Mtaalamu wa mifugo (Dr. by Veterinarian): Karibuni kwa ushauri, tiba na dawa za mifugo tu

You must be one of them!!
 
Tumekuomba ondoka kwenye jukwaa letu maana huna mchango wowote constructive kwetu ni fujo tu, tuachie mtaalamu wetu tuendelee kupata faida na kukuza mitaji yetu.
Mkuu, fanya kumpuuza.

Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwenye profile yake na kubonyeza kitufe cha IGNORE, hutoweza kuona upuuzi anaoandika.
 
Mkuu Os cordis,naomba kujua kama majan ya Lucerne yanafaa kutumika kama chakula cha nguruwe,na kama yanafaa yanamchango gan kwa fattening pigs?
Asante
Habari, kwa swali lako Majani ya Lucerne ndio hutumika kama moja wapo wa vichanganyo katika chakula cha nguruwe hasa kutengeneza chakula cha GROWERS na FINISHER.

Zifuatazo, ni sababu za kwanini lucerna hutumika kama moja wapo ya vichanganyo katika chakula cha Nguruwe.

(1) Majani hayo huwa na kiwango kikubwa cha protein ambacho ni kati ya 20-22% na katika chakula cha kukuzia nguruwe huitaji kiwango cha protein 18% na katika kumalizia au fattening huitaji kiwango cha protein 14%, kwa maana hivyo waweza ona ni kwa kiwango gani majani hayo yalivyo na umuhimu katika kujenga mwili wa nguruwe.

(2) Majani hayo yana kiwango kikubwa cha madini na vitamini na kama ikitokea yakavunywa mapema huwa na kiwango kizuri pia cha nishati na fibres. Ambazo ni muhimu sana katika ujenzi wa mwili wa nguruwe.

Zingatia; Kipimo cha lucerna katika mchanganyiko hutegemea na malighafi ulizonazo.
 
MSAADA
Habari wa ndugu naomba msaada nina ng'ombe wangu amezaa jana mwenyewe bila kusaidiwa kuvuta mtoto.
Leo nimerudi kazini nimemkuta amelala hawezi kuamka nimejaribu kila namna imeshindikana.

Naombeni msaada au hata ushauri.
 
MSAADA
Habari wa ndugu naomba msaada nina ng'ombe wangu amezaa jana mwenyewe bila kusaidiwa kuvuta mtoto.
Leo nimerudi kazini nimemkuta amelala hawezi kuamka nimejaribu kila namna imeshindikana.

Naombeni msaada au hata ushauri.
Unapatikana wapi? Shingo yake kaiweka vipi?
 
Dr ngombe wangu amezaa sasa miezi mitatu. Alipatwa na ECF nikamtibu akapona. Lkn anakonda kila siku. Nikampima wakasema ana anaplasmosis. Nikampiga OTC 30%, akapata nafuu. Baadaye akaanza kudhoofu. Nikapima wakasema bado anaplasmosis. Nikampiga hi tech akapata nafuu. Jana nampima wanasem bado ana anaplasmosis. Nifanyeje?.

Nyongeza: Kuna Dr alisema labda kala nylon, nikampa epsom salt .. magnisium sulphate??? akaharisha, wakasema salt inasaga nylon into pieces, then anainya. Mwingine aksema immunity imeshuka na hivyo anaplasmosis ina surface.... na ni ngumu kutibu. which is which?
 
Habari Mkuu, pole kwa kuuguliwa na mfugo wako ningependa kujua ulitumia njia gani kupima na kujua huyo ng'ombe yuko na Anaplasmosis ( Ndigana baridi) na Ulihakikisha vipi kuwa ng'ombe wako alipona ECF ( ndigana kali) na pia inaweza kuwa babesios.

Najua watu wengi huwa wanachanganya hayo magonjwa wakati wa kufanya diagnosis unaweza kuta unatibu anaplasmosis kumbe mfugo wako ana ECF..

Ndio maana dalili ni muhimu sana wakati wa kufanya diagnosis na dalili ukiwa expect mzuri unaweza kuwa correct kwa 60 % ila vipimo vya maabara ni 100%

Hivyo basi kama uko na uhakika ni anaplsmosis kweli jaribu kubadili dawa na tumia dawa hizo hapo chini;

 
ngependa kujua ulitumia njia gani kupima na kujua huyo ng'ombe yuko na Anaplasmosis ( Ndigana baridi) na Ulihakikisha vipi kuwa ng'ombe wako alipona ECF ( ndigana kali) na pia inaweza kuwa babesios.
Kuna mtaalamu wa maabara ndiye alitibu. Huyu baba ni mtaalamu alikuwa nafanya kazi ya utafiti kwenye maabara kuu ya Mko ilipokuwa inakuwa funded na Germany/ Uholanzi. Anaaminiwa sana katika microscopy.

Ng'ombe anakula, anacheua vizuri maziwa yamedrop kidogo toka lita 6 mpaka 4/4.5 kitu kama hicho.
 
Fanya kumpa hiyo choice ya 3 katika hiyo picha niliokupa hapo juu..

Na imani ata recover vizuri..
 
Nahitaji huduma ya ku- spay paka wangu. alikuwa mmoja mara kakaja kengine kutoka porini nikashindwa kukatupa. nitapataje hiyo huduma
 
Nahitaji huduma ya ku- spay paka wangu. alikuwa mmoja mara kakaja kengine kutoka porini nikashindwa kukatupa. nitapataje hiyo huduma
Unapatikana wapi mkuu? Huduma ipo hiyo tutafanye kubadilishana mawazo then tupange siku ya kuja kumfanyia Ovariohysterectomy (OH) paka wako.

Ahsante.
 
as
asante Dr. sasa nitumie dawa gani kati ya hizo for better results?
 
asante sana, ubarikiwe. Dosage tafadhali nisaidie
Dosage kuna hizo mbili hapo 3mg/kg kama lowest dose na 5mg/kg kama highest dosage...

So, nakushauri nenda kwa highest dose kupata volume for injection chukua uzito wa ng'ombe husika in (kg) zidisha na dosage ambayo ni 5mg/kg then gawanya na concentration ambayo ni 120mg/ml kupata injection volume mkuu...

Hope umenielewa hapo maana una akili kubwa
mpe sindano ya kwanza leo then sindano ya pili irudiwe baada ya wiki mbili kumbuka kuchoma kwenye nyama ya shingo au kwenye rump area juu karibu na eneo la mkia kule utaingia mtandaoni kuona site hiyo mkuu..

Goodluck
 
asante sana tena. Nashukuru sana tena.
Hapana sina akili kubwa, ila I can precisely follow instructions as given. nimefanya kazi for 30 yrs as a research scientist with speciality in Immunology//microbiology in one of our research Institutions.
Ubarikiwe tena.
 
Tupo pamoja mkuu pale utakapoona kuna shida mahali, na unahitaji msaada zaidi kuwa huru kuuliza.

Nitakupa all necessary information required as per asked.
 
Tupo pamoja mkuu pale utakapoona kuna shida mahali, na unahitaji msaada zaidi kuwa huru kuuliza.

Nitakupa all necessary information required as per asked.
asante sana. Looks this dawa is very expensive. How much does it cost in dar? Naweza kumchoma leo dose moja, then ingine nikatafuta ya bei nafuu Dar. I am in Tanga
300 x 5= 1500/120= 12.5 mls needed. Each meal is 2500 Tsh! .....12.5 x 2500= 31,250 Tsh. Vial nzima ya 50 mls is 75,000 Tsh
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…