Msifurahie CHADEMA kupotea

Msifurahie CHADEMA kupotea

Kununuliwa si lazima kutolewe pesa. Hata ahadi ya kugombea tena ama "kutatuliwa" shida zao nako pia ni kununuliwa!!
Chadema wasipo msima misha Nyarandu kugombea jimboni kwake Singida, ndipo nitaamini wao hawanunui
 
Kama NCCR Mageuzi ilipotea......Chadema ni kitu gani bila Sera na hoja madhubuti kwa Watanzania!? Kila kukicha mnatengeneza matukio ya kuchafua hali ya hewa. Watanzania sio wapumbavu kama mnavyofikiri.
cc: mrangi
 
Hivi tunadhubutu kulaumu wapibzani kwa jinsi serikali inavyoumiza watu. Inakuwaje kama taifa hatukasiriki?
 
AnywY chadema hakifi. Sasa hivimumeingia hai kuwanunua. Aibu sana wamachame kununuliwa. Ila ni aibu zaidi kwa ccm.
 
Vyeo vya serikali vinatolewa kwa waovu na sisi yunashangilia. Huo ni udumavu wa akili. Wake up!
 
CCM Imshindwa kwenye ujenzi wa viwanda sasa wamegeukia kwenye ujenzi wa chama, na huu ni ushindi mkubwa sana kwa CDM.
 
Kama CCM tu inawanunua itakavyo tukiwapa Nchi si mtanunuliwa na Wazungu? Maana mnapenda kununuliwa
[HASHTAG]#lissumsaliti[/HASHTAG] alishanunuliwa na acacia tayari ndo maana akawa mtetezi namabari one wa wezi wa madini.
 
Mkuu, siyo kwamba tunafurahia chadema kufa, tunasikitika; lakini Inabidi tukubaliane na hali halisi tu. Chadema itakufa kwa kuijua yenyewe kwa sababu imeshindwa kujitoa kwenye kipindi cha kuwa chama cha kiharakati kwenda kwenye chama cha kitaasisi kilicho tayari kuaminiwa na wananchi na kupewa dhama na ya kongoza nchi.
Sisi tulio nje ya chama tukiwaambia wajiangalie maana chama kimepoteza mweleleo tunaishia kubezwa, kutukanwa na kudharauliwa. Inabidi kife tu maana hakuna namna.
 
Msipende kujitoa ufahamu,Hivi sasa chadema kila kukicha ni vitisho,vipigo na kesi zisizo na kichwa wala miguu.Hivyo basi muoga na mnafiki hawezi kubaki chadema,maana upande wa pili hatafunguliwa kesi za ajabuajabu bali atapata pesa haramu.Kama itatokea chadema kufa basi si kwasababu ya siasa safi ya upande wa pili,bali ni minguvu ya upande wa pili wakishirikiana na wadau wao.Ila ni dhahiri chadema haiwezi kufa,isipokuwa itaimarika zaidi kuliko wakati wote,na ccm itaingia mgawanyiko wa ajabu na vipigo vya wenyewe kwa wenyewe.
 
kwani wanaondoka kwa hiari zao au ni umalaya wa Akili jitu zima linatongozwa kama demu yani wa tz hamna kitu unafiki tu
 
Chadema will never die.Kuna external force kubwa inatumika kukihujumu kwa kuwa huko nyuma ilitumika nguvu kutoka kwa dola na CCM ikaonekana kushindwa.Sasa JPM ameingia kwa kila namna kuimaliza Chadema.

Hizi ni propaganda tu,kwa nini madiwani na viongozi wengi wanahama ama kununuliwa ni wa kaskazini,jibu ni simple tu kutengeneza perception kwamba Chadema haipendwi ata kwenye ngome zake.

Chadema ije na mkakati mzuri wa kufanya siasa zake kwa miaka hii 10.
 
Kila anaehama wanakwambia kanunuliwa!
Majibu mepesi mepesi tu!
Na huo ndio ukweli hakuna mtu mwenye akili timamu kabisa asiye na njaa akahamia ccm , wooye wanao hamia ccm kwa sasa kuna mambo mawili kama sio matatu kwanza rushwa na hilo lipo bayana na ushahidi upo wawazi,pili tamaa ya kupata nafasi au vyeo na hasa baada ya kugundua hulka za mgawa vyeo, tatu unafiki na kujipendekeza kwa serikali nankutafuta huruma ya serikali , maana kuna watu wakiwa upinzan au baada ya kuhamia upinzani biashara zao zinafungwa na bidhaa zao zinapigwa marufuku na serikali kuuzwa hivyo wanaona bora warudi ili wapate mbeleko ( kuogopa visasi) nje na hapo tunadanganyana,
 
Ni Kweli kuwa Mh Magufuli kwa sasa anafanya mengi makuu na kujali kodi za wananchi ila tukumbuke kuwa Muda wake ukiisha tunaweza kumpata mtu mbovu kabisa. Bila vyama hivi vya Upinzani tutarudi kule kule kwenye makashfa makubwa.
Mbona mm siyaoni hayo makuu anayoyafanya huyu Magufuli?
[HASHTAG]#Itakuwa[/HASHTAG] ni Kujidanganya kabisa kama bado utaamini kuwa Chadema ya Sasa itaweza kudumu kwenye siasa kwa miaka mingine 2 ijayo. Yaani kufikia 2020 Chadema itakwa hoi bin taabani kama hali ya mambo itaendelea kiwa hii ninayoiona.
Chadema iko mioyoni mwa watu, chadema ni imani ya watu na chadema ni sehemu ya maisha ya watu kwa sasa. Ni makosa makubwa kuilinganisha chadema ya leo na NCCR ya wakati ule maana NCCR ilikuzwa na mtu, alipohama NCCR ikafa.
 
Watajua baada ya upinzani kufa na kubakia kuendeshwa jinsi watu wapendavyo ndipo watakugutuka hakuna wa kusemea tena ubaya wowote akiumizwa mwananchi kimya, haki ikiporwa kimya...

Ndipo.kilio na kusaga meno kitakapoanzia.. mwenye akili na aanze kujitafakari..
Chadema ni mpango wa Mungu hakita kufa kamwe.
 
Kama ni lazima baada ya kila muongo mmoja chama kimoja kikuu kife kwa nini kisife chama cha mapinduzi?
Je ni lazima kuwa kife CHADEMA?
Hivi unajua wakati huu unaandika ni kwamba CCM kishakufa? Ila kina pewa uhai na geshi la polish?

Usilinganishe kifo cha chadema na wakina NCCR,TLP wao walikufa vifo vya takwa la serikali,CHADEMA kifo chake ni kigumu sana,sababu uhai wa chadema umefungiwa kwenye MIOYO ya wananchi.
Ukitaka kukiucha chama cha CHADEMA,basi kiondoe kwenye mioyo ya watanzania.

Na kukuondoa kwenye mioyo ni lazima CCM ifanye wananchi wnacho taka,na sio vipigo vya polisi,kukatakata wasimamizi wa kura,kufilisi matajiri,kubomolea watu wa kimara na kuwaacha wa mwanza.

CHADEMA INA ROHO YA PAKA.
 
chadema chama la wezi na wabaishaji life tu.
 
Back
Top Bottom