Mtambuzi apata mtoto, Baby Boy

Mtambuzi apata mtoto, Baby Boy

sijui kama umekulia vijijini kama mie.

Tulikuwa hatuna mipira hii aina ya kuchezea tenesi.

Tulkuwa tunatumia mayai ya mijusi au nyoka fulani hivi kudunda dunda kama tenesi.

Ukifika umri kama huu wangu, mayai yanadunda tu na wala si unyanyapaa.

Pampzi tunapeleka wapi?

Utakuwa umesimuliwa wewe, mayai ya mijusi na nyoka umeyajulia wapi?

Pampers bila shaka zinapokelewa mtambuzi pub, tabata mtaa wa ubaya ubaya!
 
Ahsante mkuu kwa kufikisha taarifa MMU, maana ulikuwa kama vile unaangalia mechi ili kusubiri matokeo..... vile kipenga cha mwisho kinalia tu, ukaruka hewani......LOL

Mkuu wewe ni mtu wa watu sasa habari kama hizi sio za kuficha.
Basi nikaona si vibaya kuwashirikisha wadau ili mpate baraka zao.

Tuko pamoja sana mkuu kufurahia ujio wa a new baby boy!
 
Huyu Mtambuzi kumbe tapeli si amejitangazia uzee?? Mtoto wa nini sasa saa hizi??? Kuanzia leo wewe sio mzee yaani bado unatotolesha tuu??? Mie nimefunga miaka 16 iliyopita??? Kha!!!

Acha wivu shem, kwa maana imeandikwa ''Ee nendeni mkazae muijaze Dunia''
Kwahiyo Mtambuzi anatekeleza maandiko. Hata wewe bado hujachoka shem wangu unaweza kuongeza mwingine!

Wa uzeeni siunajua wanavyokuwaga wazuri!
 
eheeeee na uzee wote ule bado mtambuzi anazaa jamani
hongera bwana Mtambuzi
 
Last edited by a moderator:
hengera sana mtambuzi.
Kwa maujuzi uliyonayo nadhani mtoto atapata malezi mazuri.
 
Welcome to the world baby boy! A million of thanx to Mwita Maranya a.k.a 'M' square.

Tuko pamoja kamanda.
Mimi ndiye napokea zawadi za watu mlioko mikoani kwa niaba ya mzee mzima Mtambuzi!lol

Karibuni sana tujumuike kumpokea mtoto anayekuja kuchukua mikoba ya utambuzi JF.
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana Mkuu Mtambuzi namtakia makuzi mema mtoto wenu! Nimekuwa ni mmoja wa wafuatiliaji wakubwa sana wa mada zako mbalimbali unazoziletaga jamvini,kwa fikra zangu nilifikiri by now wewe upo umri wa kustaafu wa serikali kumbe yote yale huwa ni manjonjo tu ya kiuandishi! Hongera sana mkuu kwa mara nyingine.
 
Acha wivu shem, kwa maana imeandikwa ''Ee nendeni mkazae muijaze Dunia''
Kwahiyo Mtambuzi anatekeleza maandiko. Hata wewe bado hujachoka shem wangu unaweza kuongeza mwingine!

Wa uzeeni siunajua wanavyokuwaga wazuri!

Wivu wa nini sasa na wewe????

Mkaijaze dunia hata unamiaka 90????Hiyo ngumu kumeza haya bana hongera zake
 
Hongera Mtambuzi, nishaagiza kakontena cha vinepi na vyupi vya mikojo. Document niliziwasilisha tokea jana bandarini.
 
Nazidi kuamini humu JF wazee ni mimi na Dark City tu.

Kijana Mtambuzi hongera kwa kupata mtoto wa pili.

Kiongozi mbona umetaharuki.
Mtambuzi ni mzee mkakamavu kwahiyo usithubutu kumtenga.

Tunasubiri zawadi za mama na mtoto mtambuzi pub, tabata ubaya ubaya.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom