Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,872
- 11,337
Sasa mbona unaanza kututukana Mkuu? Kuna watanzania waliokana utanzania wao na wako ambao hawajaukana. Ukweli ni huo. Naona sasa unataka kubisha tu ili mradi ushinde.Mnadanganywa ndio maana mnaitwa WADANGANYIKA. Hakuna Mtanzania anayeishi nje aliukana Utanzania kwa sababu kuna process na balozi zetu hujulishwa pale mtu anapoukana Utaifa wake.
Hutakiwi kusikiliza parapanda za vucuzela ukaamini pasipo kutumia akili yako. Mtu akiukana Utanzania leo hii Serikali ya Tanzania itajulishwa kuwa mtu huyu kwa jina hili, passport namba hii sio tena raia wa Tanzania na pasi yake inarejeshwa Tanzania. Unaachia Passport ya Tz, Ndio utararibu wa Kimataifa. Sasa Waulize list hiyo kama wanayo.
Hapana sijatukana isispokuwa penye ukweli tuuseme, sisi Wadanganyika. Kikwete alitaka kuuza pwani yote Kwa mkataba wa bandari ya Bagamoyo hakuna Mtanganyika wala Mzanzibar alosema huyu Mtanganyika kauza nchi, tena kibaya zaidi wakamtukana Magufuli alotufumbua macho. Leo kinatokea kitu kama kile kile tayari watu wanadai Tanganyika ilihali utawala ni ule ule, watu hawa utawaitaje?Sasa mbona unaanza kututukana Mkuu? Kuna watanzania waliokana utanzania wao na wako ambao hawajaukana. Ukweli ni huo. Naona sasa unataka kubisha tu ili mradi ushinde.
Amandla...
Kwanini ?Mtanganyika ndio Mtanzania
Kwahiyo limo wapi ?Duni Haji: Jina Tanzania halimo Kwenye Hati ya Muumgano [emoji3]
Hapana sijatukana isispokuwa penye ukweli tuuseme, sisi Wadanganyika. Kikwete alitaka kuuza pwani yote Kwa mkataba wa bandari ya Bagamoyo hakuna Mtanganyika wala Mzanzibar alosema huyu Mtanganyika kauza nchi, tena kibaya zaidi wakamtukana Magufuli alotufumbua macho. Leo kinatokea kitu kama kile kile tayari watu wanadai Tanganyika ilihali utawala ni ule ule, watu hawa utawaitaje?
Swala la Diaspora waloukana Utanzania ni nchi ambazo pia hazitambui Uraia Pacha inambidi muombaji aukane kwanza Uraia wa nchi yake. Kama wapo mimi sijui na sii Diaspora tena.
Kwa sababu hawa hata wakiomba Uraia wa Tanzania lazima kwanza waukane wa huko walikopewa nje ya hapo hakuna Diaspora aloukana Uraia wake na akabakia na passport ya Tanzania.
Na Maana ya Diaspora sio Uzawa bali ni raia wa nchi fulani aishie Ughaibuni. Waisrael wote ni rais wa Israel hata kama wana uraia wa nje na ndipo jina hili lilipianzia. Kama nakosea nambie
Msingi wa Tanganyika ni chuki dhidi ya uzanzibari, ni jeuri ya kutaka kuonyesha na sisi tuna chetu ambacho tuna haki ya kukiringia.Katika mila na desturi za Kiafrika kuna maswala ambayo yamehodhi jadi za matukio ambayo yaliakisi Makabila hayo kujinasibisha na mahala kuwa makazi yao ya asili kutokana na fursa zilokuwepo.
Na historia ya makabila haya imetokana na koo zile zile za Wakulima, Wafugaji na Wavuvi kutengana aidha kutokana na vita, ukame, maradhi, maafa ama kuhamia sehemu nyingine salama wakitafuta riziki zao.
Wakati mwingine Uwindaji, malisho bora ya mifugo ilikuwa sababu pia ili mradi hesabu kamili ya utu wa mwafrika hautokani na nchi bali tumeshehena mila na tamaduni zinazofanana kama jamii ya Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wawindaji na Wachuuzi waloishi kama jamii eneo moja likaitwa nchi yao.
Kwa mukhtadha huo, mbali na uzio wa Makabila ya asili kuna Utaifa ambao ni jumuiko la watu wenye makabila yao wakiishi pamoja ndani ya himaya moja kutokana na shinikizo la mahitaji mbali mbali ya Ujima na biashara. Kwa maana hii tunaposema Tanganyika ni eneo la nchi ambalo wakazi wake wana makabila mbali mbali wakiishi kama jamii moja bila kujali asili zao ama walitoka wapi.
