Msifunge ndoa kwasababu 'mnapendana'

Msifunge ndoa kwasababu 'mnapendana'

Umeandika kwa busara sana....

Ingawa nakiri niliolewa sababu ya kupenda; uamuzi nilochukua ulikuwa very risky...

Lazima kuwe na cha ziada...kilikuwepo ingawa by then hakikuwa that important ila kwa sasa nafurahia chaguo langu.

Ukute umeoa dad mzuri wa muonekano ...lakini anakupeleka puta...utavumilia ila ikifika pale umeanza kumuona kama dada yako; atakukomaje???

Unatakiwa uwe na sababu zaidi ya tatu za kumkubali mtu awe mwenza wako wa maisha...ukiona unajiuliza jibu linakuja moja tu 'Mzuri' jua unakoelekea kubaya.

Hapa umesema ukweli mkubwa sana

Kuna watu wameoana huku sababu ikiwa ni kupendana tu

Lakini wanafanikiwa kuishi pamoja kwa kuwa kuna kitu zaidi kilikuwepo bila wao kujua

Hawa ndo wanaotengeneza hoja kwamba mbona wao walioana kwa kupendana na wanadumu

Ukweli ndoa ina mabo mengi sana mapenzi ni sehemu tu ya yanayotakiwa kuwepo ili muoane lakini kuoana kwa sababu mnapendana ni hatari sana
 
Huwezi kumpenda mtu with no reasons. Vigezo vyote unavyovipenda awe navyo mwenzi wako ndio vinapelekea upendo uzaliwe kati yenu. Upengo huo unakamilishwa na satisfaction ya tendo la ndoa. Ndio mapenzi yenyewe.

Wrong!

Kuna mapenzi
Kuna ngono
Kuna kupenda
Kuna maisha

Haya ni mambo tofauti sana inatakiwa ujifunze ili uweze kuyatofautisha

Unaweza kuwa na mapenzi na mtu lakini akawa sio mzuri kitandani[ngono]
Unaweza ukampenda mtu lakini usiwe na mapenzi nae
Unaweza ukawa na mapenzi na mtu lakini usimpende
Unaeza kuwa na mapenzi na mtu lakini akawa hajui lolote kuhusu maisha

Utakapoweza kuyatofautisha haya utajikuta unafnya maamuzi sahihi sana kwenye maisha yako!
 
Ukweli unabaki pale pale.. Hapa duniani hakuna mtaalamu wa ndoa.
Kuna wanaooana kwa mapenzi.. ndoa zinawashinda
Kuna wanaooana kwa mapenzi.. ndoa zinadumu
Kuna wanaooana bila mapenzi... ndoa zinawashinda
Kuna wanaooana bila mapenzi.. ndoa zinadumu
Kuna wanaoendana tabia kama mapacha.. ndoa zinawashinda
Kuna wasioendana kabisaaaaa.. ndoa zinadumu
Kuna wanaoishi kwa mazoea.. ndoa zinadumu
Kuna ambao hata hawajui kwanini walioana.. ndoa zinadumu!
Kuna wanaochunguzana miaka kumi.. ndoa zinawashinda
Kuna ambao hawaoani kabisa.. wanaishi tu.. miaka nenda rudi hawana tatizo.. wako happy
Kuna wanaokutana na kuoana ndani ya miezi miwili.. ndoa zinadumu.....nakadhalika.. nakadhalika.
AND VICE VERSA

Bottom line:
1. Kama unataka kuoa/olewa fanya hivyo pale utakapohamua. Kama hutaki/hujaamua ACHA.
2. Kama uko kwenye ndoa, live each day as it comes. Enjoy the moment
3. Kama ndoa yako ina amani, mshukuru Mungu wako.. usiseme ni kwasababu nilifanya hivi.. au nilifanya vile..
4. Ukioa/olewa ishi the best way unavyojua wewe. The end will justify the means
5. Mwisho, kumbuka ndoa ni ARTIFICIAL sio natural. Naturally, binadamu hauko wired kuishi na mtu mwingine for the rest of your life.

SHIKAMOO!
shikamoo tena!
dah!
uve just said it AAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAALL!
 
Wrong!

