Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,559
- 3,953
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime, amethibitisha kuwa hali ya usalama nchini ni shwari na salama, akiwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo vyao vya kupigia kura ili kutimiza haki yao ya kikatiba.
Akizungumza leo, Oktoba 29, 2025, kwenye kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1, Misime alisema hakuna tishio lolote la kiusalama lililobainika hadi sasa.
“Niendelee kutoa wito kwa wananchi wajitokeze bila hofu katika vituo vyao. Askari wapo kimsingi katika vituo vyote kuhakikisha usalama wa kutosha. Tutahakikisha kazi hii inafanywa kwa weledi, busara na haki kubwa ili wananchi watekeleze haki yao ya kupiga kura,” alisema Misime.
Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi limeandaa mikakati madhubuti kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu kote nchini.
Akizungumza leo, Oktoba 29, 2025, kwenye kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1, Misime alisema hakuna tishio lolote la kiusalama lililobainika hadi sasa.
“Niendelee kutoa wito kwa wananchi wajitokeze bila hofu katika vituo vyao. Askari wapo kimsingi katika vituo vyote kuhakikisha usalama wa kutosha. Tutahakikisha kazi hii inafanywa kwa weledi, busara na haki kubwa ili wananchi watekeleze haki yao ya kupiga kura,” alisema Misime.
Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi limeandaa mikakati madhubuti kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu kote nchini.