Mtaani kwetu hakuna kabisa stori za Lissu

Mtaani kwetu hakuna kabisa stori za Lissu

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
23,717
Reaction score
57,243
Toka wiki iliyopita nikiingia JamiiForums nakutana na nyuzi nyingi kuhusu Lissu na ziara zake nchi za Magharibi.

Juzi nikasema nifanye utafiti; je, wananchi wa kawaida mitaani ambao sio member wa JF wana habari zozote zinazoendelea?

Nikapita katika vijiwe vyangu (mitaa ya Ubungo na Tabata) kiukweli kabisa sijabahatika kusikia watu wakizungumza hizi habari. Sanasana utakuta wanajadili mipira, kubet n.k.

Nikaenda kwa mafundi masofa, gereji, madukani nikawa nawasimulia zile interview za Lissu yaani huwezi amini hawajui lolote linaloendelea wakabaki wananisikia mimi.

Toka juzi natembelea vijiwe vya watu wengi nakuta stori kubwa ni mpira na watu wengi wanajadili namna ya kuanza ratiba za kufanya mazoezi ili kujiweka vizuri kiafya.

Sasa kama huku mijini watu wa kawaida hawana habari za Lissu je huko vijijini kabisa? Kwahiyo Lissu na ziara zake hazina madhara yoyote kwenye siasa za nchi yetu.

Hizi habari zinaishia Jamiiforums pekee wakati jamii kubwa ya watanzania hawapo JF.
 
Shamba uko limeni tu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Sasa kama huo mtaa hadi weye unaishi?Si mtakuwa wachuma mboga wote hapo mtaani?Hahahahaaa
 
Mtaani watu wanaogopa kupiga stori za kukosoa serikali , lakini ukimwita mtu pembeni ukamdadisi vizuri anakwambia hii serikali ni ya kishetani haijapata kutokea. Endeleeni kujifariji lakini mkae mkijua upepo wa Lissu utaibadili serikali kuwa ya watu.
 
Watu wako bize na maisha who on earth is Lissu?
 
Kwaio unafanya shughuli yote hio ili upate nini?
 
Huo mtaa wenu una ile aina ya watu ambao hawajui dunia imetoka wapi, imefikia wapi, na inaenda wapi. Wako tu ili mradi wako. Kiujumla hawajui habari zinazotawala headlines duniani ni zipi. Wanaishi kwenye sayari yao wenyewe. Wananikumbusha mzee mmoja fundi cherehani kiziwi kwenya movie ya "The gods must be crazy". Huyu mzee magaidi wamevamia kijiwe chake na wanafanya uporaji huku wakiwa wamewalaza watu chini kwa mirindimo ya risasi lakini yeye anaendelea kushona tu na haelewi kinachoendelea pembeni yake. Ilifikia wakati yule gaidi alipiga risasi kwenye cherehani anayotumia na kuutoa uzi ule lakini jamaa hakuelewa, alidhani uzi umedondoka wenyewe hivyo akautafuta na kuendelea na kazi yake. Kiujumla ni kuwa tangu tukio linaanza mpaka linamalizika hakujua ni nini kimeendelea, ilikuwa ni yeye na cherehani yake tu. Hii ndio aina ya watu wa mtaani kwenu.
 
Sasa kama hao watu wala hawajadili ndege, SGR, stiegler gorge na flyover Bali wanajadili mpira huoni hao ni wale wanaojua bado Nyerere ni rais wa Tz? Hao tunawaburuza tu sisi watu wa jf. Tena ilibidi uwanunulie na mpira ili wajadili mpira wakiwa wanauona
 
Ubungo ipi hiyo na tabata ipi au ubungo kijiji kule ambako tigo pesa ipo moja?
 
Nasikia leo amealikwa chuo kikuu cha Maryland na wanafunzi tayari wamefurika ukumbini hadi imebidi milango ifungwe. Yericko Nyerere ndio kaleta hii habari ya mwaliko leo asubuhi.
 
Back
Top Bottom