Kuna mapenzi
Kuna ngono
Kuna kupenda
Kuna maisha

Haya ni mambo tofauti sana inatakiwa ujifunze ili uweze kuyatofautisha

Unaweza kuwa na mapenzi na mtu lakini akawa sio mzuri kitandani[ngono]
Unaweza ukampenda mtu lakini usiwe na mapenzi nae
Unaweza ukawa na mapenzi na mtu lakini usimpende

Unaeza kuwa na mapenzi na mtu lakini akawa hajui lolote kuhusu maisha

Utakapoweza kuyatofautisha haya utajikuta unafnya maamuzi sahihi sana kwenye maisha yako!

mi nilishakubali kuwa kilaza wen it comes ni wewe
lakini saasa sio kilaza kihivyo bana,hebu nielewesha hapa kweny bold unamaanisha nini!
elewesha mimi katika akili zangu za darasa la 2B sio za chuo kikuu kama zako!lol!
 
Baada ya kusoma maoni ya watu nimebaki na swali...kwani ukimpenda mtu unakuwa umependa nini hasa?????????????

Unajua unaweza kumpenda mtu sababu ya tabia au muonekano au basi tu hata sababu huna.

Kumpenda mtu kwa muonekano mara nyingi ni kumtamani...lust...lakini ndio mwanzo wa mapenzi ya kweli au kuonjana tu.

Sidhani kama kuna mtu humu ata feel proud kujua mwenza wake alimtamani...kila mtu angependa kujua kuwa kuna cha ziada kilichofanya achaguliwe yeye badala ya yule...kama ni muonekano tuuuu; what if ataonekana mwingine?

Ukiwa na cha ziada unakuwa more secured.

Huyo anayejisifu kujua kugegeda...what if akiugua magonjwa yanayotumia dawa kali ulijali wake ukapungua...?

Marriage is not only about sex wajameni...ni union ya mambo mengi saana unless mnazungumzia hizi za dot.com


Watu huwa wanaangalia sana mapenzi bila kukagua mabo mengine

Kuna ndoto zenu binafsi
Kuna ndoto za kifamilia
Kuna uwezo wa kukabiliana na changamoto
Kuna uwezo wa kutengeneza mahusiano mema na watu wengine

Ndoa ni maisha sio mapenzi!!
 
mi nilishakubali kuwa kilaza wen it comes ni wewe
lakini saasa sio kilaza kihivyo bana

Acha maneno mingi mama!
,hebu nielewesha hapa kweny bold unamaanisha nini!
elewesha mimi katika akili zangu za darasa la 2B sio za chuo kikuu kama zako!lol!
Haya mama

Unaweza ukampenda mtu lakini usiwe na mapenzi nae

Kwanza kupenda ni hisia chanya ya juu zaidi kuliko zote
Hii ni hali ya kumkubali YOYOTE BILA SHARTI LOLOTE na huyu ni MTU YOYOTE SIO LAZIMA AWE MUME AU MKE
Mfano:mwanao unaweza kumkubali[kumpenda] hata kama ni kilaza darasani,hakuelewi unapomuelekeza[simaanishi usimuadhibu anapokosea]
Rafiki yako unamkubali hata kama hana hela au ni mlemavu au ana hasira sana[simaanishi usimkosoe]

Hivyo kwa ufafanuzi wangu huu unaweza kuona kuwa unaweza kumkubali mtu kama alivyo[binadamu] lakini usiwe na mapenzi nae [tazama ufafanuzi wa mapenzi hapo chini]

Unaweza ukawa na mapenzi na mtu lakini usimpende
Ampenzi
Hii ni hisia ambayo mtu anakuwa nayo kwa mtu wake wa karibu sana mke/mume,kaka,dada,mama n.k
Hapa elewa kuwa kupenda ni kumkubali mtu bila kumbagua lakini mapenzi kuna kama ubaguzo hivi kwasababu unaweza kwenda kumnunulia chakula mtu uliekutana nae barabarani kwa kuwa ni binadamu mwenzako[upendo] lakini ukashindwa kulala nae chumba kimoja[mapenzi] kwa kuwa hujui hasa kama anaweza kuwa ni mwizi ama la

Nadhani nimejitahidi kuelezea vya kutosha
Mambo mengine ni vigumu kuelezea kwenye maandishi hadi uwe na taaluma hiyo[uandishi wa habari au mwalimu]
Lakini kuna mengine hayaelezeki kabisa!
 
hata hivyo ukimpenda mtu una vigezo vyako na ndio sababu zenyewe hizo.
 
hata hivyo ukimpenda mtu una vigezo vyako na ndio sababu zenyewe hizo.

