Mtandao wa SMILE punguzeni ujanja ujanja kwa watumia huduma zenu!

Himalaya

Senior Member
Mar 27, 2019
174
276
NAHISI KUNA BAADHI YA KUMPUNI NI CHUMA ULETE

Jana nilishawishika kununua Router kwa ajili ya matumizi ya kiofisi. Katika zunguka zunguka nikatumbukia kwenye kampuni ya Smile. Nikaelimishwa juu ya routers zao nikashawishika kununua moja. Kwakweli Routers zao ni nzuri sana na ni 4G. Zina kasi ya kufa mtu na kwahakika zinafaa sana kwa matumizi ya kiofisi. Lakini tatizo leo hawa jamaa wako so expensive kwenye Bundle zao kwa mfano bundle ya GB1 inauzwa kwa TZS 5000 na ukiweka bundle hilo utastaajabu ndani ya saa moja kwisha kabisa na ni matumizi ya kawaida tu.

Jana nililazimika kununua kifaa hiki kwa ajili ya matumizi ya kiofisi. Nikapewa GB 1 ya ofa, na mimi nikanunua bundle ya mwezi ya TZS 25000 na nikapewa GB 5 ukiplus na ile GB 1 ya offer nikapata GB 6. Sasa cha ajabu nilipoanza tu kuitumia chini ya masaa 24 bundle lote kwisha. Wakati mimi nilijua nitatumia mwezi mzima lakini wapi hola. Nikawaendea wakaniambia eti matumizi yangu ni makubwa wakati matumizi yangu ni yaleyale ya kiofisi tu kutuma email, kutafuta taarifa mbalimbali kwenye mitandao na wakati mwingine kurefresh youtube kidogo kitu ambacho nilikuwa nikikifanya before nikiwa na line yangu ya airtel ikiwa na GB 1 tu. Siku nikiamua kununua bundle la mwezi la GB 5 kwa TZS 15000 inakwenda mwezi mzima lakini kwa Smile licha ya bundle zao kuwa ghali hazikai zinawahi sana kuisha.

Baada ya kuisha lie bundle Mwezi, nikasema nifumbe macho, nijiribu tena kununua bundle la GB 1 kwa TZS 5000, ilikuwa majira ya saa 11: 02 lakini ilipofikia saa 12: 30 jioni ya leo bundle lote limekatika na sijaingia hata youtube zaidi ya matumizi ya kawaida tu ya kuperuzi kwenye mtandao wa Internet na kujifunza mambo kadhaa bila kudownload japo pdf poja.

Kwa siku mbili za matumizi ya kifaa hiki kwa hakika nimwanyoshea mikoni na siwataki tena, na nitakapi kwenye draw hadi watakapojirekebisha vinginevyo sitatoa tena hela yangu kununua bundle mana naona hawa jamaa wana kila dalili ya uchuma ulete.

Byebye Smile, sina hela ya kuchezea.

Aman Ng'oma
0767989713
DODOMA

C&P
IMG_20190925_222504.jpeg
 
Mkuu kama watumia PC za window 10 basi WINDOW imeupdate
window 10 kasi ya internet ikiwa kubwa inaupdate automatic na file mpk kumaliza si chini ya gb 6 mpk 10 Kama hujaupdate muda mrefu na huwezi kukataa
Ila km watumia window 7 turn off automatic Update

Jambo la kuzingatia YOUTUBE video ya dakika 3 inaweza ikalamba mb 500 wakati video ya dkk 15 ikatumia mb 50
Hvyo kablaa hujawalaumu SMILE fikilia tena unatumiaje vifaa vyako
 
Watu wengi wanakosea sana wanapotaka kununua modem au Router kwenye haya makampuni. Mambo ya kuzingatia unapotaka kununua Router au Modem inabidi uangalie ambayo ni Universal (Utakayoweza kutumia mitandao yote), kama ni ya kampuni angalia je, inaweza kuwa unlocked? Wewe unatumia Router au modem ya kampuni fulani ya simu halafu haichakachuliki. Hapo lazima ile kwako tu kwasababu haya makampuni yapo kibiashara zaidi yaani wanaangalia upande wao tu. Hapo ushapoteza pesa yako, ingekuwa ni universal ungeweka SIM Card ya mtandao wowote ukaaendelea na maisha lakini leo unaiweka kabatini.
Sasa hivi vifurushi zinapunguzwa kila siku. Enzi zile tsh 2000 unapata GB 5 kwa mwezi Vodacom lakini sasa 1000 unapata mb 200 masaa 24. Hiyo TTCL nayo utaipaki tu. Ukijumlisha hela uliyonunulia Router + Hela ya kifurushi = SIMU. Hiyo hela ya kununulia Router ya TTCL, ongezea ununue simu ya 4G halafu tumia WIFI HOTSPOT kwa ajili ya internet
 
Jana nililazimika kununua kifaa hiki kwa ajili ya matumizi ya kiofisi. Nikapewa GB 1 ya ofa, na mimi nikanunua bundle ya mwezi ya TZS 25000 na nikapewa GB 5 ukiplus na ile GB 1 ya offer nikapata GB 6.
Kwanza: Ilitakiwa ujue matumizi ya ofisi kwa siku/ wiki/ mwezi ni GB ngapi?

