Hii ni hospital kubwa ya kimataifa inayohudumia watu kutoka maeneo mbalimbali nchini na duniani.
Kwa mujibu wa maelezo, ndio hospital ya mwisho ambapo mgonjwa akishindikana basi anapelekwa nje ya nchi. Maana yake inashikilia roho za wengi na ina mabingwa wa kutosha.
Ikumbukwe hii hospital iliboreshwa mno enzi za Magu na kuongezewa uwezo wa vifaa tiba na wataalam.
Lakini cha ajabu ni siku kadhaa sasa hospital haina huduma ya maji. Tahadhari ni kuwa ukienda na mgonjwa beba shuka maana hakuna mashuka, yote ni machafu.
Hali ni mbaya. Ummy hata kama unalijua hili najua linakuumiza ila yawezekana lipo nje ya uwezo wako.
Wakati huo Juma Aweso yupo Marekani anakula keki na Kikwete New York. Huku wengine wanaimba mama anaupiga mwingi.
Hivi na mvua hizi utasingizia nini sababu ya kukosa maji. Mungu anazidi kuwaumbua.
Mama nae yupo bize kugawa hela kwenye michezo. Hawa watu hawana uchungu na lolote sababu wanajua wao, watoto zao na wajukuu zao hawawezi pata huduma yoyote kwenye hizi hospital. Hizi ni za wanyonge.
Enzi za Magu aliweka utaratibu wa hawa viongozi kutibiwa pia kwenye hizi hospital.
Kwa sasa wanapishana angani kama chini moto unawaka(Benard Membe).