Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
JESHI la Polisi nchini limetangaza zawadi ya Sh milioni 5 kwa atakayewezesha kukamatwa kwa watuhumiwa waliohusika na mauaji ya raia wa China, Zhang Hongfa (23), ambaye alikuwa mhandisi wa kampuni ya ujenzi wa miundombinu ya maji safi mkoani Pwani.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani, Absalom Mwakyoma, ametangaza zawadi leo alipozungumza waandishi wa habari ofisini kwake.
Kamanda Mwakyoma, amesema, fedha hizo zimetolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema, kama motisha na kivutio kwa watoa taarifa.
Alisema Oktoba 17 mwaka huu, saa 1.30 usiku Kwa Mathias, wilayani hapa, kundi la majambazi wapatao kumi, wakiwa na silaha za aina mbalimbali zikiwamo shotgun, MarkIV, mapanga na marungu, walivamia kambi ya ujenzi wa miundombinu ya majisafi wilayani hapa ya kampuni ya China Hunan and Constraction na kumuua Mhandisi Hongfa.
Uchunguzi wa daktari ulionesha kuwa mtu huyo alifariki dunia baada ya kutokwa na damu nyingi katika tukio hilo ambapo raia wengine watano wa China walijeruhiwa kwa mapanga.
Waliojeruhiwa ni Huii Quan (52), Liuo Guobo (24), Huxiao Jie (28), Wu Jiano au Ping (35) na Yong Chin Jiao (23) wote wahandisi wa maji kutoka China na walipelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
Kamanda Mwakyoma alisema kabla ya kuingia kwenye kambi hiyo majambazi hao walifyatua risasi nne angani kwa lengo la kuwatisha watu waliokuwa jirani na eneo hilo, wasisogee kwenye tukio ili waweze kupora kirahisi.
Baada ya kufyatua risasi hizo, majambazi hao waliwaweka chini ya ulinzi watumishi wote waliokuwa kwenye kambi hiyo na kupora silaha ya mlinzi wa zamu katika kibanda cha ulinzi huku askari akiwa ameiacha bila taarifa zozote.
Siku hiyo kulikuwa na walinzi watatu wa kampuni ya ulinzi ya Muungano ya Maili moja, mmoja kati yao akiwa na silaha aina ya shotgun na risasi tatu za mlinzi.
Alisema makachero wa Polisi wanawahoji walinzi wote watatu kuhusiana na tukio hilo huku likiwatafuta majambazi waliohusika.
Walinzi wanaohojiwa ni Abdallah Katema (34) ambaye alikuwa na silaha ya zamu siku ya tukio, Abdallah Moyo (45) na Asha Musa (32) wote wa Muungano.
Katika tukio lingine juzi saa 6.30 mchana kwenye barabara ya Mkuranga-Kisiju mkoani Pwani gari namba T 541 AWL aina ya Toyota Corola ikiendeshwa na mtu aliyejulikana kwa jina moja la Charles liliacha njia na kugonga mti na kuwaka moto.
Dereva na abiria, William Matola, walikufa papo hapo na abiria mwingine kujeruhiwa. Aliyejeruhiwa ni Martin Samwel (30), mkazi wa Kawe, Dar es Salaam.
Maiti wamehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam wakisubiri ndugu kuwatambua na majeruhi alipelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3942
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani, Absalom Mwakyoma, ametangaza zawadi leo alipozungumza waandishi wa habari ofisini kwake.
Kamanda Mwakyoma, amesema, fedha hizo zimetolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema, kama motisha na kivutio kwa watoa taarifa.
Alisema Oktoba 17 mwaka huu, saa 1.30 usiku Kwa Mathias, wilayani hapa, kundi la majambazi wapatao kumi, wakiwa na silaha za aina mbalimbali zikiwamo shotgun, MarkIV, mapanga na marungu, walivamia kambi ya ujenzi wa miundombinu ya majisafi wilayani hapa ya kampuni ya China Hunan and Constraction na kumuua Mhandisi Hongfa.
Uchunguzi wa daktari ulionesha kuwa mtu huyo alifariki dunia baada ya kutokwa na damu nyingi katika tukio hilo ambapo raia wengine watano wa China walijeruhiwa kwa mapanga.
Waliojeruhiwa ni Huii Quan (52), Liuo Guobo (24), Huxiao Jie (28), Wu Jiano au Ping (35) na Yong Chin Jiao (23) wote wahandisi wa maji kutoka China na walipelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
Kamanda Mwakyoma alisema kabla ya kuingia kwenye kambi hiyo majambazi hao walifyatua risasi nne angani kwa lengo la kuwatisha watu waliokuwa jirani na eneo hilo, wasisogee kwenye tukio ili waweze kupora kirahisi.
Baada ya kufyatua risasi hizo, majambazi hao waliwaweka chini ya ulinzi watumishi wote waliokuwa kwenye kambi hiyo na kupora silaha ya mlinzi wa zamu katika kibanda cha ulinzi huku askari akiwa ameiacha bila taarifa zozote.
Siku hiyo kulikuwa na walinzi watatu wa kampuni ya ulinzi ya Muungano ya Maili moja, mmoja kati yao akiwa na silaha aina ya shotgun na risasi tatu za mlinzi.
Alisema makachero wa Polisi wanawahoji walinzi wote watatu kuhusiana na tukio hilo huku likiwatafuta majambazi waliohusika.
Walinzi wanaohojiwa ni Abdallah Katema (34) ambaye alikuwa na silaha ya zamu siku ya tukio, Abdallah Moyo (45) na Asha Musa (32) wote wa Muungano.
Katika tukio lingine juzi saa 6.30 mchana kwenye barabara ya Mkuranga-Kisiju mkoani Pwani gari namba T 541 AWL aina ya Toyota Corola ikiendeshwa na mtu aliyejulikana kwa jina moja la Charles liliacha njia na kugonga mti na kuwaka moto.
Dereva na abiria, William Matola, walikufa papo hapo na abiria mwingine kujeruhiwa. Aliyejeruhiwa ni Martin Samwel (30), mkazi wa Kawe, Dar es Salaam.
Maiti wamehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam wakisubiri ndugu kuwatambua na majeruhi alipelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3942