samilakadunda
JF-Expert Member
- Oct 13, 2011
- 1,780
- 360
Hata mm sina imani na UKAWA!Muundo wa serikali 3 haijathibitika kama tukipata ndiyo tutaondokana na umaskini huu wa kutisha!
UKAWA wanapoteza nafasi adimu ya kuwapa watz katiba yenye mustakabali wao!Rasimu ya Warioba ina vipengele vingi muhimu vitakavyo badilisha maisha ya Watz zaidi ya serikali tatu wanayotaka tuamini ndiyo tiba ya maisha hoe hae ya Mtz!!
Vipengele muhimu ktk rasimu ya Warioba ni:
(1)Tume huru ya uchaguzi
(2)Bunge tu liwe na uwezo wa kupeleka nchi vitani
(3)Majaji wateuliwe na Rais waidhinishwe na Bunge na Rais asiweze tena kuwafukuza
(4) Kufutwa kwa viti maalum vya Ubunge
(5)Pesa za serikali zidhibitiwe na Bunge sio kama sasa Gavana anaipa serikali pesa yyt wakiomba!Madai tajwa hapo juu yana umuhimu mno kurekebishwa now zaidi hata ya muundo wa serikali yetu uweje!
UKAWA eleweni kuwa katiba ni compromise sio kila kitu mnachotaka mtapewa na sio kila kitu CCM wanachopewa watapata!Wapeni CCM serikali 2 na wao wawapeni madai hayo 5 juu mtakuwa na nafasi nzuri ya kuiondoa CCM mwakani!
Bila Tume huru hamuiondoi CCM kwenye sanduku la kura hata iweje!
CC MwanaDiwani Lizabon ifweero Simiyu Yetu
acha porojo wewe, ikiwa TUNU TU ZA TAIFA MMEZI FUTA ZILIZO CHUNGU KWENU, JEE? VIPENGELE VINGINE JE?
Last edited by a moderator: