Mtafuteni Mungu siyo miujiza!

Mkungunero

JF-Expert Member
Aug 13, 2023
408
568
MTAFUTENI MUNGU SIO MIUJIZA;
Maombi ya Asubuhi 🔥
Zaburi 98

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.
2 Bwana ameufunua wokovu wake, Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.

Sisi wana wa Dunia tukumbuke maneno aliyosema Bikira Maria, Alipowatokea watoto wa Fatima Lucia Fransis na Yasinta, Alisema Tusali, Tusali Rozari Tupate Amani na Wasiyo Mwamini YESU Mwokozi Wamuamini ili wa Okokee. . .

Ahsante MUNGU Mwenyezi kutulinda na kutupa Kibali Kuiona Leo, Ahsante kwa Huruma yako na Wema wako. . .

Utusamehe makosa yetu ya kila siku, Ufalme Wako Utufikie duniani kama mbinguni, Utupe Mkate wetu wa leo Tusitende dhambi tena kwa Huruma yako. . .

Kwa Huruma yako Utulinde katika hatari zote za Roho na mwili, Utupe Hitaji la mioyo yetu na Matamanio yetu, Utujalie kuyafikia Malengo yetu. . .

Kwa Maombezi ya Mama Bikira Maria, Ee Bwana Utujalie Kuja kwako kwa Ajili ya Upendo Tulio nao kwako na sio kwa kutanguliza Mahitaji yetu. . .

Kwa Maombezi ya Mama Bikira Maria, Tunaomba kwa ajili ya Wagonjwa na wote wanaoteseka kwa namna moja au nyingine iwe kwa maradhi ya kusababishiwa ama laa, Mwenyezi MUNGU awafanyie wepesi wapate Kupona. . .
Tunaomba na kushukuru Amina 🙏
 
Siku hizi watu wanatafuta miujiza tu Mkuu, Habari za Mbinguni hawana shida nazo hata Wachungaji wenyewe wanadai maisha ni hapa hapa duniani ndio maana wanazisaka sadaka kwa kila hila.
 
Mungu wa mbinguni akubariki sana,

Kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,
Tumsifu Yesu Kristo.....
 
Mungu huyo anatafutwa kwani amepotea?

Yani Mungu muweza wa vyote anatafutwa tena?

Kwamba amejificha?

Mungu huyo ana chekesha sana.
 
Back
Top Bottom