Msifunge ndoa kwasababu 'mnapendana'

Msifunge ndoa kwasababu 'mnapendana'

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Leo ni jumapili karibu asilimia kubwa ya walioko kwenye mahusiano yoyote watakutana leo
Hebu kwa wale mnaokutana leo jaribuni kujiuliza hili:

Hivi mapenzi tu ndo ynatosha kutufanya mimi na wewe kuoana?

Binafsi kuna kitu nimejifunza kwenye haya mambo
Watu wanaoana kwakuwa wana hisia hizi
Kila mmoja kwa mwenzake lakini baada ya muda wanaachana au wanaishi kwenye ndoa ya kimazoea tu huku kila mmoja akiwa na mahusiano nje
Kwanini?


FIKRA ZANGU KUHUSU HILI:
Mapenzi ni hisia tu kuna wakati zinatoweka na hapa zinapotoweka ndipo matatizo huanza,mimi nadhani inatakiwa watu kabla hawajaoana wanatakiwa wawe na kigezo zaidi ya hiki
Ndoa ni mahusiano ya maisha yote sio kipindi fulani tu hivyo unapoamua kuoana na mtu ni bora ukajiuliza kuhusu maisha yako yote yaliyobakia kuanzia hapo unapofunga ndoa

Mimi nadhani kuna jambo la muhimu,nalo ni mtazamo wa kila mmoja kuhusu maisha zaidi,hapa kunakuwa na mambo mengi sana kama vile malengo ya kimaisha,mazingira,familia na zaidi imani za wahusika n.k

Hua inafikia mahali wanandoa wanakuwa hawaitaji tena mapenzi kwa wenza wao kama kiunganishi kilikuwa ni hicho tu mahusiano yao yanayumba na kunakuwa na ufa mkubwa sana baina yao

Ni muhimu kuwe na zaidi ya kitu kimoja kinachowaunganisha,na kitu hiki kinatakiwa kisiwe ca muda mfupi,mapenzi yamekuwa kama ni kigezo cha mtu kuoana,lakini nyakati za mababu zetu walitazama mambo mengi sana
Kuna bibi mmoja aliniambia wakati anachumbiwa wale wapelelezi walikuja kukagua kama anaweza kufanya kazi[kulima],ana heshima,anajua kupika n.k

Nyakati hizi ni kama mapenzi hayakuwa kigezo na watu walizeeka wakiwa kwenye ndoa

Hebu jaribuni kujiuliza hili!!!!!!!!!
 
changamoto ni nyingi sana katika ndoa.
Na ni ngumu sana kuzitolea majibu mepesi.
lakini mapenzi na upendo ndio kigezo kikubwa zaidi kikiambana na FURAHA.
Mana ni rahisi kwa mtu anaekupenda kukuvumilia,ni rahisi kukusamehe makosa yako.
MAPENZI ,UPENDO NA FURAHA vinapungua ama kukata kwa sababu pia.
Mfano mpenzi wako anaweza kukuvumilia tabia asiyoipenda,badala ya kuacha unaendelea,inafika wakati anakata tamaa kukubadilisha anaanza kuishiwa upendo na furaha na hapo kuna ndoa za wengine anazitamani kwa mtazamo wake.HAPO AKIPATA MTU AKAJIONA MWENYE FURAHA NDIO MAMBO HUHARIBIKA KABISA.
mimi vigezo vyangu ni kama ifuatavyo.
1.uzuri ndio nambari moja(plus usafi)
2.tabia mjema(hili ni pana)
3.awe na heshima kwa kila mtu
4.mpole
5.asiwe mbaguzi(mf hatakiwi kuwa mchoyo)
7.MAPUNGUFU YAKE LAZIMA NIYAJUE NA NISIPOYAJUA HAPO BADO SIJAMUA KUMUOA HATA MPAKA KESHO.
sababu ya mapungufu ndio huvunja ndoa nyingi.
UNATAKIWA KUJUA MAPUNGUFU YAKE ILI UJUE KAMA UNAWEZA KUYAVUMILIA MUDA WOTE WA NDOA,mana haya huwezi kuyaondoa kamwe
 
Hakuna binadamu asieweza kuishi bila binadamu mwingine



Binadamu yoyote anaweza kuishi bila mahusiano ya kimapenzi achilia mbali kuishi bila binadamu!!!!

^^
Ndivyo ilivyo ktk mapenzi,,ni ngumu kuishi na msiependana.
From ur heading,,Kama mnapendana msiingie ktk ndoa? Maana yake nitafute tunaechukiana?
Asiyekusitiri mchana Usiku hataweza.
^^
 
Baadae binadamu anaona kuwa aliyenae si chochote wala si lolote na kwa kuwa hamna upendo wa dhatio na uvumilivu basi inakaua ndoa ndoano.
 
^^
Ndivyo ilivyo ktk mapenzi,,ni ngumu kuishi na msiependana.
Narudia tena hakuna hiyo kitu
Mtu ukishaanza kusema huwezi kuishi bila mtu mwingine wewe unakua na maradhi ya utegemezi wa hisia
Unakuwa unahitaji tiba

From ur heading,,Kama mnapendana msiingie ktk ndoa? Maana yake nitafute tunaechukiana?

Soma mada nzima utaelewa!
Asiyekusitiri mchana Usiku hataweza.
^^

Unamaanisha nini?
 
Narudia tena hakuna hiyo kitu
Mtu ukishaanza kusema huwezi kuishi bila mtu mwingine wewe unakua na maradhi ya utegemezi wa hisia
Unakuwa unahitaji tiba



Soma mada nzima utaelewa!


Unamaanisha nini?

^^
Eiyer unataka tu-reason philosophical wise,,lakini unapokuja ktk mapenzi,,mapenzi hayahitaji nguvu sana ya kufikiri.
Yanatokea tu,Yanakua,Yanatoa matunda,Yanakufa wakati unapofika.
Sasa,nafasi ya kupendana ikitokea tuitumie vema,,maana hata maisha na fujo zake zote yana hatima yake.
^^
 
Last edited by a moderator:
^^
Ishi na ambaye huwezi kuishi bila yeye,,usiishi na ambaye unaweza ishi bila yeye.
^^

Hakuna mtu yeyote asiyeweza kuishi bila mtu mwingine ambaye wamekutana ukubwani. Those are poor minds illusions and lack of stability. Katika umri fulani kila mtu huishi akiamini hivyo. later on, as you grow old and matured utaona kuwa yote hayo yalikuwa vichekesho vya akili za kitoto.
 
Mapenzi kwanza! !!!!!

Kwani hupendi ukiwa hayawani bali ukiwa timamu kichwani na vigezo vyako kwa hiyo utapenda tabia,uelewa wa mtu,na mengine baada ya kuwa umeona appearance na kufanyia kazi yasiyoonekana!!!!!

Ila nimejifunza badae kuwa interest za mke na.mume sio lazima ziwe mutual kwani mmoja aweza kuwa enterprising mwingine john kisomo imagine mtu ana masters lakini ukisafiri hata kitabu cha dukani hawezi kukifanyia haki!!!!!!Hapo ndo mbinde huanza yaani unaweza jiona ulikosea kumbe ni interest missmatch kumbuka hukuoa/kuolewa na shopkeepper so kubali kuwa sio inerest yake na endelea na maisha regardless kuwa ni kipato chenu wote!!!!!
 
^^
Eiyer unataka tu-reason philosophical wise,,lakini unapokuja ktk mapenzi,,mapenzi hayahitaji nguvu sana ya kufikiri.

Hapa ndipo tunapopotelea wengi
Kwanini tusifikiri?
Yanatokea tu,Yanakua,Yanatoa matunda,Yanakufa wakati unapofika.
Sio kweli
Kwanini usiwe na hisia za mapenzi na yoyote kama yanatokea tu?
Hakuna kinachotokea tu,kila kitu/hisia zina sababu ya kuepo au kutokea
Ukiwaza kwa namna ya kisirani utapata hisia za hasira
N kwenye mapenzi nako ni hivyo hivyo

Sasa,nafasi ya kupendana ikitokea tuitumie vema,,maana hata maisha na fujo zake zote yana hatima yake.
^^

Hii haimaanishi tusiutumie uwezo wetu wa kufikiri!
 
Ukweli unabaki pale pale.. Hapa duniani hakuna mtaalamu wa ndoa.
Kuna wanaooana kwa mapenzi.. ndoa zinawashinda
Kuna wanaooana kwa mapenzi.. ndoa zinadumu
Kuna wanaooana bila mapenzi... ndoa zinawashinda
Kuna wanaooana bila mapenzi.. ndoa zinadumu
Kuna wanaoendana tabia kama mapacha.. ndoa zinawashinda
Kuna wasioendana kabisaaaaa.. ndoa zinadumu
Kuna wanaoishi kwa mazoea.. ndoa zinadumu
Kuna ambao hata hawajui kwanini walioana.. ndoa zinadumu!
Kuna wanaochunguzana miaka kumi.. ndoa zinawashinda
Kuna ambao hawaoani kabisa.. wanaishi tu.. miaka nenda rudi hawana tatizo.. wako happy
Kuna wanaokutana na kuoana ndani ya miezi miwili.. ndoa zinadumu.....nakadhalika.. nakadhalika.
AND VICE VERSA

Bottom line:
1. Kama unataka kuoa/olewa fanya hivyo pale utakapohamua. Kama hutaki/hujaamua ACHA.
2. Kama uko kwenye ndoa, live each day as it comes. Enjoy the moment
3. Kama ndoa yako ina amani, mshukuru Mungu wako.. usiseme ni kwasababu nilifanya hivi.. au nilifanya vile..
4. Ukioa/olewa ishi the best way unavyojua wewe. The end will justify the means
5. Mwisho, kumbuka ndoa ni ARTIFICIAL sio natural. Naturally, binadamu hauko wired kuishi na mtu mwingine for the rest of your life.
 
Hakuna mtu yeyote asiyeweza kuishi bila mtu mwingine ambaye wamekutana ukubwani. Those are poor minds illusions and lack of stability. Katika umri fulani kila mtu huishi akiamini hivyo. later on, as you grow old and matured utaona kuwa yote hayo yalikuwa vichekesho vya akili za kitoto.

^^
Kupendana kunahusisha wawili,,kupenda ni upande mmoja,,kupendwa ni upande mwingine.
Je si bora sasa,kuishi na ambae mnapendana kuliko kutegemea kupenda tu au kupendwa tu?
^^
 
Back
Top Bottom