ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,699
- 9,462
Habari wadau wote
Kuna nyakati mbalimbali tunazopitia katika maisha yetu ziko nyakati za furaha , huzuni, kicheko, kupata na kukosa kuwa na kitu ama kutokuwa nacho, kuwa pekee au kuwa na watu, kuwa mtu wa juu ama wa chini yote katika maisha yapo hivyo huna budi kupambana na kujifunza na kumshukuru Mungu kwa yote upitiayo
Yawe mambo ya kutia moyo au kukatisha tamaa wewe mshukuru Mungu kwa kukupa uhai na afya njema, kuna ambao wako hospitallini hawajiwezi kabisa hawana tumaini lakini katika kipindi hicho huna budi kumshukjru Mungu kwani ndiye atupae kuishi na kutoishi pia ndiye atuondoleae wapendwa wetu ama atupae wapendwa wetu shukrani za kwa Mungu milele.
Hivyo huna budi kumshukuru Mungu kwa hali zote unazopitia hata kama unakosa chakula au unapata chakula, wewe jifunze kumshuukuru Mungu
Tunavyoenda kufunga mwaka huuu angalia mangapi ambayo Mungu amekutendea, mangapi ambayo amekulinda , je umemlipa nini Mungu kwa pumzi unayopumua, uhai , jifunze kurudisha shukrani kwa Mungu aliyekuumba sema asante Mungu kwa kuwa wewe umwema kwangu
NIWATIKIE MWAKA MPYA MWEMA WENYE BARAKA NA FURAHA NA AMANI TELE TUWE WATU WA SALA KWA MWAKA UJAO 2024
Nawapenda sana mabestito wangu wa jf
Wasalaamu;
Ladyf aka mama mfundaji
Kuna nyakati mbalimbali tunazopitia katika maisha yetu ziko nyakati za furaha , huzuni, kicheko, kupata na kukosa kuwa na kitu ama kutokuwa nacho, kuwa pekee au kuwa na watu, kuwa mtu wa juu ama wa chini yote katika maisha yapo hivyo huna budi kupambana na kujifunza na kumshukuru Mungu kwa yote upitiayo
Yawe mambo ya kutia moyo au kukatisha tamaa wewe mshukuru Mungu kwa kukupa uhai na afya njema, kuna ambao wako hospitallini hawajiwezi kabisa hawana tumaini lakini katika kipindi hicho huna budi kumshukjru Mungu kwani ndiye atupae kuishi na kutoishi pia ndiye atuondoleae wapendwa wetu ama atupae wapendwa wetu shukrani za kwa Mungu milele.
Zab 136:1-25Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele. Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Hivyo huna budi kumshukuru Mungu kwa hali zote unazopitia hata kama unakosa chakula au unapata chakula, wewe jifunze kumshuukuru Mungu
Tunavyoenda kufunga mwaka huuu angalia mangapi ambayo Mungu amekutendea, mangapi ambayo amekulinda , je umemlipa nini Mungu kwa pumzi unayopumua, uhai , jifunze kurudisha shukrani kwa Mungu aliyekuumba sema asante Mungu kwa kuwa wewe umwema kwangu
NIWATIKIE MWAKA MPYA MWEMA WENYE BARAKA NA FURAHA NA AMANI TELE TUWE WATU WA SALA KWA MWAKA UJAO 2024
Nawapenda sana mabestito wangu wa jf
Wasalaamu;
Ladyf aka mama mfundaji