Mshamba ni mtu wa namna gani?

Mshamba ni mtu wa namna gani?

Eddy Love

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2011
Posts
13,655
Reaction score
8,584
Je mtu akitoka kijijini akija mjini ni mshamba na je mtu asiyejua chochote ni mshamba na je anayeishi mjini anaweza akawa mshamba?

Je mshamba ni nani haswa?

Hebu tujadiliane kwa mapana.
 
Kwa maana ya asili mshamba ni mtu yeyote anaetoka kijijini(wakati huo kijijini palijulikana tu kwa kilimo-mashambani) na kufika mjini(kusiko na mashamba),kwa maana ya kisasa mshamba anaweza kuwa mtu yeyote ambae kwa wakati fulani anaonekana kutojua kitu fulani.
 
Mshamba = Mtu yeyote anayelishangaa jiji (jiji lolote) Iwe barabara,magari,maghorofa, n.k.
Lakini HASIYEJUA KUTUMIA KITU FULANI HUYU SI MSHAMBA.
 
Mtu kutoka kijijini anaweza kuwa na limited exposure lakini aimaanishi akishapata experience atabaki vile vile.

Binafsi nachukulia mtu mshamba ni yule anaejifanya anajua asichokijua, awe NY or Dar or Lindi ni mshamba tu.
 
Pole kwa kuwa wewe ni mshamba shamba la Mh Mbowe na genge lake, kwa sababu wewe ni shamba na ni mshamba uliuzwa kwa vi billion hahahaha, jamaa anakula mrija kwa kuku tu sasa washamba mkiwa mnamilikiwa na nyeupe hahahah
Sasa wewe unachocheka ni nini kama siyo ushamba, mshamba kiazi tu wewe!
"Vibilioni" unavijua?
Ushamba ni janga lingine kwa mshamba kama wewe...
Watu kama nyie ni "mazoba koko shamba
"
 
Naona tafsili nyingi zinaendana na neno mjinga sijui yanafanana ila yanamatumizi tofauti
 
Ni kasumba tu iliyojengeka.
Mshamba ni mbadala wa ugeni wa kitu fulani kwa muda.
Kwa mantiki hiyo kila mtu ni mshamba katika mazingira tofauti yasiyokuwa yake.
Mfano :wazungu ni washamba sana kuliko wamasia wa Ngorongoro au wazaramo wa Dar ni washamba sana kwa wakurya kule Tarime.
 
mshamba ni mtu yeyote ambae atatoa mchango wa kitu asichokijua hapa if, mwenye taaluma ndogo na maranyingi mtu huyo huwa kama bendera ipepeayo katikati ya kimbunga !!

siku nyingine ukichangia thread jaribu kutumia huo mviringo wako juu ya shingo bwana mdogo Eddy Love
 
Back
Top Bottom