Siku hizi watu mna Raha sana. Nakumbuka mwaka 1967 nikiwa darasa la sita baba alikua mwalimu huko usweken. Kulikua hakuna simu Wala Nini, mwisho wa mwezi ukifika mwalimu mmoja anatumwa kwenda wilayani kuchukua mishahara ya walimu wote. Watu walikua Ni waaminifu sana. Nakumbuka ikiwa zamu ya baba kufuata mishahara town lazima arudi na mikate na mchele.
Sio siku hizi eti kila jioni Ni wali.
Enzi zile hakuna pilau Wala biriani. Ni wali tu halafu Mimi nilikua najua wali hauliwi na kitoweo.
Tulipohamia Kisosora TANGA 1968 Niko la Saba ndio nikaanza kushangaa watu wa mjini eti hawezi kula wali hivi hivi bila samaki au nyama