Mtambo wa kuchenjua Makinikia wakamilika kwa asilimia 95%. Watoa suluhu kwa wachimbaji wadogo na wakubwa na kudhibiti wizi wa dhahabu

Nyie mnafurahisha sana hebu, tuambie capacity ya huo mtambo, unajengwa na nani? Tends ya kumpata mjenzi ilitangazwa wapi? Bugeti ,yake ilipitishwa na nani??
Hiyo dhahabu mtamuuzia nani?
Maswali gani haya ndugu yangu? Nyie ndio wapenzi wenu wanapowapa style mpya mnaanza kuwapiga kwa kudai wamelala nje na kujifunza hizo style, right? Hamna shukrani.

Kuwa skeptical kwa kila kitu siyo kwa afya njema, otherwise na wewe ni kundi lile lililokuwa lipinga kuchenjua makinikia nchini kwa kigezo kuwa hatukuwa na teknolojia ya kujenga kiwanda cha uchenjuaji.
 
mnataka kuchenjulia makinikia mtachimba kwa machepeo ? wawekezaji wamejiondokea mmeachiwa mchimbe kwa sululu .
Hivi siku hizi umeamuakuwa raia wa nchi gani?
====
Narudi kwenye mada:
1. Kwa nini unaogopa kumiliki na kufanyia kazi rasilimali za nchi yako? kwa maneno mengine, kwa nini unaona ukakasi watanzania kumiliki uchumi wa nchi yao kwa kutumia rasilimali zilizopo wakati huo huo unaona/hisi utamu kwa rasilimali zetu kama nchi kumilikiwa na watu kutoka nje?
2.Je. dhahabu inayochimbwa na sululu inaupungufu wa thamani kwenye soko?
------
3.Kitendo cha wanaodhaniwa (kwa lugha za kisheria) kutudhulumu wakifungasha vilago hiyo naona ni nafuu kwa nchi kama hawataki kubadilika na kufanya win-win business.
 
Nilidhani kutokana na yale yaliyotokea kwenye sakata la makinikia huo mtambo utakuwa suluhisho... kumbe ni hadi hizo kampuni kubwa zitapohitaji?
Hivi sheria yetu si-imekataza kubeba mchanga na kwenda kuuza nje bila kuchenjuliwa? Ama nilisikia vibaya.
 
Mtambo wa Kuchenjua dhahabu uko mbioni kukamilika baada ya kufikia asilimia 95%. Mtambo huo unajengwa katika eneo la Lwamugasa, mkoani Geita.

Waziri wa Madini, Angela Kairuki alisema kuwa, lengo la mtambo huo ni kusaidia wachimbaji wadogo na wa kati lakini pia hata kwa kampuni kubwa zitajazohitaji kuchenjuliwa madini ya dhahabu.

Mtambo huo uliojengwa na Serikali utakuwa chini ya Shirika la Taifa la Madini (STAMICO) ambao watakuwa wasimamizi wakuu wa mtambo huo.

Hayo ni matokeo ya maagizo ya Rais Magufuli kufuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Kuchunguza Makinikia chini ya Profesa Mruma, iliyoshauri Serikali kujenga mtambo wake wa kuchenjua makinikia ili kuepuka kupoteza kiwango kikubwa cha dhahabu.

View attachment 951068

Hakuna walao hata "picha" ya kuonesha hicho "kiwanda"?
 
Au waliojenga mtambo huo hawajui makinikia ni nini au aliyeleta habari haelewi na hivyo ametoa taarifa ya uwongo.

Ukweli ni kwamba, zaidi ya kampuni ya Acacia, hakuma kampuni nyingine hata moja nchini inayozalisha makinikia. Tangu makinikia yakamatwe Dar mwakajana, Acacia waliacha kuzalisha makinikia.

Kama makinikia yanazalishwa na kampuni moja tu, na hiyo kampuni imeacha kuzalisha, huo mtambo utakuwa unaprocess makinikia ya kutoka wapi?

Kuna process ndefu ya kuzalisha makinikia (concentrate).
 
Ni shauri yao, wasipokuja kwenye mtambo huo itakula kwao kwani kwa sasa hatutaruhusu kupeleka makinikia nje ya Nchi. So wao wataamua ama kusuka au kunyoa.
Huelewi unachoongea. Kwa sasa hakuna kampuni hata moja inayozalisha makinikia. Inavyoelekea hujui makinikia ni nini.
 
Wange yapitisha yale makinikia yetu yalio zuiwa huko ili sisi wakina Tomaso tujue ukweli wa nini na kiasi gani cha dhahabu etc viko kwenye makinikia hayo ujulikane. Ni maprofessa au Acacia walikuwa wanasema ukeli? Professorial rubbish or Acacia thievery!!!!!! Washushe na data za kiuchumi.
Usiamini maneno ya mleta mada. Mpaka sasa, hatuna mtambo hata mmoja Tanzania wa kuprocess makinikia. Huyu anachoongelea ni mtambo wa kuyeyushia dhahabu (Gold Elution) kutoka kwenye carbon.

Shida ya watu wetu ni kujifanya wanajua sana hata pale ambapo hawajui kabisa.
 
Mtambo wa Kuchenjua dhahabu uko mbioni kukamilika baada ya kufikia asilimia 95%. Mtambo huo unajengwa katika eneo la Lwamugasa, mkoani Geita.

Waziri wa Madini, Angela Kairuki alisema kuwa, lengo la mtambo huo ni kusaidia wachimbaji wadogo na wa kati lakini pia hata kwa kampuni kubwa zitajazohitaji kuchenjuliwa madini ya dhahabu.

Mtambo huo uliojengwa na Serikali utakuwa chini ya Shirika la Taifa la Madini (STAMICO) ambao watakuwa wasimamizi wakuu wa mtambo huo.

Hayo ni matokeo ya maagizo ya Rais Magufuli kufuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Kuchunguza Makinikia chini ya Profesa Mruma, iliyoshauri Serikali kujenga mtambo wake wa kuchenjua makinikia ili kuepuka kupoteza kiwango kikubwa cha dhahabu.

View attachment 951068
Tunataka kujua yale matrilioni mlio twambia mtalipwa yameishia wapi?
 
Mleta uzi huu hujui lolote khsu uchenjuaji wa dhahabu.......
Usilete porojo na siasa kwenye mambo ya kitaalam!

Ova
 
Tupeane taarifa baada ya mwezi mmoja wa kufanya kazi..., baada ya watumiaji kuona ubora wake na mapungufu yake.
Ndio sisi wengine tupate cha kusema
 
Wakuu....
Nimejikuta napitia na kusoma huu uzi kwa umakini sana, na mwisho nimegundua kwamba.....
Hii habari ina upotoshaji ndani yake, kwasababu kadhaa. Hapa naona watu wengi wameshindwa kutofautisha makinikia na kifusi madini, na hili kosa nimeliona kuanzia kwa mwandishi wa gazeti, mahijiano na Waziri husika pamoja na mleta mada.
Kwajinsi nilivyo soma gazeti hilo, nimemuelewa mtaalam akisema kwamba.... mtambo huo ulio jengwa huko Lwamgasa, utakua umerahisisha kazi za uchenjuaji kifusi madini (processing plant).
Lakini mtaalamu huyo hakugusia kwamba mambo huo utahusika na kuchenjua makinikia.
Wakuu, hapa naona hii mada imechanganya wachangiaji kutokana na aina ya uwasilishaji wa mada nzima.
 
Back
Top Bottom