Mshahara wangu

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Bongo kuna vituko, hebu soma kilichombuka huyu mwenzetu!


Hi Team!

Hope you all fine. Jamani napenda kuwapa tahadhari wenzangu kutokana na kilichonipata Jana (sunday 31 May 2009). Ilikuwa hivi: Nilikwenda Mlimani City kufuata Salary yangu . Nilikomba kiasi chote (si mnajua pesa yenyewe kiduchu na daima huwa haitoshi). Nikaondoka bila hata kuangalia left or right kuepusha tamaa ya jengo lile.

Baada ya kujipakia ktk daladala kuelekea kwangu TABATA. niliketi seat ya dirishani na mwanamke mmoja aged kidogo yuko kama lateforties (48,49....) . Baada ya kutoka pale kufika kituo cha superstar that aged woman waved her hand usoni kwangu. Suddenly my body was heavy, my lips went more heavier . I couldn't move a hand or anything. Nilistuka kituo cha RELINI (mwananchi) that woman alinigusa begani akaniambia NASHUKA KWA HERI then kama vile nimestuka usingizini nikamwambia OK.

There after fahamu zikanirudia kutazama my handbag iko wazi wallet yenye SENT zangu imefunguliwa na hakuna sent tano. Nikawaambia abiria wenzangu "nimeibiwa". Ilibidi driver asimamishe bus kusikiliza huo wizi na ikibidi bus liende police. abiria wenzangu wakanieleza kuwa mimi na that woman tulikuwa tunazungumza vizuri muda wote kama watu tunaofahamiana na hata manaeno yangu walinisikia nikimwambia huyo woman kuwa pesa ziko LAKI NNE NA ISHIRINI. kusema kweli nilikuwa na kiasi hicho kweli na ilinibidi kukubali kuwa ni kweli nimeshaibiwa kwa ushirikiano wa hali ya juu. kila mtu mle katika daladala hakuamini kuwa ati nimeibiwa na yule SHOSTI wangu. Wengine walidhani ninataka kuwatapeli na kuwasingizia. Kumbe muda wote mimi najiona mzito kufanya chochote lakini machoni kwa wengine nilikuwa kawaida tena very cooperative. Mshahara wangu wote umeondoka kwa that style.

My advice jamani wizi huu umefikia hatua ya ajabu zaidi ambayo sikuwahi kufikiria. Tahadhari za ziada zitakazokujia usizipuuze zitakusaidia Dunia imekuwa tambara bovu. Tumuombe Mungu atusaidie

Frankly speaking NIKO CHALI sio mchezo. mwezi huu nimefulia tena bila sabuni. Inaniuma sana kuwa nitaishije this month. Yote namwamchia MUNGU naomba awalinde na nyie pia wambieni ndugu jamaa na marafiki muwapendao wakao chonjo.
 
Lakini kaka mbona ulilewa mapema hivyo? siku nyingine uwe unpiga some konyagi au valuer hutalewa mapema hivyo
 
Pole sana mkuu, lakini huu wizi ni kiboko mwanawane, yaani wewe upo hoi lakini kadamnasi inakuona uko poa tuanyway nashukuru kwa somo lako
 
Pole sana daima kumbuka kusali haya mambo yatakuwa mbali nawe.

Kuna jambo moja huwa wanaliita chuma ulete hivi lipo? Maana kuna watu huwa wanapoteza pesa kimazingara mara baada ya kutoa chenchi au kulipia huduma au bidhaa...
 
Mkuu wangu Masanilo POLE SANA.Ila nataka kujua wewe Milimani City ulifika ukiwa unatokea wapi maana unawezekutuoa hii tahadhari kumbe huyu Shostito alikuwa amekulia timing muda mrefu,ila wewe umekuja kush2ka kakujeruhi.
Ili tujifunze zaidi 2uleze ulikotokea kable haujafika Milimani City.
Once again pole sana
 
pole sana ila nakushauri next time utembee na kitabu cha dini i.e biblia kama mkristo au Quran kama ni mwiislamu .. kuna versions hizi ndogo hata kwenye mfuko wa surual inakaa kwa ajili ya kinga kwani ulikutana na mfuasi wa shetani

Na ile revolver yetu ilienda wapi .. ungewatwanga wote
 
sasa kama una laki 4 na ushee mfukoni: kwa nini usichukie taxi ya 15,000 kukufikisha home? Kwa nini upande dala2 ya 300?
 
Ninachoweza kusema ni kuwa duniani kuna mambo mengi ambayo ni beyond scientific explanations. Juzi nilisafiri na mfanyabiashara kotoka mkoani ambaye alinisimlia jinsi ambavyo wanakuja Dar kununua mizigo ya dukani. Wanalipa hela kwa wenye mali hapa Dar let say 10 million halafu wakilejea kwao zile pesa walizolipa Dar zinawalejea huko mkoani na hasara inakuwa kwa mwenye mali maana atakapofunga mahesabu atakuta loss kubwa sana. Ni vijimambo tu vinavyoendelea hapa Tz.

Tuzidi kumwomba Mungu atuepushie mbali.
 