Hivyo basi, naposikia watu wakidai Tanganyika ya Watanganyika, hunielemea hoja ya kutaka kujua haswa tafsiri halisi ya madai haya na wakazi wake! - Mtanganyika ni nani?
Je, Mtanganyika ni kizazi cha watu walozaliwa kabla ya Muungano wa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar ama ni Wakazi wa leo wa Tanzania bara ambao hujinasibu kama wao ni wazawa wa bara? Bila shaka inaswihi tunapodai Tanganyika ni vema pia tukawajua warithi wake yaani Watanganyika ni kina nani?
Na kama sikosei mwaka jana niliandika makala nyingine nikiuliza MZANZIBAR ni Nani? Na sababu haswa zinatoka na tafsiri hasi isokuwa na historia nyuma yake isipokuwa kwa kutumia jina la nchi ili kutambua Watu wake. Kwa mfano Wakerewe sio Kabila bali kisiwa ndicho kinaitwa Ukerewe na wakazi wake wakaitwa Wakerewe.
Kuna hadithi nilipewa inasemekana asili ya Wakerewe ni Mkoa wa Kagera ama niseme jamii ya Wahaya waliokimbia Kagera baada ya ndugu wawili watawala wa kabila moja kupigana vita, kisha ndugu mmoja kukimbilia kisiwa cha Ukerewe kupata hifadhi na usalama wa watu wake.
Lakini pia Ukerewe haikuwa visiwa pekee bali utawala wake ulikuwa hadi nje ya visiwa hivyo mpaka sehemu ya Mkoa wa Mara haswa Mwibara ambako kuna makabila ya Wakwaya, Wajita, Waruri ambao pia naambiwa ni jamii ya Wakerewe. Na wao pia wakagawanyika katika koo nyingi zikaunda makabila mengineyo mengi kutokana na muingiliano na koo nyingine za kijamii.
Aidha hadithi hii iwe na ukweli ama laa hasha, lakini ndivyo makabila mengi yametokana na miingiliano ama migogoro ndani ya jamii moja kutengana na kisha kuzaliwa kwa kabila na himaya tofauti lakini zenye asili ya nasaba moja.
Na kwa bahati mbaya sana ndivyo yalivyo Makabila mengi ya Tanganyika na hata Zanzibar pia, nchi hizi hazikutokana na Utawala. Chukulia Utawala wa Zanzibar na Oman, ni urithi wa ndugu wawili watawala ambao sii tu wana asili moja bali walikuwa ndugu wa damu, isitoshe baba yao Said bin Sultan yeye pia aliikuta Zanzibar tayari ikiwa na wakazi wake. Zanzibar haikuwa Zanzibar kwa kutawaliwa, watawala waliikuta Zanzibar - Nasherehesha tu.
Nirudi katika hoja yangu ya leo, ndugu zangu Watanzania nawaasa sana tuwe makini sana na hii mihemko ya Utanganyika na Ikumbukwe kwamba Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa katika moja ya hotuba zake akisema haya:-
"Tunataka Rais ambaye si Mkabila, si Kaburu. Makaburu wa Tanzania ni wale wanaojiita wazawa. Ni makaburu tuu, mimi siwaonei haya hata kidogo ni makaburu tuu.
"Kwa sababu kama una mawazo yaleyale kama ya kaburu wa South Afrika ila tofauti yako kwamba ni mweusi ni kaburu tu."
" Wazungu wa South Afrika tulikuwa hatuwapingi kwa rangi yao, tulikuwa tunawapinga kwa Ubaguzi wao. Hatuwezi kuwa na makaburu hapa halafu tukawaheshimu kwa sababu weusi. Ni Makaburu tu"
- Mwisho wa nukuu
Kwa undani wa nasaha hii ya mwalimu imegawanyika sehemu mbili ambazo hatumhitaji kiongozi wa aina hii MKABILA au KABURU na wote kwa ujumla wanahodhi sifa za KIBAGUZI. Aidha atajali watu wa kabila lake na atawatenga watu wengine katika haki na maendeleo yao.
Na tunapodai Tanganyika ni Tanganyika ipi?
1. Ile kabla ya Mjarumani.
2. Ya Mjarumani yenye nchi za Burundi na Rwanda,
3. Ya Muingereza alokabidhiwa na Umoja wa Mataifa baada ya kugawanywa vipande.
4. Au Tanganyika ya miaka mitatu ilopewa Uhuru na Muingereza na kutambuliwa na Umoja wa Mataifa kuwa kigezo tusikubali badiliko jingine lolote la Utaifa baada ya Muingereza!.
- Ni Tanganyika ipi tunayodai?
