Msilolijua kuhusu Wilson Kabwe

Mimi nilisema hizi habari za summary execution ni kuficha mengi.
 
Hapo nimejifunza kitu kimoja tu kwamba kumbe eneo la Kabwe pale Mbeya ni legacy ya huyu Wilson Kabwe, basi.
 
Hapo nimejifunza kitu kimoja tu kwamba kumbe eneo la Kabwe pale Mbeya ni legacy ya huyu Wilson Kabwe, basi.
Acha kupotosha watu wewe! Jina la kabwe lilikuwepo kabla hata hamjamleta huyo fisadi wenu awe mkurugenzi pale
 
Hyo Kabwe ya Mbeya unayosema ilikuwepo kabla hata ya huyo Wilson kuwa Mkurugenz wakati huo sugu anasoma pale Sangu hyo Kabwe iko tu usitudanganye bana
Yah!!! Ni kweli panaitwa hivyo tangu Nyerere na Mwinyi
 
Acha kupotosha watu wewe! Jina la kabwe lilikuwepo kabla hata hamjamleta huyo fisadi wenu awe mkurugenzi pale
Mkuu mbona povu linakumiminika? Angalia post No. 1 ndio react hapo usinitemee vumbi la mate.
 
Hyo Kabwe ya Mbeya unayosema ilikuwepo kabla hata ya huyo Wilson kuwa Mkurugenz wakati huo sugu anasoma pale Sangu hyo Kabwe iko tu usitudanganye bana

Wakati mwenzio anaongelea jengo wawe anaongelea kituo cha daladala
 
viwanda vya kutengeneza uongo vimeshaanza kazi yake
 
Mwaka 1997 nimekanyaga Mbeya kwa mara ya kwanza nilikuta eneo linaloitwa Kabwe.
Wakati huo Kabwe alikuwa Mkurugenzi wa Mbeya?
Eneo hilo lipo toka mimi napata akili zangu, labda inawezekana kabwe kadumu zaidi ya miongo minne madarakani. Wenye kujua historia vizuri njooni mtuweke sawa.
 
UKWELI HUU UNAJULIKANA. NA MJUE ILE HALI ILIYOTOKEA PALE JANA NI HESABU TU YA NJISI YA KUMSHUGHULIKIA JAMAA KWANI ILIKUWA NGUMU KUDEAL NAYE.MAGHUFULI MJANJA ILA WATZ TUNAKIMBILIA KULALAMA BILA KUFIKILIA KWANINI MH RAIS KAFANYA HIVI AU VILE

Mkuu ulichokiona hata mimi nilikiona. Katika hali ya kawaida Mh. asingefanya vile. Alifanya hivyoakijua kabisa kuwa bila kufanya hivyo atapigiwa simu na walioko nyuma ya Kabwe ku-nutralize mambo. Hiyo aliyotumia Mh. ni tactic nzuri sana kwa watu wanaofuja mali kwa kiburi cha kuwa na vigogo nyuma yao.
 
You have generalized it too much! Be specific with facts. Cjui mara kaharibu! Kaharibu kwa kufanya nn?
Yadaiwa kila anakohamishiwa kikazi huzua fujo


Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe

Bunge limetangaza 'kumshughulikia' Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe, ang'olewe kwa madai kuwa ni kiongozi mbovu na tatizo.

Kwa kuanzia, wabunge wamemshtakia' kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakidai amekuwa akizua fujo kila anakohamishiwa kikazi, huku akiendelea kulindwa na baadhi ya vigogo serikalini.

Hatua hiyo ilitangazwa na Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, wakati akijibu mwongozo wa Spika ulioombwa na Mbunge wa Rombo (CHADEMA), Joseph Selasini, bungeni jana.

Mwongozo huo uliombwa kufuatia kauli ya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli bungeni jana kwamba Kampuni ya Tanzania Building Works Limited inachunguzwa kwa kushindwa kutekeleza ujenzi wa soko la Mwanjelwa, mkoani Mbeya kwa wakati kinyume cha mkataba, uliofikiwa kati yake na Halmashauri ya Jiji la Mbeya na hivyo, kunyang'anywa kazi hiyo.

Katika ombi lake, Selasini alihoji iwapo kampuni hiyo itachunguzwa, kwanini isichunguzwe sambamba na Kabwe kwa madai kwamba mkurugenzi huyo ameonyesha kila anapohama, huhama nayo na kuipatia kazi kwenye maeneo ambayo anapewa.

Akijibu, Zungu ambaye pia ni Mbunge wa Ilala Jiji la Dar es Salaam, alisema yeye akiwa ni sehemu ya watu wenye maslahi na suala linalosemwa na Selasini atailaumu serikali.

"Serikali bado mnazembea viongozi wabovu, mnawahamisha kutoka sehemu moja kuwapeleka sehemu nyingine. Huyu mtu (Kabwe) ni tatizo kubwa sana. Na siyo tatizo Dar es Salaam, amefanya tatizo Mwanza. Chama Cha Mapinduzi kimekosa uongozi Mwanza sababu ya huyu mkurugenzi," alisema Zungu.

