Msifurahie CHADEMA kupotea

Msifurahie CHADEMA kupotea

Hivi hawa wachoma mageti waliishia wapi?
images (17).jpg
 
Mimi tangu Chadema waliponiambia Katibu Mkuu wao Dkt Slaa kanunuliwa naamini kila Mtu ndani ya Chadema anaweza kunuliwa!

Hata Mbowe mkimuweka mbali na Fuko la Ruzuku la Chama anaweza kurudi CCM
Chama chenyewe kilishauzwa kwa tajiri mfugaji kutoka ccm ndo iwe viongozi na wanachama wake wasiuzike?
 
Tokea lini suti za mtumba zikauzwa laki sita? mwenyekiti ni bingwa wa kuwahadaa watanzania.
Huyu Mwenyekti Siku akiondolewa kwenye Cheo cha kumiliki Fuko la Ruzuku Chadema ndani ya Miezi miwili anarudi CCM kuunga Mkono jitihada za Rais
 
Huyu Mwenyekti Siku akiondolewa kwenye Cheo cha kumiliki Fuko la Ruzuku Chadema ndani ya Miezi miwili anarudi CCM kuunga Mkono jitihada za Rais
Hahaa..anyway kachama kenyewe kanajifia nayeye hajali, hashauriki hana hata huruma.uchaguzi ujao atabaki yeye na mkewe..
 
Ubakataza siasa kwa wengine halafu wewe unafanya.
Huku unapiga risasi vyama vingine,unatangaza uchaguzi halafu unazuia mawakala wa vyama vingine kuwepo ktk uchaguzi.

CHADEMA haitapotea hata iweje,hata wazimbabwe walikaa kimya lakini si uliona machozi ya furaha waliyotoa baada ya kuondoka ki babu.
Hata ccm itatoka believe me.
 
Chadema haiwezi kufa kwani hadi sasa nikiongozi gani wa chadema aliyekwenda ccm? Ni mmoja patrobas lkn uongozi wote uko intact sasa kitakufaje?. Ngoja matawi yadondoke wakati wa kiangazi ili mti uchanue vizuri 2020
 
Chadema haiwezi kufa kwani hadi sasa nikiongozi gani wa chadema aliyekwenda ccm? Ni mmoja patrobas lkn uongozi wote uko intact sasa kitakufaje?. Ngoja matawi yadondoke wakati wa kiangazi ili mti uchanue vizuri 2020
Good point!
 
Chama gani ukabila na roho mbaya imewajaa mpak kwnye ruzuku ??? Bora ifilie mbali tuepukane na mipasho...
Wanamaa sisi ni Nomaaa..hata nyerere alihanyaaa....ww piga domo tuuu lkn ukienda klmanjaro watu wanaish km Ulayaa...
 
Mimi tangu Chadema waliponiambia Katibu Mkuu wao Dkt Slaa kanunuliwa naamini kila Mtu ndani ya Chadema anaweza kunuliwa!

Hata Mbowe mkimuweka mbali na Fuko la Ruzuku la Chama anaweza kurudi CCM
Muwekeni sasa mbali na fuko LA ruzuku mumnunue.
 
Vyama vya upinzani vitakapokufa vyote kabisa, ndipo watanzania watajua umuhimu wa kuwa na vyama vya upinzani vyenye nguvu.
 
Kama CCM tu inawanunua itakavyo tukiwapa Nchi si mtanunuliwa na Wazungu? Maana mnapenda kununuliwa
Kwahiyo ukata huu babu yako kakwambia usijiongeze,watu wameiona fursa ya milioni 30 hadi zaidi wewe unataka kufa njaa,ngoja mje kubanana hukohuko mtanyooka.
 
