Sir John Roberts
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 9,639
- 15,970
Habari wana jukwaa la kimataifa. Hii ndio habari iliyotangazwa leo saa 2 usiku katika taarifa ya habari Azam. Msemaji wa serikali ya israeli ameutangazia umma wa watanzania kuwa mwili wa Joshua mollel aliyetekwa na kundi la Hamas tarehe 7.10.2023 huko Israeli ulichukuliwa mateka na kundi hilo na kwamba kwa sasa eti mwili huo upo Gaza mikononi mwa Hamas.
Nina maswali machache sana ya kuuliza kwasasa.
1. Hamas waliwazaje kuuteka mwili wa mtu ambaye tayari wameshamuua ndani ya israeli na kumpeleka Gaza huyu mtu ana umuhimu gani sana kwenye hii vita? Tuzingatie waliuliwa 1400 siku hiyo
2. Tunavyofahamu mpaka sasa Gaza hakuna umeme , hospitali zimebomolewa je Hamas watakua wameuweka wapi mwili wa ndugu yetu ikizingatiwa leo ni siku zaidi ya 70 tangu auwawe? Je mwili bado upo?
3.kwanini Hamas katika taarifa zao za mateka waliokufa wakishikiliwa hawajamtaja Joshua?
Jamani naomba ndugu zangu nauliza haya maswali kwa nia njema tu sijaleta vita.najua watanzania hatupendi kuulizwa maswali lakini tujitahidi kufikiria mambo kwa kina hasa tunapokuwa ni watu wa kupokea taarifa kutoka nje.
Karibuni kwa mjadala wa kistaarabu. Moderators na Maxence Melo mkuu naomba wasifute uzi wangu tujadili tu mbona sijavunja sheria yeyote?
Ahsante.
Nina maswali machache sana ya kuuliza kwasasa.
1. Hamas waliwazaje kuuteka mwili wa mtu ambaye tayari wameshamuua ndani ya israeli na kumpeleka Gaza huyu mtu ana umuhimu gani sana kwenye hii vita? Tuzingatie waliuliwa 1400 siku hiyo
2. Tunavyofahamu mpaka sasa Gaza hakuna umeme , hospitali zimebomolewa je Hamas watakua wameuweka wapi mwili wa ndugu yetu ikizingatiwa leo ni siku zaidi ya 70 tangu auwawe? Je mwili bado upo?
3.kwanini Hamas katika taarifa zao za mateka waliokufa wakishikiliwa hawajamtaja Joshua?
Jamani naomba ndugu zangu nauliza haya maswali kwa nia njema tu sijaleta vita.najua watanzania hatupendi kuulizwa maswali lakini tujitahidi kufikiria mambo kwa kina hasa tunapokuwa ni watu wa kupokea taarifa kutoka nje.
Karibuni kwa mjadala wa kistaarabu. Moderators na Maxence Melo mkuu naomba wasifute uzi wangu tujadili tu mbona sijavunja sheria yeyote?
Ahsante.