Aliongeza: "Huko Mbeya amefanya fujo, sasa mnamleta Dar es Salaam anafanya fujo, na Dar es Salaam siyo fujo. Tumetangaza na tumetoa taarifa serikalini mipaka ya halmashauri imechukuliwa, Tamisemi wamekaa kimya, mkuu wa mkoa amekaa kimya."

"Mimi naiagiza serikali na leo hoja hii ya huyu mkurugenzi tunakwenda nayo kwa waziri mkuu."
Awali, Selasini akiomba mwongozo huo, alisema Kabwe akiwa mkurugenzi wa jiji la Mbeya ndiye aliyeipa kampuni hiyo kazi hiyo.

Hata hivyo, alisema Kabwe aliondoka Mbeya baada ya kelele za madiwani na wananchi na kuliachia jiji hilo hasara kubwa.

"Kabwe huyo huyo alipelekwa Mwanza na pale Mwanza ameacha hasara kubwa sana. NSSF pamoja na viwanja, ambavyo aliuza na fedha hazikujulikana zilikokwenda. Lakini amehama na kampuni hii," alisema Selasini.

Aliongeza: "Kabwe huyu huyu aliondoka Mwanza baada ya kelele kubwa za wananchi pamoja na madiwani. Mheshimiwa mwenyekiti, sasa Wilson Kabwe yuko pale Dar es Salaam, Mkurugenzi wa jiji la Dar es Salaam."

Alisema akiwa Dar es Salaam, nako pia ameanzisha mtafaruku mkubwa akipora vitega uchumi vya manispaa akizifanya kuwa za jiji.

Selasini alisema Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeshatoa maelezo na mapendekezo mengi kwa serikali kuhusu Kabwe, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.

"Mheshimiwa mwenyekiti, picha inayotolewa ni kwamba, inawezekana Wilson Kabwe mkurugenzi anao wakubwa wanaomlinda huko Tamisemi," alisema Selasini.

Aliongeza: "Sasa mheshimiwa mwenyekiti, naomba mwongozo wako, kama hii kampuni ya Tanzania Building Works itachunguzwa, kwanini isichunguzwe sambamba na Wilson Kabwe ambaye ameonyesha kwamba kila anapohama, anahama nayo na kuipatia kazi kwenye maeneo, ambayo anapewa?"

CHANZO: NIPASHE
 
Hyo Kabwe ya Mbeya unayosema ilikuwepo kabla hata ya huyo Wilson kuwa Mkurugenz wakati huo sugu anasoma pale Sangu hyo Kabwe iko tu usitudanganye bana
Nami nilitaka kumwambia the same.
 
Akiwa mkurugenzi wa jiji la Mwanza alipiga dili nyingi ambazo vijana wa njini wanasema 'za usoni kabisa' akawa analelewa tu.. Kupitia dili hizo alijenga vitega uchumi kadhaa ikiwemo Hoteli ya kifahari ya "Royal Sunset Beach" kule Luchelele!

na huko ndiko (inadaiwa) alipeleka pampu za kusukuma maji za gari mojawapo la zimamoto la halmashauri ya jiji la Mwanza ili zitumike kusukuma maji hotelini/kwenye mabwawa ya samaki hotelini hapo kutoka ziwani.
 
na huko ndiko (inadaiwa) alipeleka pampu za kusukuma maji za gari mojawapo la zimamoto la halmashauri ya jiji la Mwanza ili zitumike kusukuma maji hotelini/kwenye mabwawa ya samaki hotelini hapo kutoka ziwani.

Tutajua mengi!
 
Kwa muda mfupi niliomfahamu Wilson Kabwe, amewasikitisha sana watu wa Mwanza, miongoni mwa mengi aliyoharibu ni kwamba, amepiga dili katika uuzaji na Ujenzi wa Klinic Makongoro mwanza, ambayo Ujenzi wa clinic tunaambiwa ni zaidi ya billion 2 zimetumika wakati hospital haina hadhi hiyo, lkn pia ameacha vilio vingi ktk ugawaji wa viwanja Luchelele, watu walijiuliza kiburi hiki jamaa anakitoa wapi chakutafuna hela za watanzania bila aibu. Tunauomba uchunguzi usiyaache haya tafadhali.
 
kuna kipindi JK alikuwa mwanza sijui akizindua daraja flani hivi akasema kuwa anajua mwanza kuna MCHWA wa kutafuna fedha sasa sijui mr. dhaifu alichukulia poa tu
 
We chizi nini...mbona hueleweki ulichokiandika.
 
Kwa ajili yakuwatendea haki wanamwanza na watanzania wahanga kwa uongozi wa huyu Wilson Kabwe tunawaomba wahusika wamfungulie mashtaka huyu jamaa, nihatari sana kwa ustawi wa Tanzania yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…