Hivi ni kweli Tanganyika haikuwepo hata kabla ya ukoloni mpaka ilipogumbuliwa na mzungu aitwaye Speke ambaye hata jina Tanganyika halikuwa katika ulimi wala lugha yake! Nini chanzo na maana ya Tanganyika ikiwa sisi wenyewe hatufahamu asili yake isipokuwa ile tulofundishwa na Wazungu.
Ndugu zangu, Mwalimu Nyerere siintu alituasa bali ametuachia tunu kubwa ya Utaifa wetu kuwa nchi hii inaitwa Tanzania. Ni jina walochagua waasisi wetu na wakaamua wenyewe kuunganisha nchi zetu mbili kama ilivyo asili ya ndoa zetu tukazaliwa sisi. Hatuwezi badilisha Ubini wetu kwa sababu ya urithi wa mali.
Tuwaenzi viongozi wetu mwalimu Nyerere na Sheikh Abeid Karume kwa kuheshimu kazi kubwa waloifanya kabla ya Uhuru na baada ya Uhuru kwa sababu walitambua umuhimu wa Muungano wetu sii wa dini wala Makabila bali jamii ya WATU wenye tofauti zao.
Kuhitilafiana kupo hata kwa ndugu hutokea lakini katu kizazi hakiwezi kupoteza historia yake kwa matakwa ya mali na urithi. Tusitumie mapungufu na makosa ya baadhi yetu kuwa sababu ya utengano kwa sababu hakuna Mtanganyika wa Miaka mitatu tu (1961-1964) isipokuwa unatokana na asili ya wazazi watu.
Tuwaheshimu wazazi wetu
Maasalaam.
Limo katika katiba ya jamhuri ya Muungano wa TanzaniaKwahiyo limo wapi ?
Jina la Tanzania halitakiwi kisheria kuwa ndani ya hati isipokuwa nchi zinazoungana. Kwa afeika nzima ni sisi tu tumeweza. Isitoshe jina ni jina tu mnaweza badilisha wakati wowote kwa nchi ile ile hata kama hati ya Uhuru imeandikwa jina jingine.Limo katika katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanza
Tumepewe na wakoloni kivipi una maana wao ndio waanzilishi kabisa kabisa wa Jina Tanganyika? Ninachojua Mimi Walipotugawanya Afrika kwa % kubwa walikuta majina yapo.Ulosema yote nakuelewa na nakubali nawe lakini kilichokosekana hapo nini? jina tu la Tanganyika ulopewa na mkoloni ndio unalilia. Sasa ndugu yangu wewe utakula jina? Kuwa na jina Tanganyika utafaidika na kipi au fahari ya macho! maana unapoomba kitu ujue faida na hasara zake.
Jina tu la Tanganyika kweli au kuna jingine? Kwani tukiitwa Tanzania Bara (Tanzania Mainland) kinapungua kitu gani? Acha wao wajiite Zanzibar sijui Wazanzibar ni fahari kwao lakini inawagharimu. Kwangu mimi hiyo ni Tanzania Visiwani, Zanzibar ni mji.
Kuwa na rais wanamlipa, baraza la Wawakilishi wanalipwa na kodi zao kifupi Serikali nzima inalipwa na wananchi wakati Ofisi moja ingeweza kuhudumia Bara na Visiwani. Mzee Karume akiwa Makamu wa rais alifanya mambo mengi makubwa kuliko hawa viongozi wote waliofuatia.
Cancer ya Mwafrika ni fikra za Ukabila na Udini tu. Unakuta tunapugania kwa nini Mawaziri wengi Wakristu! Je anapokuwa Muislaam anawasaidiaje Waislaam? Mimi sijaona iwe, Mwinyi Kikwete au Mama Samia na Mawaziri wote wanafanya kazi ya Chama na sii kabila wala dini.
Hata hivyo viti maalum kwa Wanawake ni Ujinga mtupu ikiwa wanawake hao hawahusiki na maswala ya Wanawake.
Kwangu mimi Tanganyika ni uzao wa MKOLONI yaani nchi ilogawanywa kwa mfumo wa divide and rule tukazipoteza Rwanda na Burundi. Leo hii tuna wakimbizi wengi kutoka Burundi na Rwanda raia wa Tanzania tofauti yetu ni mipaka tu.
Siku tutakuwa na Tanganyika, basi ujue hatutakuwa salama kesho. Mikoa ya kanda ya Ziwa Geita na Mara watajitoa kwa sababu dhahabu yao inachukuliwa kwa jina la Tanzania na Tanganyika.