Sijakuelewa

Kwanza kumpenda mtu hakuhitaji vigezo
Mapenzi nayo hivyo hivyo
Kumchagua mtu ili awe rafiki yako kwaajili ya ngono kuna kigezo kimoja tu nacho ni kuwa awe na jinsia ya tofauti na yako
Ila ili mtu awe mkeo/mumeo kuna vigezo zaidi ya kimoja kwa sababu unafanya jambo linalokusanya mabo mengi sana
Mwenza wako akiwa mlevi ndoa haiendi
Akiwa mkorofi ndoa haiendi
Akiwa mfujaji wa kipato ndoa itawashinda
Vurugu ziko nyingi sana,ukimpima kwa mapenzi[kingono] zaidi mtaishia kuja hapa kuanzisha uzi wa kulalamika

Ndoa ni jambo lenye mambo mengi sana kulitazama
Ukienda pupa kwa mapenzi utaishia kujilaani na kuwalaani wenzako tu!
 
Ndoa zina mambo mengi sana...kuna kaka mmoja mkewe ni mkarimu sana na alisomea kupika basi anajua kupika kupita Sheraton. Basi yule kaka kwa kukaribisha watu kwake...yani yuko proud sana na mkewe...tena anakwambia kabisa Nyumba kubwa karibuni dinner kwangu....mkisifia msosi basi utamsikia...'Panga siku wife akufundishe kupika' ...Huyu kaka mapenzi kwa mkewe hayachuji kwa kuwa hata jamii inamkubali mkewe...yuko proud saaana kwa watu...kwa ufupi anamringishia mkewe kwa watu vibaya mmno. Kwa hiyo nakubali jamii ikimkubali mkeo inakufanya kila siku nawe ukumbuke kuwa she is special
Watu huwa wanaangalia sana mapenzi bila kukagua mabo mengine

Kuna ndoto zenu binafsi
Kuna ndoto za kifamilia
Kuna uwezo wa kukabiliana na changamoto
Kuna uwezo wa kutengeneza mahusiano mema na watu wengine

Ndoa ni maisha sio mapenzi!!
 
[SIZE=-1]well said mkuu we need to think about other stuff.
nitazingatia daima coz cwez kukurupuka kama naenda toilet vile[/SIZE]
[SIZE=-1]

[/SIZE]
:disapointed::disapointed:[SIZE=-1]
"It is commonly a weak man who marries for love."
[/SIZE]
Samuel Johnson[SIZE=-1]
[/SIZE]
 
Sijakuelewa

Kwanza kumpenda mtu hakuhitaji vigezo
Mapenzi nayo hivyo hivyo
!
hivi unaweza kumpenda mtu bila kuwa na sababu mbili tatu zinazokuvutia kwa huyo mtu? basi wengine tuna vigezo vyetu vya kupenda. lol
 
Ndoa zina mambo mengi sana...kuna kaka mmoja mkewe ni mkarimu sana na alisomea kupika basi anajua kupika kupita Sheraton. Basi yule kaka kwa kukaribisha watu kwake...yani yuko proud sana na mkewe...tena anakwambia kabisa Nyumba kubwa karibuni dinner kwangu....mkisifia msosi basi utamsikia...'Panga siku wife akufundishe kupika' ...Huyu kaka mapenzi kwa mkewe hayachuji kwa kuwa hata jamii inamkubali mkewe...yuko proud saaana kwa watu...kwa ufupi anamringishia mkewe kwa watu vibaya mmno. Kwa hiyo nakubali jamii ikimkubali mkeo inakufanya kila siku nawe ukumbuke kuwa she is special


Kuna ukweli mkubwa kwenye maneno yako

Ili ndoa iwe imara na ya furaha kuna mambo mengi sana ya kuzingatia

Siku hizi ni kama watu hawajui ni kwanini wanaoana!
 
hivi unaweza kumpenda mtu bila kuwa na sababu mbili tatu zinazokuvutia kwa huyo mtu? basi wengine tuna vigezo vyetu vya kupenda. lol

Dah!

Inaonekana hujasoma kabisa nilichoandika
Hebu rudia tena!
 
Ni mada nzuri Mkuu Eiyer, ni kweli kuna mengi ya kujifunza kuliko mapenzi kupelekea ndoa. Nafahamu watu ambao wali-ignore masuala ya imani zao za kidini kwasababu tu walipendana lakini baada ya kuoana na kuzoeana na mapenzi kuchuja, imani zao za kidini ndio zilikuwa source ya mfarakano wa ndoa yao.
 
Back
Top Bottom