Pili: Ungeuliza hapa JF na ungepewa mapendekezo ya Mtandao wa kutumia na kifurushi kitakacho kufaa.

Tatu: Umechagua smile ila hukutaka kujua fifurushi rafiki walivyo navyo ni vipi?
- Badala ya kununua 1GB kwa TZS 5,000 - Ungeweza kununua SMILE daily kwa TZS 2,000 na unapata 1.5GB na ukapata
1569808422140.png

Hapa tatizo sio smile - Tatizo ni lako wewe binafsi hukufanya uchambuzi yakinifu kuhusu vifurushi vyao.

- Badala ya kununua 5GB kwa TZS 25,000, Badala yake ungeweza kununua 10GB kwa TZS 14,500 tu
1569808531246.png

Hapa tena tatizo sio smile bali ni wewe kutofaunya uchaguzi sahihi.

Bundle zao zote ziko hapa: https://smile.co.tz/data-bundles/ kwa uwazi kabisa wameweka bei na kiasi cha GB unachopata, ni swala la wewe kuchagua kile ukitakacho kulinganan na mahitaji yako.

1569808722492.png

Nimeandika hii post nikiwa connected na smile na kifurushi cha 10GB kwa TZS 14,500

Hitimisho.
- Kwa vifurushi vya internet kwa bei rafiki - kwa sasa TTCL hana mpinzani, unapata 10GB kwa TZS 10,000 weekly bundle ( T- Connect )
- Kwa speed kubwa ya internet ( hutegemea mahala ulipo ) kwa upande wangu mahala nilipo ni: Smile, TTCL na Vodacom
 
Hizi huduma za fibre zina unafuu wowote? Maana naona kuna mtu mmoja post za juu kasema anataka kuhamia kwenye fibre.

Na vile vile kama ukiwa na matumizi ya tuseme GB 60 kwa mwezi ni kifurushi gani kinakufaa?
Kwanza: Ilitakiwa ujue matumizi ya ofisi kwa siku/ wiki/ mwezi ni GB ngapi?

Pili: Ungeuliza hapa JF na ungepewa mapendekezo ya Mtandao wa kutumia na kifurushi kitakacho kufaa.

Tatu: Umechagua smile ila hukutaka kujua fifurushi rafiki walivyo navyo ni vipi?
- Badala ya kununua 1GB kwa TZS 5,000 - Ungeweza kununua SMILE daily kwa TZS 2,000 na unapata 1.5GB na ukapata
View attachment 1219213
Hapa tatizo sio smile - Tatizo ni lako wewe binafsi hukufanya uchambuzi yakinifu kuhusu vifurushi vyao.

- Badala ya kununua 5GB kwa TZS 25,000, Badala yake ungeweza kununua 10GB kwa TZS 14,500 tu
View attachment 1219214
Hapa tena tatizo sio smile bali ni wewe kutofaunya uchaguzi sahihi.

Bundle zao zote ziko hapa: https://smile.co.tz/data-bundles/ kwa uwazi kabisa wameweka bei na kiasi cha GB unachopata, ni swala la wewe kuchagua kile ukitakacho kulinganan na mahitaji yako.

View attachment 1219215
Nimeandika hii post nikiwa connected na smile na kifurushi cha 10GB kwa TZS 14,500

Hitimisho.
- Kwa vifurushi vya internet kwa bei rafiki - kwa sasa TTCL hana mpinzani, unapata 10GB kwa TZS 10,000 weekly bundle ( T- Connect )
- Kwa speed kubwa ya internet ( hutegemea mahala ulipo ) kwa upande wangu mahala nilipo ni: Smile, TTCL na Vodacom
 
Ni wapuuzi sana,nilinunua router yao ya LAN ukitoka tu maeneo ya town bar za signal inapunguza mpaka kupotea,hivi kweli kwa ushindani huu uliopo Service zinapatikana tu town,pembezoni hamna network,baada ya kuona ujinga huo,nimeachana nao,speed yao ya network ni nzuri tatizo ndio hivo coverage ni ndogo
 
Back
Top Bottom