Mtwara nao watadai Gas yao kwa sababu fikra ni zile Ile kugawana URITHI kwa kisingizio cha NCHI
Kumbuka tu kabla ya Mjarumani hatukuwa na Tanganyika. Bara iliongozwa na Machief wake ambao mpaka kesho wanataka watambuliwe. Libya leo hii Machief ndio viongozi mbali na Serikali ilosimikwa. Ugonvi hauishi kwa sababu ya Mafuta..
Nitakujibu kwa kifupi sana. Niliwahi kusoma makala moja ya historia ya kina Speke na Burton wakiwa wakizungumzia utafiti wao wa chanzo cha mto Nile na kufika ziwani (Tanganyika). Walidai kuwa chanzo cha jina hilo kwa lugha yetu ikiwa na maana ya "sail in the Wilderness". Wakati wakizunguka ziwani wasione mwanzo wala mwisho wake! Hivyo watafsiri wakasema Sail = Tanga na Wilslderness= NyikaTumepewe na wakoloni kivipi una maana wao ndio waanzilishi kabisa kabisa wa Jina Tanganyika? Ninachojua Mimi Walipotugawanya Afrika kwa % kubwa walikuta majina yapo.
Taabu au shida ilijitokeza kwa wazungu ilikuwa Ni kushindwa kutamka majina Kama walivyoambiwa na BABU ZETU:;
Mfano:-
Idodomia wao waksema Dodoma.
Masingida wao waksema Singida
Tararangir wao waksema Tarangire
Kilimanjaro,Arusha,Babati na mengine yalivyopatikana yametokea kwa kutofautiana matamshi.
Tuna mfano mwingine Jinsi Kijiji Cha KOLOMIJE mahali alipotokea MKUU wa Mkoa mstaafu - Makonda,Wasukuma walishindwa kutaja ipasavyo Jina la Mzungu aitwaye JONATHAN akawarahisishia kwa kuwaambia CALL ME J akijaribu kuwarahisishia namna ya kumwita bado wao ndio wakakorofa zaidi Badala ya kumwita J wakasema COLOMIJE [Call me J)
Utambulisho wetu Kama TAIFA HALISI na halali lililopata Uhuru mwaka Dec.9, 1961 Ni wa Jina lipi Sasa.
Kwanini utambulisho huo unatumika kwa TANZANIA ambayo imezaliwa kwa Muungano wa NCHI mbili - TANGANYIKA na ZANZIBAR 1964?
Kuna ujanja,Hila na upotoshaji wa namna tumeadhimisha Sherehe za Uhuru.Pia haijakaa sawa,Zanzibar wao wanasherehe yao ya Kupata Uhuru wao,AMRI JESHI MKUU anaufyata kwenye protocal hii Ni aibu haijakaa sawa kabisa.
Wengine tuliosoma Siasa while ya msingi tunaweza tusiwe na shida Sana lakini kizazi kisicho mjua NYERERE na KARUME.
Kizazi Cha instant coffee hawana subira,ninyi walafi madaraka na wapiga MADEAL kitawahukumu Asubuhi Kama so Mchana kweupe.
Msiliingize TAIFA kwenye majanga na uumwagaji wa damu usio wa Lazima.
Nini kinawashida kutengekeza HATA KATIBA MPYA ILI TUACHE WATOTO NA WATOTO WA WATOTO WETU KATIKA MIKONO SALAMA KWENYE KATIKA ISIYEMPENDELEA YEYOTE?
KATIBA iliopo inatoa mwanya wa kuiba chochote, iwe RASILIMALI, KURA NA MPAKA HATA MKE WA MTU na bado ukipita mtaani bado utaitwa mheshiwa.
Mnaipendea wapi TANZANIA?
Mpaka leo mikataba ya Hila Kama ya wakoloni wakizungu na waarabu walivyowafanyia BABU ZETU ndio bado IMESHAMIRI IKULU KWA SERIKALI YETU???
INAKERAAA SANAAAA!!??
Yaani wasichokitaka ni jina Tanganyika, lakini jina Zanzibar sawa sawa.Mkandara,
..kama jina Tanganyika linawakera basi tuitwe Tanzania Bara na tupewe serikali yetu.
..Na kwenye hati ya muungano jina Tanganyika libadilishwe na kuwa Tanzania Bara.
..Muungano wetu utambulike kama muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar.
..Kwa kifupi ni kwamba, huwezi kuwa na muungano wa nchi mbili, halafu usitambue, au ufute, utambulisho wa mmoja wa washirika wa muungano.
..Kuna mambo ktk muungano ambayo ukitaka kuyashughulikia, na ili HAKI itendeke, ni lazima washirika wa muungano wawepo mezani.