Pole sana Masanilo, lakini hizi ni nguvu za giza.
Unatakiwa kabla hujatoka nyumbani kwako ujiweke mikononi mwa Mungu na shughuli zako kila siku watu kama hao hawatakufuata hata kukusemesha tu hatathubutu, kwa kutumia imani yako.
Sasa utaishije na leo ndo tarahe 5 au una source nyingine ya income?
 
Pole sana Masanilo, lakini hizi ni nguvu za giza.
Unatakiwa kabla hujatoka nyumbani kwako ujiweke mikononi mwa Mungu na shughuli zako kila siku watu kama hao hawatakufuata hata kukusemesha tu hatathubutu, kwa kutumia imani yako.
Sasa utaishije na leo ndo tarahe 5 au una source nyingine ya income?

Asante sana mwezi utaisha tu ila cha moto kitaonekana!
 
jamani tupitishe kapu basi la kumchangia mwana JF mwenzetu sio tunapiga siasa tu
MKONO MTUPU HAULAMBWI
 
sasa kama una laki 4 na ushee mfukoni: kwa nini usichukie taxi ya 15,000 kukufikisha home? Kwa nini upande dala2 ya 300?


....Mkuu, Una Kijipointi hapo! Ukweli ni kwamba wakati mwingine Ubahili nao unatumaliza mno! Unakuta mtu anaenda kwenye ATM anavuta zaidi ya laki tano halafu akitoka hapo moja kwa moja kwenye Dala2 akiwa na imani kwa hakuna aliyemuona!!
jamani sina hela lakini nikikamata zaidi ya laki 3 mi nachukua Tax, potelea mbali kwamba huko nako kuna mengine!
Kwa Mkuu aliyetaka kujua huyo jamaa ya Masanilo (aliyeibiwa sio Masanilo ni Jamaa yake!) alikuwa wapi kabla. Ukweli ni kwamba timing nyingi zinaanzia kwenye ATM ambapo kuna watu utawaona kila siku maeneo hayo wakishangaa shangaa huku wakiangalia nani kavuta nini kutoka kwenye ATM! Ila hii ni Kali! Tujihadhari.
 
sio masanilo alietapeliwa..shem hawezi kutapeliwa na shori mwenye over 45 yrs sidhani kama atakuwa anavutia.....

....mashori wamekuwa wezi....ile bidhaa yao kitumbua siku hizi havinunuliwi..
 
sasa kama una laki 4 na ushee mfukoni: kwa nini usichukie taxi ya 15,000 kukufikisha home? Kwa nini upande dala2 ya 300?
mkuu kwa maisha haya ya siku hizi taxi si anasa? hizo laki nne ukidumbukiza mfukoni hakuna hata anayeweza kukudhania! laki nne yenyewe hata katikati ya mwezi haikufikishi then uwaze taxi, aaah jamani! mkuu haijawahi kukufika, hawa jamaa wa nguvu za giza wanaweza kukuvizia hata ukishashuka kwenye hiyo taxi then wakalamba chao....mkuu hawa jamaa hawafai...walishaniliza hata mimi, I wish ningekuwa na uwezo wa kuwakamata..ningewatafuna wabichi....pole masanilo
 
mkuu kwa maisha haya ya siku hizi taxi si anasa? hizo laki nne ukidumbukiza mfukoni hakuna hata anayeweza kukudhania! laki nne yenyewe hata katikati ya mwezi haikufikishi then uwaze taxi, aaah jamani! mkuu haijawahi kukufika, hawa jamaa wa nguvu za giza wanaweza kukuvizia hata ukishashuka kwenye hiyo taxi then wakalamba chao....mkuu hawa jamaa hawafai...walishaniliza hata mimi, I wish ningekuwa na uwezo wa kuwakamata..ningewatafuna wabichi....pole masanilo

Kiteitei,

Saa ingine ni ubahili tu!

Nakumbuka in 2001 tulienda Moro ktk seminar..basi tulikuwa kama 10 hivi toka ofsini..na kila mtu akapewa perdiem ya 210k (30k kwa siku 7). Guest nzuri wakati huo Moro ilikuwa ni 5-10 k (self). Basi jamaa yetu yeye kwa ubahili wake akachukua guest ya elfu 2 isiyo na self. Basi ktk kwenda kuoga..ile pesa ingine kama 200k hivi ilikuwa mfukoni..basi wapangaji wengine wakaziiba! reception wana sheria kuwa pesa au mali ya thamani uwape na wakupe risiti..yeye hakufanya hivyo! Hivyo hawakumsaidia!

Basi alilia sana..akawa hana kitu ikabidi chonde2 tumchangie!!

sasa kama una laki 2 mfukoni..kwa nini ulale guest ya elfu mbili??
 
mnasema kutembea na kitabu cha dini?wapo matapeli watakuambia wanakuombea feza iongezeke na hata aibu hawana wanabeba vitabu vya dini.shetani ana njia kibao tuwe imara jamaa na maombi.
 
Wanawake ni wezi cku hizi hakuna mfano,pole saana ndugu yangu na mungu akubariki kwa kufanya hivyo,yaani kutuelimisha.
 
Back
Top Bottom