Mshahara wangu

Mshahara wangu

Oooops!! jana nilipitia harakaharaka habari hii nikadhani ni Mheshimiwa Masa aliepata mkasa huu, kumbe sio.... sasa ule mwekundu wa msimbazi itabidi niusitishe!
 
Nziku, siyo Masanilo aliyepatwa na dhoruba hili ila ni rafiki yake. Lakini bado ushauri wa kuchukua taxi muhimu kama una pesa nyingi.

aah! kumbe, sasa kwenye post yake ya kwanza hajaeleza kwamba anamzungumzia mtu mwingine. Maneno yake yote yanaeleza 1st person, yaani anaeleza kukutwa na mkasa husika.
 
Never ever trust any body even yourself. Kila hatua unayochua plz calculate risk; mkuu 420 000 na daladala wapi na wapi, hata kama ni kiduchu ndio ukombe wote?

Plz ujifunze kukiogopa hata kivuli chako hapo utainua tahadhari yako = risk calculation
 
Oooops!! jana nilipitia harakaharaka habari hii nikadhani ni Mheshimiwa Masa aliepata mkasa huu, kumbe sio.... sasa ule mwekundu wa msimbazi itabidi niusitishe!

Usikonde mazee, ila twaweza iangamiza wote hata kwenye nyama choma na unywaji.....

Thanks thou!
 
Usikonde mazee, ila twaweza iangamiza wote hata kwenye nyama choma na unywaji.....

Thanks thou!

Kweli ningetamani ssana "TUKAE" najua watu wengi humu wana upeo na nivizuri sana kukutana nao......
Lakini Mhh, mkuu! haya magamba ya kobe tuliyovaa siyo rahisi kuyavua, tushasemasema mengi humu tusije "tukadugudwa!" Hata ile msimbazi ningetumia mbinu za UWT kukupatia nisingevua gamba langu kirahisirahisi!
 
"do not talk 2 strangers" maelekezo hayo tuliyokuwa tunafundishwa na wazazi wetu ni muhimu sana kwa nyakati hizi tulizonazo kuliko nyakati zozote.

Tusisahau kuwafundisha watoto wetu pia.

Pole Masa
 
Mkasa kama huu uliwahi kumpata mdada mmoja kwenye supermarket..akiwa ananunua mahitaji yake.
Inawezekana siyo nguvu za giza bali mauzauza ya madawa ya kulewesha.
Tujihadhari wakati wote, mahali popote kwa maana uhalifu unazidi kuwa sophisticated kila kukicha.
 
Kweli ningetamani ssana "TUKAE" najua watu wengi humu wana upeo na nivizuri sana kukutana nao......
Lakini Mhh, mkuu! haya magamba ya kobe tuliyovaa siyo rahisi kuyavua, tushasemasema mengi humu tusije "tukadugudwa!" Hata ile msimbazi ningetumia mbinu za UWT kukupatia nisingevua gamba langu kirahisirahisi!

Teh teh teh kwa kweli hili nalo ni issue kuna watu natamani kuonana nao ila haya magamba ni tatizo kubwa ...kumbuka sijawahi ona hata memba mmoja wa JF...huwa nahisi tu...!
 
Hii kitu OMBA MUNGU ISIKUKUTE BWANA!we angalia tu yanawakuta wengine

POLE NYINGI KWA MUATHIRIKA
 
Mimi kuna siku nilienda Kariakoo nilikuwa nimebeba mil. 1..nitazitoa mfukoni nikanunua vitu (hardware) kwa laki 6 ktk duka la Mwarabu..pia walikuwepo watu wengi wananunua bidhaa! Kisha ile laki 4 nikarudisha mfukoni wa rambo niliokuwa nimebeba.

Nilipofika home ..kuangalia ktk rambo ninakuta makaratasi tu..na sii pesa!

Hati leo sijui ile laki 4 ilipotelea wapi..na kwa nini nikakuta yale makaratasi!
 
Mambo haya yapo bwana, yakikukuta ndo utayaelewa vizuri, pole MzalendoHalisi
 
Mimi hizi naamini ni Ndumba tu haiwezekani mtu hujitambui kifahamu ukamabidhi mtu mwenyewe mshiko ingekuwa dawa ya kulevya mtu unapoteza fahamu au unazimia kabisa lakini hii wewe mwenyewe unamkabidhi bila shaka ni ndumba.
 
Mimi hizi naamini ni Ndumba tu haiwezekani mtu hujitambui kifahamu ukamabidhi mtu mwenyewe mshiko ingekuwa dawa ya kulevya mtu unapoteza fahamu au unazimia kabisa lakini hii wewe mwenyewe unamkabidhi bila shaka ni ndumba.

Haya ni mambo ya kimazingara, sasa abiria wengine hawakuweza hata kujua linaloendelea!!
 
Ushauri wa Mzalendo halisi ni sahihi kabisaa! Umebeba kitita chako cha mwezi kwanini upande dalax2?? Chukua taxi mara nyingine.
 
sasa kama una laki 4 na ushee mfukoni: kwa nini usichukie taxi ya 15,000 kukufikisha home? Kwa nini upande dala2 ya 300?

kweli wewe hujui kabisa maisha yaani mshahara wa 450,000 unataka kuuchukulia taxi ya 15,000. hiyo hela si itaisha mara moja lazima uwe na bajeti


swali la kuuliza je huo mshahara wa 450,000 unamtosha????

mwenyewe ameshakueleza kuwa mshahara wake ni mdogo na haumtoshi na anaenda kuutoa wote wewe unamwambia achukue taxi, atamudu vipi maisha
soma hapo kwenye maandishi mekundu mwenyewe anavyosema
Hi Team!

Hope you all fine. Jamani napenda kuwapa tahadhari wenzangu kutokana na kilichonipata Jana (sunday 31 May 2009). Ilikuwa hivi: Nilikwenda Mlimani City kufuata Salary yangu . Nilikomba kiasi chote (si mnajua pesa yenyewe kiduchu na daima huwa haitoshi). .
mtu anaepata 450,000 hana uwezo wa kuchukua taxi ya 15,000 labda awe na mgojwa maututi
 
Last edited:
Back
Top Bottom