwa sisi tunawabana kwenu zanzibar tuondoke , ndo maana wadau wengi wanadai kuwa hayo ni mambo ya nchi ya kigeni.

Hivyo ujue Nyerere alikuwa Kichwa na alikuwa na maono sana wewe tu chuki zako (zenu). Kama umefika Zanzibar (hivi karibuni maana wengi wenu mpo huku bara mkijifanya wazaliwa wa Tanga, lakini lazima mjue kuwa kuna siku itaanzishwa Operation Kimbunga ya hali ya juu) utakuwa umesikia juu ya kauli kuwa "Sisi Jodari, wao Vibua" hizi ni kauli za kejeli ambazo mzee mmoja alinieleza kuwa kabla ya Muungano hali ya ubaguzi ilikuwa mbaya sana kati ya hawa unaowatetea may be nawe ni mmoja wao.
 
Let Zanzibar Go, Tumechoka na Vitimbwi Vyao, tuachane nao na tujenge Tanganyika yetu.
Historia inaonesha kuwa Tanganyika hatujawahi kuwa na Ubaguzi kabla na hata Baada ya Uhuru na Muungano.
 
Mimi nadhani haya yamepitwa na wakati tunatakiwa tukae tujenge taifa letu siku zote wosia wa baba na mama ni muhimu katika familia hivo WOSIA WA NYERERE NA MZEE KARUME Ni MUHIMU

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Ayo mambo ya nyerere alisemaje bila kuangalia alisema kipindi gan ni akili za kuazimwa cha msingi je kwa sasa kuna aja ya kuendelea na muungano? Mm nasema no need mosi wanasiasa wetu wameproove kuwa kwa ukubwa wa tanganyika tuu ni kazi kutimizi mahitaji ya wananchi wote kumbuka ukichukua kenya,uganda,burundi na rwanda bado tanzania kubwa kuzidi nchi zote zi kiungana rejea soviet state ilivotengana unaona ilivo go forward
 
Tatizo ni wapemba Dk Shein na Maalim Seif kupewa hako kainchi,waunguja awakutaka kabisa hao wapemba wapewe hiyo nchi kwa sababu awakushiriki mapindunzi.Vinginevyo ni upepo tu utapita.:A S-confused1:
 
Wewe ndiyo unaleta utani!. Mwl. Nyerere kwenye swala la Zanzibar kujitenga hakujenga hoja kwa kuona mbali, bali alitumia historia kwa njia ambao ionekane kama anajenga hoja kwa kuona mbali wakati alichokuwa anafanya ni ku-rewind historia na kumbusha tu ambao hawakuijua au waliosahau.

Ukisoma vizuri hii article atagundua kuwa matatizo yalikuwepo na yaliendelea kuwepo chni ya kapeti kwa vile kuyatoa nje ni kupambana na kosa la uhaini ndani ya katiba ya nchi. Kamuulize Mzee Aboud Jumbe na Maalim Seif Shalif Hamad watakueleza nini maana ya hiki ninachokisema

Tusipende kutoa sifa na pongezi kwenye jambo ambalo halistahili.

Ndiyo maana ya historia. Kama ww hilo hulijui utaona Mwalimu anasifiwa bure.
 
Tatizo ni wapemba Dk Shein na Maalim Seif kupewa hako kainchi,waunguja awakutaka kabisa hao wapemba wapewe hiyo nchi kwa sababu awakushiriki mapindunzi.Vinginevyo ni upepo tu utapita.:A S-confused1:
Ni ajabu na kweli! Kwa hiyo Waunguja wanataka watawale Zanzibar wenyewe milele!!??
 
Mimi ni mchache wa historia, naomba nifahamishwe hivi hapo mwanzo kulikuwapo muungano wa Pemba na unguja ndio ikazaliwa zanzibar iliyoungana na Tanganyika kuzaa tanzania? au huu uhusiano wa Pemba na unguja ukoje?
 
Tusiendekeze upuuzi kama huu. Ni lazima tuelewe kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Tukiendekeza hili la leo, kesho na keshokutwa tutasikia Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma nao wanataka kujitenga na kudai uhuru kamili.

Kwani kuna shida gani? Baada ya halmashauri kuwa na mamlaka kamili zitaungana kuwa the Federal Government of Tanganyika.
 
DHAMBI YA UBAGUZI,ni sawasawa na Kula nyama ya mtu!WAZANZIBAR wanaendelea kula nyama ya WATU!
 
Baba wa Taifa aliona Mbali sana,dhambi ya ubaguzi haiishi kamwe.. kumbe Pemba na Unguja sio wamoja tena, na hawajawai kukubaliana kuwa pamoja.

Muda sio mrefu tutashuhudia Pemba ikiwa ngome kuu ya Allshababi.

Ili kuikoa Zanzibar dawa ni Serikali moja Ya Tanzania.!


masuala ya zanzibar ni magumu sana hebu kwanza tuwaache ndugu zetu huru ili wakishindwa warudi tena kwetu.:A S-confused1:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom