Mshitakiwa


Umenikumbusha dada mmoja alikuwa anafanya kazi kwenye shirika fulani la wazungu halafu yeye akawa anawapeleleza Watz wenzake na kupeleka taarifa zao kwao. Kweli wale waliopelezwa walifukuzwa kazi lakini na yeye baada ya muda alifukuzwa kwa kuwa ilionekana asingeweza kuwa msaliti kwa Watz wenzake halafu akawa mwanifu sana kwako. ndiyo maana wanasema 'He who gossps to yuou will gossip about you'. Hata kama mtu anakuwa fundi wa kutoa siri za chama fulani kwa kingine kwa kepewa fedha eventually wale wanaopewa zile siri watamtenga kwa kuwa hawatajua ni lini atapewa fedha nyingi zaidi na kusema siri zao. Uaminifu na uadilifu ni bora kuliko usaliti.
 
Hoja yako nini mwanangu Nape Nnauye? Umeshazoezwa 'ku-copy' na 'ku-paste' basi tena.Haya ndiyo yanayofifisha kahadhi kako kalikobaki.Toa hata na maoni yako basi

Kichwa panzi kama Nape Nnauye ni ngumu sana kuelewa kuwa mustakabali wa muungano uko mikononi mwa raiya na sio kwa Maalim Seif wala Mrisho Kikwete.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Serikali tatu ni lazima hilo sio ombi na unatakiwa ulipokee na ulikubali na kulitekeleza sawa bwanamdogo
 
Mohammed Seif Khatibu naye simpendi kwa matusi yake aliyotoa pale Morogoro 21.4.2013.na kinachoonekana ni kuwa hawa wawili kuna mahala waliwahi kugongana.Haishii kumsema Maalim Seif.Wote nyie mna uozo uliopitiliza.
Na wewe Nape huu uzi umeona bora uletwe hapa ili upate uungwaji mkono.Mbona mengine huleti hapa na mkilipua mabomu kwa wanaowapinga hamuonekani jamvini.
 
Serikali tatu ni lazima hilo sio ombi na unatakiwa ulipokee na ulikubali na kulitekeleza sawa bwanamdogo
 
nepiiii! nngejua ww ndo umeandika hii post nsingesoma. nashukuru kama mnajijua kwamba ninyi ni wazandiki na wabambikizi wa kesi.
 
Kubadili mawazo kunakubalika tu, mbona hata jamaa mmoja hapa alishawahi kuanzisha chama baadae akageuka, mbona jamaa mmoja hapa ashawahi kutamba kuvua watu magamba lakini amepotezea?
 
sioni kosa la mshitakiwa, alikuwa bado kijana - wanasiasa vijana wanapita katika majaribu mengi hata huyu mleta hii sredi pia yumo majaribuni.

Huyu Nape si aliasi CCM na kuunda chama chao (CCJ) na Mzee 6 na Mzee wa TPA na TRC? Leo anahoji wenzake. Huyu si ndio aliye mzushia Lowasa ufisadi wa jengo la UVCCM baada ya yeye kuiba nyaraka nyeti za huo ufisadi, Leo anamfanya Seif anaonekane kituko. Kilichompeleka CCJ ndicho kilicho mpleka Seif aliko sasa. Nape, ungali kijana mdogo ukikua utabadilika tu
 
Nape ana busara sana

Wow...mtu akijamba tu ana busara. Sasa hiyo story aliyoweka Nape hapo ina busara gani? Soma story ya Steve Jobs alivyofukuzwa Apple na baadaye kurudi kwa kufanya mageuzi kwa wakati tofauti, kisha linganisha na hii stori.

Kila kitu na wakati wake, ingekuwa hivyo katiba zingeendeleakuwa hivyo hivyo zilivyoandikwa awali bila kufanyiwa marekebisho. Mabadiliko ya wakati huleta mabadiliko ya mazingira ingawa Lumumba LLC bado wanang'ang'ania logic ya Mwenge kuzungushwa all over the country while ukiwa umeshapitwa na wakati......
Kweli naona kuna busara hapo......
:A S wink:
 
1964 Kambona alimsaidia mkuu wa kaya wakati huo,akamwepusha na hasira za T.R na 1967 (Miaka mitatu tu baadaye) Mkuu wa kaya akamsaliti, na kumkimbiza nchi.
Kisiasa hayo yapo, wala si usaliti bali ndio mchezo wa siasa. kumbuka, richmond, mtoa taarifa ni mwanafunzi wa mshtakiwa, hadi akaachia nafasi yake ya juu kabisa serikalini. Kumbuka ulivyomshupalia avue gamba, na ngoja 2015 awe mkuu wa kaya. hapatatosha. hiyo ndiyo siasa. there is a rise and fall.
 
Amefilisika kisiasa Mohammed Seif Khatib hana mpya alobakia kutia fitna na sumu za Karne nyingi Ilizopita
 
Tusiruhusu akili ndogo kuongoza akili kubwa!

Yote aliyosema mwenezi ni utumbo na uharo mtupu maana hajaonyesha standing yake kama kijana msomi na anayeenda na wakati zaidi ya kubase kwenye porojo, fitina, uchochezi na ugamba



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Nape mleta Uzi Huu huna maana hata bure huuziki maana hujui ufanye nini maana nyote CCM ni wafa maji. Muulize Mohammed Seif Khatibu eti kweli ulikuwa ukipiga kigoma kwenye mikutano ya hadhara ya HIZBU na Baada ya UVAMIZI wa mwaka 1964 akabadilika akawa ASP mzuri tu. Nini hichi na yeye Kama Si unafiki wa kisiasa
 
Wote hao ni "system", wanaoneana wivu tu, "kwanini yeye si mimi?".

Kwani hayo huyajui Nape Nnauye?

kwani mkuu wewe hujui Nape Nnauye anatumika na wakati mwingine anaongea tuuu, iko wapi falsafa ya kujivua gamba?? sijui imeishia wapi, kwenye kikao cha CCM mkoa nikiwa mjumbe nimewahi kuuliza bila kupata majibu...
 
Last edited by a moderator:
Unajuwa huu ukumbi si zile maskani za vijana muliowanyima elimu na kuwaongoza katika propaganda za siasa chafu, fitna na fujo. Kwanza na tumjadili mwandishi wa hii article ambae ni Mhe Mohamed Seif Khatib na namna gani yeye mwenyewe aliandika shairi juu ya muungano na then tuweze kumpa benefit of doubt kama ni mtu msema kweli na mtetezi wa kweli chama na sera butu, au ndio kama anavyosema katika shairi lake hapo chini: Shairi la Mohamed Seif Khatib kutoka kitabu chake cha Wasakatonge shairi No 4 pg 3 :

KOSA?
1. Metufunga kamba,
Za miguuni,
Za mikononi,
Za midomoni,
Na kututosa baharini !
2. Eti mnataka,
... Tuogelee,
Tujongelee,
Tujiokoe,
Hadi tufike ufukweni !
3. Kosa letu kubwa,
Kudai haki?
Yetu miliki?
Mna hamaki,
Na huku mnatukashifu !
4. Msitunyanyase,
Siyo watwana,
Watu wa mana,
Tuloungana,
Kwa heshima na taadhima!

5. Sisi tuna kwetu,
Wenye asili,
Ilo kamili,
Na serikali
Ilopatikana kwa damu !
6. Kuheshimiana,
Kwa kupendana,
Kuelewana,
Kusikizana
Hilo tutakubaliana ! Waungwana hawa ndio akina Nape na genge lao, hili shairi aliliandika Mhe Mohamed Seif Khatib katika kitabu chake kinachoitwa WASAKA TONGE ..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…