Vyama vya upinzani vitakapokufa vyote kabisa, ndipo watanzania watajua umuhimu wa kuwa na vyama vya upinzani vyenye nguvu.
Hakuna kitu kibaya kama njaa,njaa hubadili watu msimamo,watu wameona fursa ya kuteuana kila jumatatu wewe unafikiri nani asiyependa mwanae akasome Marekani,wacha vife tutaanza upya ila hata ccm kwenyewe ni njaa na mateso,wacha tuisome namba ndo akili zitarudi haraka,Mbona mtu mwenyewe anawawinda wapinzani kama kuku na wengine wako hoi vitandani anasema waxi kabisa hamkinichagua lazima niwabomolee then watu wanaona anafaa,this is more than a threat
 
Chadema ngoja ife, hapa CCM mbele kwa mbele
Tuwe wakweli, hivi hata kama serikali iliyopo inafamya vizuri, unafikiri kweli ni vema upinzazi ufe ili mfumo wa chama kimoja urudi?. Vyama vya upinzani mi muhimu duniani kote, kazi yake ni kuleta changamoto kwa chama tawala
 
Ila wapinzani nao kwa kweli wanastahili kukimbiwa mana kwa hakika hawana mizizi.

Ni vyama vinavyoendeshwa kama BIKO .
Leo ipo kesho wameiondoa kwenye mtandao.

Hivi Mbowe haoni tatizo litakalotokana na kukosekana kwa ofisi za chama kuanzia Taifa mpaka kwenye mashina au mitaa?

Kukosa ofisi ni sawa na kijana aliyeoa na kuishi maisha yake yote bila kuwa na sehemu ya kuishi au kujenga nyumba.
Siku akikorofishana na mke wake familia inasambaratika mana watoto wengine wataenda kuishi kwa bibi mzaa baba wengine bibi mzaa mama na wengine kwa wajomba n.k.

Ofisi zinazojengwa na chama ni mali hivyo zinawafanya wanachama kuwa wavumilivu na kulinda mali zao.
Chama kikiwa na mali zake hakuna mtu anayewaza kukiacha chama na nguvu zake zikapotea bure.

Hii tabia ya Mbowe kuendelea kukikopesha chama mpka vitu vidogo vidogo ambavyo wanachama wangehamasishwa wangechangia ni hulka mbaya kabisa ya kukiona chama kama mali yake binafsi na hapo ndipo patakapoleta taswira ya VICOBA badala ya chama kinachotazamiwa kushika dola.

Hiyo mipango mingi wanayojifanya hao wapinzani kuiandaa na kuikosoa serikali kwenye bajeti ya kila mwaka kwa nini hatuioni wakiipanga kwenye chama chao tukaona kinaibuka ghafla na kuipiku CCM kimiradi na kimapata yanayotokana na ubunifu wa miradi mingi yenye kujenga chama na kutoa hata ajira kwa vijana ili wasiwe na mawazo ya kukimbia kimbia?

Tatizo ni moja hawaaminiani!

Ndio maana kila mtu anayeingia upinzani hasa Chadema anatoka haraka mana anaona kama ametemgwa na hakuna mikakati zaidi ya matamko!

Jipangene ,tafuteni watu makini wenye maono mapana msijione kuwa mko sawa. Kubalini mawazo mapya na pia kukosolewa.
Mnalaumu serikali ya awamu ya Tano kuwa haishauriki lakini nanyi pia mna tabia hiyo hiyo. Mkishauriwa mnatoa lugha chafu na za kejeli. Ni udikteta nao huo.

Nakumbuka Mh. Rais alimshauri Mbowe kuwa chadema kijenge Ofisi yake Dodoma kwa kuwa makao makuu yatahamia huko mapema.
Mpaka leo hawana ofisi huko wakati ile ilikua ni fursa kubwa ya kujitangaza kisiasa.
Siasa ni maendeleo sio porojo majukwani tu. Kila jambo linalogusa jamii likitumika vizuri ni siasa na linaweza kujenga chama.
Hivi Kweli Mtu alikua Waziri anahamia chama ambacho hakina hata Ofisi.
Ofisi ya kanda inakua kama Frem ya duka la Mangi halafu kweli mtu huyo akiitwa tena CCM kwa ahadi ya kupata maslahi na mazingira mazuri ya kisiasa asiruti? Thubuutu sio kwa nchi hii ambayao CCM ina makada mpaka kule kwenye walinzi wakubwa kabisa wa madola.
 
Back
Top Bottom